Askari wa Jeshi la Polisi wakiwa wamewtia mbaroni baadhi ya watu wanaoshukiwa kwa uhalifu wa ukabaji na uporaji katika eneo la Jangwani jijini dar asubuhi ya leo, ikiwa ni katika kampeni kabambe ya afande kova ya kutokomeza kabisa mambo ya loba na ngeta katika eneo hilo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 19, 2009

    bora sasa tutalala salama, mana ilikuwa huthubutu kurudi home saa tatu na nusu, kuwahi asubuhi ishu, ngeta njenje, naomba mjipange tena muibukie mchikichini kuna dawa za kulevya simchezo, big up kova

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 19, 2009

    bomoweni hivyo vibanda vinatia aibu kati ya jiji, serikali ipige grader pote hapo, pawe level papandwe ukoka, pawe kama park ya uhuru.pakiwa wazi wezi watapunguwa

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 19, 2009

    Na pale Kituo cha daladala kinondoni studio upande wa kuelekea magomeni. Kuna vibaka wa kumwaga, kuna mmoja anavaa kofia na mkononi ashika kitambaa muda wote, ni mweusi hivi na kundi lake. kila siku wapo hapo mida ya jioni. Askari wa doria wanapita hapo wanawavuta pembeni na kuwauliza kama wana simu (walizoiba). halafu wanawaacha jamaa wanarudi kuja kuibia abiria tena.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 19, 2009

    Nafikiri Kova angeanzia na vibaka waliopo ndani ya jeshi lake. Hawa jamaa wanashirikiana na vibaka kwa vibaka kupeleka hesabu. Njia pekee ya kutokomeza loba na ngeta si zima moto ya kukamatakamata wakifika kituoni wanatoa chochote kitu na kuachiwa. Njia pekee ni kujenga kituo kikubwa cha polisi hapo Jangwani na kuwa na Polisi waaminifu.

    Ila huwezi pata polisi waaminifu kama unawalipa mshara wa laki moja wakati maisha ya Dar pango ni laki tano kwa mwezi. Wajengewe makazi mazuri hapo jangwani na atakaye bainika kushirikiana na kibaka tu anatimuliwa bila nini wala nini?.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 20, 2009

    Polisi wawe wanahamishwa. Wakishakaa town muda mrefu wanakua wasanii tu, wizi mtupu!
    Walipeni mishahara mizuri,wakae pahala muda mfupi wahamishwe kabla hawajawa socialized na vibaka.
    Ni mtazamo wangu tu lakini.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 20, 2009

    DAH HIYO BACKGROUND ILIVYO CHOKA KWELI BONGO KAZI TUNAYO,KAMA ALIVYOSEMA MDAU HAPO JUU AT LEAST WAPANDE UKOKA,NAMNA HII WATU NI BORA WABEBE BOX TUUUU!!GOVT OF TZ WAKE UP!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...