Juu na chini kijana Mlemavu, Eliabu Buliro Kamoga akimkabidhi Rais Jakaya Mrisho Kikwete zawadi ya sanamu yake, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere na Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin Mkapa wakati kijana huyo alipokuja kumuona Rais Kikwete ikulu ndogo iliyopo mjini Musoma,Mkoani mara.Kijana huyo ambaye alisema yeye ni yatima alimwomba Rais Kikwete ampatie msaada wa usafiri kutokana na hali yake ya ulemavu na msaada wa kulipiwa karo ya masomo ambapo sasa hivi anasoma katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru,Mkoani Arusha kwa kulipiwa ma wafadhili mbalimbali na kutokana na kazi zake za sanaa.Pembeni anayeangalia ni mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Mkuu wa mkoa wa Mara Enos Mfuru.

JK akipandisha bendera ya CCM muda mfupi baada ya kufungua Tawi la Wanachama CCM wa Maisha Plus, Kitaji,katika Manispaa ya mji wa Musoma.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Solution ya walemavu si kwenda kwa rais kuomba msaada. Tanzania ina walemavu wangapi? Ni walemavu wangapi ambao watapata nafasi ya kuonana na rais even hata kiongizi mwingine wa serikali?

    Solution taifa linatakiwa liwe na sera madhubuti ya kuwahudumia walemavu. Labda sera hii ipo maana walemavu wapo tangu siku nyingi na wataendelea kuwepo katika jamii.

    Taifa linatakiwa liwe na sera nzuri na pia sera hiyo itekelezwe kwa vitendo.

    Kikwete sijui kama amewauliza viongizi wa karibu na huyu kijana kama wanamtambua huyu kijana na kama walikwishafanya juhudi yoyote ya kumsaidia huyu kijana.

    ReplyDelete
  2. we anony Fri Oct 16, 05:10:00 PM hivi hujuwi kama kampeni za 2010 zimeanza? sasa rais asipomlipia huyo mlemavu na kumfunga mtoto kamba za viatu, unategemea kura zitatoka wapi?

    ReplyDelete
  3. huyo kijana hamfahamu rais wa awamu ya pili,alhaj Alli Hassan Mwinyi au anabagua katika hiyo sanaa yake?? pengine muheshimiwa Mwinyi ndo angempa msaada mkubwa ila kwa vile kambagua,itakula kwake...

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...