Na Mwandishi Maalum
Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Dkt. Augustine Mahiga atatunukiwa Tuzo ijulikanayo kama ‘ “The Spirit of the United Nations” kwa mwaka wa 2009.
Balozi Mahiga anakuwa mwana-diplomasia wa tatu kutunukiwa tuzo hiyo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2007.
Waandaji na watoaji wa tuzo hiyo ni Kamati ya Taasisi isiyo ya kiserikali inayojihusisha na masuala ya kiroho, maadili na mambo yanayo hususu ulimwengu katika ujumla wake (CSVGC-NY), ikishirikiana na taasisi nyingine isiyo ya kiserikali ya Umoja wa Mataifa inayo husika na masula ya mikutano na uhusiano.( CONGO)
Aidha kuanzia mwaka huu wa 2009 waandaji wa Tuzo hiyo ya “The spirit of the United nations”, wameamua iwe inatolewa kwa makundi matatu ambayo ni wana-diplomasia,wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, na wawakilishi wa taasisi zisizo za kiserikali ambazo zinauhusiano na Umoja wa Mataifa kupitia Kamati ya inayohusika na masuala ya Uchumi na Maendeleo ya Jamii (ECOSOC) au Idara ya Mawasiliano ya Umma (DPI)ya Umoja wa Mataifa.
Balozi Mahiga atatunukiwa tuzo hiyo Oktoba 26 katika wiki ambayo taasisi hiyo huadhimisha wiki ya kiroho, maadili na masuala yahusuyo ulimwengu. Maadhisho ya wiki hiyo yalizunduliwa rasmi mwezi Octoba mwaka 2007 kama sehemu ya kuendeleza utamaduni wa amani kama inavyotambuliwa ndani ya katiba ya Umoja wa Mataifa.
Kwa mara ya kwanza Taasisi hiyo ilimtunuku Tuzo hiyo mwaka 2007, Balozi Anwarul K. Chowdhury, (2007) aliyekuwa kwa wakati huo Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia masuala ya nchi maskini na zinazoendelea, nchi zisizokuwa na bahari, na nchi zinazoendelea za visiwa vidogo.
Balozi wa Pili alikuwa ni Balozi wa Kudumu wa Ufilipino katika Umoja wa Mataifa, Hilario G. Dvide, Jr. aliyetunukiwa tuzo hiyo mwaka 2008.Watunukiwa wote hao waliteuliwa kupokea tuzo hiyo kutokana na juhudi zao za kutangaza na kuendeleza masuala kiroho na maadili katika Umoja wa Mataifa.
Wanaopatiwa tuzo hiyo ni watu ambao pamoja na sifa nyingine wanatakiwa wawe wameonyesha kwa vitendo dira na maadili ya kiroho ya Umoja wa Mataifa kama ilivyoainishwa katika katiba ya Umoja wa Mataifa na Tamko la haki za Binadamu kama msingi mkuu wa kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa.
Aidha anatakiwa awe ni mtu ambaye amefanya kazi katika Jumuia ya Umoja wa Mataifa kwa takribani miaka mitano mfululizo.
Pongezi Dr. Mahiga. Tunakutakia kila la heri. Mdau Ahmed.
ReplyDeleteEti nasikia yeye ni Balozi wetu wa kudumu katika UMOJA WA MATAIFA.teh teh teh sasa sijui ni vigezo gani vinavyotumika katika serikali yetu ya Tanzania kuchagua hawa viongozi?!!!waosha vichwa wenzangu nisaidieni.Hongera kupata hiyo Tuzo
ReplyDeleteMdau-Ukerewe!!!
Pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Balozi! Tunafurahi kwa kuipatia sifa Tanzania. Mdau wa Ukerewe, uliza nini maana ya 'Balozi wa kudumu Umoja wa Mataifa' uelimishwe na siyo uulize swali lako kwa kebehi. Nafasi hiyo ina maana zaidi ya hivyo unavyofikirikuwa ni ya upendeleo. Ninatumaini utaeleweshwa na wenye kufahamu.
ReplyDeleteHongera kwa Dk.Mahiga. Kwa ufahamu wangu kidogo jina au neno la balozi wa kudumu ni kwa sababu tu ya tafsiri ya kiingereza kwa mabalozi wote wa umoja wa mataifa. Fuatilia http://www.un.org/members/missions.shtml utakuta zile ambazo kwa sehemu nyingine zinaitwa 'Embassy', kule UN zinaitwa 'Permanent missions', na kwa faida zaidi waingereza zao zinaitwa 'High comissions' na wawakilishi wa hizo sehemu wanapaswa kujulikana kutokana na jinsi ubalozi unavyoitwa, mfano Embassadors, Permanent repreentatives, na High comissioners. Kazi inakuja sasa ukifanya translations kwa kiswahili, maana inaweza kupotea. Kifupi yeye ni balozi tu kama walivyo wengine, na uchaguzi/uteuzi ndiyo uleule tu.
ReplyDeleteNawasilisha.
ale bela mnyalukolo..inguluvi itange hongera sana
ReplyDeleteila iyo ya balozi wa kudumu ata mie hainiingii akili kabisaa,tueleweshwe
MICHUZI WEWE UMENISTUA KWELI NILIVYO ONA PICHA NA MWANZO WA MANENO BALOZI AUGUSTINE MAHIGA BASI MIMI NIKA FIKIRI AMEAGA DUNIA...WEWE MICHUZI USIWE UNATUPA PRESSURE WENZAKO HATUZIWEZI
ReplyDeleteHiyo tafsiri ya habari haiko sahihi.
ReplyDeleteWewe mshamba hapo juu balozi wa kudumu ni jina linalotumika kwa mabalozi wote walioko UN, hata kama atakaa siku moja.
Michuzi hawa watu wengine uwe unawajibu huko huko, wanatuchafulia siku.
kabagabaho! kafanya nini cha maana???
ReplyDeleteKaka MICHUZI namjibu huyo annoy wa 20 oct saa 04:40:00 kama ifuatavyo.tuko katika blogu ya jamii kuchangia mada na wala si kukosoana PUMBAVU MKUBWA WEE.sasa kinachokushangaza ni nini mtu kuuliza maana ya ubalozi wa kudumu?!!.Kaka MICHUZI usinibanie post hii coment yangu ili huyo mdau aione alaaah.
ReplyDeleteMdau-Ukerewe!!!
Tuliowahi kufanya kazi na Balozi Mahiga tunajivunia heshima aliyopewa. Sio tu anastahili bali pia ni heshima kwa nchi yetu.
ReplyDeleteHuyu mzee alimpa vidonge vyake yule balozi wa marekani UN wakati wa Bush alikuwa anaitwa john bolton, jamaa ndiyo wale mlengo wa kulia kabisa. Nawapa homework wadau mtafute alichomwambia wakati muda wa john bolton umekwisha na hakuweza kupitishwa tena na senate ya marekani. Baada ya hapo nikamuheshimu sana....
ReplyDeleteWakuu hivi ukitaka kujiunga na chuo cha diplomasia kigamboni requirements ni zipi? Umri umekwenda lakini I wouldnt mind kuspend miaka 2 hivi pale, vilevile itanisaidia kujuana na future foreign ministers/presidents.
ReplyDeleteSIZANI KAMA KUNA BALOZI AU KIONGOZI WA AFRICA ANASTAHILI KUPEWA TUNZO YOYOTE DUNIANI...KWANI HAKUNA WANACHOSAIDIA AFRICA CHOCHOTE.
ReplyDeleteMDAU MONEY UK.
HILI JAMAA NI LINYALUKOLO LILILOKWENDA SHULE, KAMA MAREHEMU BALALI, ISIPOKUWA DR. MAHIGA HANA KASHFA YA KUIBA HELA ZA SERIKALI. DR. MAHIGA ALISHAKUWA BALOZI CANADA, MWAKILISHI KWENYE NGAZI ZA KIMATAIFA NA BALOZI NCHI ZINGINE. SOMA HABARI ZAKE ONLINE. MTANGLULIZI WAKE NAYE ALIKUWA MNYALUKOLO DAUD MWAKAWAGO. HUU SI UBALOZI NCHINI MAREKANI, BALI NI UN. BALOZI WETU USA YUKO D.C PALE.
ReplyDeleteAnon wa Oct 20 07:50 ninafikiri unamaanisha Chuo cha Diplomasia Kurasini. Ninavyofahamu umri siyo kigezo ila kuna programu ambazo sifa za kujiunga ni kuwa na elimu ya kidato cha sita au 'equivalent qualification' na zipo ambazo utahitajiwa kuwa na degree ya kwanza. Nilisikia kuwa wana mpango wa kuanzisha programu nyingine mwaka huu, ila sina uhakika. Kwa programu zote kuna kiwango cha kufaulu ambacho utategemewa kuwa nacho.
ReplyDeleteAsante kwa msaada wako anon wa Oct 21, 11:21:00 AM, nitajaribu kufuatilia. Nipo kwenye late 20s. Ila nadhani admission inaweza kuwa strict sana, sitashangaa kukuta nchi kama msumbiji na drc wanategemea chuo hicho hicho.
ReplyDelete