Ankal....
Embu angalia snow ilivyofanya noma Washington DC (Kisarawe).
Tulikua ndani tu siku mbili. Hiyo ya Reading mbona cha mtoto??
Mdau Mganga



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. Virginia huko ndani ndani ilikuwa about 3 feet.... it was craaazy! imagine mtu unachimba weeee, kuja kuangalia gari siyo lako, inabidi uanze tena...hadi mikono imeota sugu. But hey, it is winter time, AND I AM LOVING IT,I CAN NEVER TRADE SNOW OVER VUMBI KHA!

    ReplyDelete
  2. Wapi ! bora joto unaweza kuvua nguo, kwenye hiyo baridi vua nguo uone tehe tehe mpaka msuli wa nanihii unaganda bongo tambarareee mambo ya winta tunge kufa sie maana mvua ikinyesha mifereji inajaa dakika mbili mwenge hakupitiki sasa theluji si balaa?? Kweli Mungu yuko Afrika tunapeta tu vumbi hoyeee!

    ReplyDelete
  3. Afadhali vumbi kuliko huu upuuzi!Don't you question why they escap their home during cold season!!!
    Jambo la msingi ni kuboresha mazingira yetu. But our land has no comparison eeh!

    ReplyDelete
  4. Acha umbea! nyumbani ni nyumbani hata kama ni pangoni

    ReplyDelete
  5. Mimi hizi habari za barafu sasa mpaka zinani bore, inakuwa kama mashindano vile, tunajua kuwa mpo ughaibuni sawa,lakini si inatosha sasa,maana hata kwenye TV si tunaona jamani. Michuzi hebu achana ha hizi habari za barafu, barafu, barafu. hata hapa bongo barafu kibao, yaani frezer langu nyumbani limejaa barafu tupu subirini nitawapostia picha baadae

    ReplyDelete
  6. jamani acheni ushamba sasa. walioko hapo DC wameiona huna haja ya kuwaambia. waliopo nyumbani tanzania wanaziona kwenye TV kila kukicha habari za safari za ndege na train kusimama ulaya na marekani kwa sababu ya snow. halafu bongo siku hizi watu wanakuja sana ulaya na marekani si kama bongo ya nyerere mliyoiacha nyie na si kama nyie mmefika huko basi tena ndege hamzijui manake either mmejilipua au mnaishi kwa kuibia mnaogopa mkirudi bongo hamtakuwa eligible kurudi tena mamtoni. watu bongo wana hela sana siku hizi na wanakwenda mamtoni kutumia kama hawana akili nzuri. wale wasionazo na wenyewe siku hizi wamejaa ulaya wanaletwa na scholarships kama ford, nuffic, danish, british chevening, commonwealth, fullbright scholarship so siku hizi hakuna kuleteana hizo watu wengi wanaijua dunia vizuri cku hzi. halafu hiyo ya Reading na wewe mdau unatupostia vijibarafu gani hivyo hata ndani kwangu naviona kila siku hata wakati wa summer we hivyo umeona vibarafu navyo. hebu njoo hapa manchester, au liverpoo au newcastle uone maana halisi ya snow covers na watu washajizoelea sasa nyie kila kukicha na vidigital kamera vyenu snooo snooo, snoooo, snoooo hebu badilikeni kama sivyo bro michu anza kuzichinjilia baharini post zote za snow. ila ya huyo mbongo aliyeko home aliyeahidi kutupostia picha ya barafu za kwenye frizer lake usimtose mwache awaonyeshe watu kuwa snow hata bongo wanaziona. ni hayo tu
    michu nawe siku hizi umezidi kunibania poa lakini yote maisha nami ntaanzisha blog yangu halafu nikuibie wateja wote we haya tu.

    ReplyDelete
  7. Rahaa ilikuwa pale mko wawili ndani, hakuna kwenda kazini and kibaridi kunakufanya mlale pamoja siku nzima ... alafu ukute wife hana ketch-Up, raha iliyoje. Nahisi watoto wengi watazaliwa bada ya hii miezi 9 kwisha!

    ReplyDelete
  8. wewe annon wa 6:31 nakufagilia sana inaelekea umesoma na akili unazo za kuzaliwa.
    Comment yako ina maana sana na umewapa ukweli washamba dah I respect and like you.

    ReplyDelete
  9. Nyie wala vumbi you can't be us mpende au msipende watu tunakula maisha america tuna enjoy four season of the year kama hujui ....winter,spring,summer and fall wakati huko kwenu mnakula vumbi 24/7, 365 days vumbi na jua na wala siwezi kuuita hali hiyo summer naomba uipe jina mwenyewe like tanuru la moto eeeh stop bitching.
    Mdau USA

    ReplyDelete
  10. WIVU TU, ENDELEENI KULA VUMBIIII...

    ReplyDelete
  11. WEWE ANNON WA DEC 22, 06:31:00PM NAONA HUNA JIPYA,MAANA UMEANZA NA KUPONDA WENZIO KUHUSU SNOW HALAFU UNAWAAMBIA ETI WAJE LIVERPOOL,NEWCASTLE WAONE SNOW,INA MAAANA GANI?,AU NA WEWE UNATAKA KUONESHA UPO UK?.INAONESHA ULITAKA KUPIGA PICS ILA NAHISI CAMERA HUNA,MAANA KAMA UNGEKUWA NAYO BADALA YA KUONGEA NAHISI NA WEWE UNGETUWEKEA PICS HAPA.THANKS

    ReplyDelete
  12. malimbukeni wa mamtoni utawajua tu,hahahahaa kwi kwi kazi ipo adi izi ubongo za kibongo za wabeba box zitakapo kuja pata akili timamu,,
    annon 6.31pm una akili sana
    kwa taarifa tu ushatoa sina la kuongeza maana nilitaka niwatell apa ukweli,,,mbona kawaida saaaana?!!eti snooooow
    bongo oyeee,matanuzi mamtoni from bongo to mamtoni (returned) kwa raha zetu

    ReplyDelete
  13. We HELO unaelekea una uwezo mdogo sana wa kusoma kitu na kukichambua. mwenzako kasema snow huko manchester, liverpool nk ni heavy zaidi na watu washajizoelea hawaoni sababu ya kuzipigia kelele. hivyo ndivyo anavyosomeka huyo anoni wa 6:31 na si kushindwa kununua kikamera cha £300

    ReplyDelete
  14. msalimei tuma

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...