Marehemu Mzee S.P. Kallinga

Sisi watoto wa Familia ya Mzee S. P. Kallinga wa Jakaranda Mbeya kwa Huzuni kubwa tunapenda kuwajulisha wadau wa Globu hii ya Jamii popote pale mlipo kuwa tumeondokewa na baba yetu tuliempenda sana sana Mzee S P Kallinga.

Baba alifariki kwa Ugonjwa wa moyo Jumapili tarehe 14 June 2009 saa 5 asubuhi katika hospitali ya Rufaa Mbeya.

Kwa mapenzi makubwa na ushirikiano wa wapendwa mbali mbali tulifanikiwa kumpumzisha baba yetu mpendwa katika makaburi ya sabasaba Mbeya tar 17/06/2009.
Tunatoa shukurani zetu za Dhati kwa wale wote mlioshirikiana nasi kwa Hali na Mali katika kipindi hiki kigumu sana katika maisha yetu.

ASANTENI SANA
Bwana Alitoa na Bwana Alitwaa
Jina Lake na Lihimidiwe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 06, 2009

    Poleni sana jamani...Tuliksikia msiba wa mzee wetu! tulihuzunishwa sana na msiba huo...Sisi tuliokulia Mbeya hasa maeneo ya Jakaranda na Uhindini tulimfahamu sana mzee Kalinga!! Poleni sana na Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya Marehemu mzee wetu

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 06, 2009

    Poleni sana Jamaa nzima ya marehemu. Mungu ailaze roho yake mahali pema amen. Je, Ni babake Sekela Kallinga aliyesoma Sisimba na Mbeya Day?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 06, 2009

    Poleni sana.. I am not sure if he was related to an old class mate at Sisimba Primary School, Sekela Kalinga.....Poleni tena....

    G.H.C

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 07, 2009

    Poleni sana kwa msiba huo mkubwa. Naikumbuka sana familia ya mzee Kalinga na hasa Mama Kalinga ambaye alinifundisha Mbeya Primary school (Mbalizi road)

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 08, 2009

    Ni kweli mmepatia ni baba yake sekela kallinga, tunawashukuru wote kwa ushirikianoo wenuuu wa dhati!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...