daraja la mungu juu ya mto kiwira wilayani rungwe
Kaka Michuzi,
naomba nikuletee hii kwa faida ya Watanzania wote!
Baadhi ya wafanyakazi wa DAWASCO tulipata nafasi ya kufanya ziara ya mafunzo kwa wenzetu ma Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Mkoani Mbeya UWASA tarehe 13 – 16 October 2009.

Tulibahatika pia kutembelea sehemu za kitaliii ambazo kwa kweli Wizara ya Maliasili na Utalii ikizitangaza, itakuwa ni sehemu ya kuweza kuliingizia Taifa letu mapato kwa namna Fulani!

Picha ya pili, tatu na nne ni sehemu inayoitwa KIJUNGU, wenyeji wanasema sehemu hii ni ya maajabu makubwa, maji hutumbukia hapo (pamekaa kama chungu) na hayaonekani huelekea wapi! inasemekana mtu akitumbukia eneo hili hawezi kuonekana hadia baada ya siku saba na tena baada ya kufanyiwa mila na wenyeji wa eneo hili,

Sehemu hii inasemekana aliwahi kutumbukia mtu mmoja tu na kutoka akiwa hai! Na alipotoka aliokoka na kuhama sehemu hii kutokana na maajabu aliyoyakuta humo ndani!

Picha ya juu inaonyesha sehemu ya maajabu mengine sehemu hii hiii, ni dalaja la ajabu ambalo linavukaa mto Kiwira! Wenyeji wanaliita daraja la Mungu

Mdau Lameck Victor Kashindye
Dawasco HQ

mdau akivinjari daraja la mungu
wadau chini ya daraja la mungu
wadau wakila pozi kwenye 'Kijungu'

juu ya kijungu





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. sasa mngeomba mungu hapo ili maji yaende mto Kizinga

    ReplyDelete
  2. Kaka Lameck ongera kwa trip ya huko Mbeya.

    Mimi nilisharudi machimboni kwangu huku.

    Kazi njema

    Kweba

    ReplyDelete
  3. uncle George nakuona unavinjari tu sasa kweli sio mchezo nimefurahi sana kukuona.. ha ha ha
    Rajabu[UK]

    ReplyDelete
  4. tanzania ina vivutio lukuki na tungekuwa wajanja km wakenya tungefunika vibaya-vibaya!!

    sema tu sijui nn jaman uwiiiii

    ReplyDelete
  5. Kijungu chenyewe mbona hakionekani?

    ReplyDelete
  6. naifahamu vizuri sana hii sehemu wakati nikiwa chuo magereza kiwira mdau usa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...