Stars United FC
Houston Serengeti Boyz


Na Ripota wa Globu ya Jamii, Houston
Timu ya Stars United F.C. inayoundwa na Wabongo wanaoishi state mbali mbali Marekani,wakicheza kandanda safi la uhakika lenye kiwango cha T.B.S.mbele ya haraiki wakazi wa Houston,waliojitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao,walijikuta wamepata kigugumizi la kutojua la kufanya baada ya dakika 20 za kwanza timu ya Houston (Serengeti Boys) kuchezewa nusu uwanja,huku wakifundishwa soka la kisasa, lililomfanya kocha wa Serengeti Boys kubadilisha takribani wachezaji sita kwa mpigo.

kunako dakika 10 ya mchezo Hadji Helper iliipatia Stars United bao la kuongoza baada ya beki ya kushoto Libe kupanda na mpira na kuachia kiki kali iliomgonga mlinda mlango na kumkuta mfungaji alieitumbukiza nyavu ndogo.
baada ya bao hilo Stars United iliendelea kuliandama lango la wapinzani kama nyuki,na kunako dakika ya 20 ya mchezo mcheji Gilles wa Stars united alikwatuliwa ndani ya eneo la hatari lakini kwa mshangao refa alipeta faulo hiyo.

Mechi iliendelea kuwa kali na ya kusisimua pale Houston(Serengeti Boys) walipopata bao la kusawazisha kwa mpira ulionaswa na mshambuliaji wa Houston baada ya makosa yaliofanywa na beki ya Stars United,baada ya kutegeana na kipa Ommy Guy na mpira kunaswa na mshambuliaji wa Houston na kufunga kirahisi.

katika dakika ya 44 ya kipindi cha kwanza,stars nao walifanya mabadiliko kwa kumtoa Haji na kumwingiza Evans na kufanya Rahim aliyekua akicheza beki ya kati kuchukua na fasi ya ushambuliaji,mabadiliko yalioipa Stars United Uhai zaidi kwenye safu ya Ushambuliaji iliopelekea Stars kupata bao la pili lilifungwa na mshambulaji Gilles alie kua mwiba kwa Houston,mpaka mapunziko stars walikua mbele kwa mabao 2-1.

kipindi cha pili kilianza taratibu kwa Stars United,huku Houston wakijaribu kutafuta goli la kusawazisha,kunako dakika ya 65 ya mchezo,Houston walipata kona na kupata bao la kusawazisha lililo lalamikiwa na wachezaji wa Stars kwa madai kipa alisukumwa,kwa mshangao Refa alilikubali goli na kufanya Stars united kuja juu na kuliandama lango la Houston kama nyati aliye jeruhiwa na kuweza kupata bao la 3 kunako dakika ya 79 ya mchezo.mpaka dakika 90 Stars United waliibuka kidedea 3-2 dhidi ya Houston.Hii timu imeonyesha mwanga na matumaini,ni timu nzuri inayocheza soka la kisasa,alisikika Kocha wa Houston akiisifia Stars United

Mechi hii ilikuwa ya pili ikifuatia mechi ya utangulizi kati ya Housto na Minnesota iliisha kwa Houston kuifunga Minnesota kwa 1-0,goli lililo leta utata na kutaka kugomewa na (Kili Stars)baada ya muamuzi kuipa Houston goli la tuta,kwenye dakika ya 89 ya mchezo,baada ya kocha wa Minnesota kuwabembeleza wachezaji na kuwasihi warudi uwanjani,baada ya dakika 90 ya mchezo Houston waliibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Minnesota.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. hahahaaaa dennis(dman) bado una kaba 3 pole umeshindwa walipita kwako nini.nice
    mdua ban2 y

    ReplyDelete
  2. Mfadhili wa timu Massawe(DC),hakikisha vijana wote wanapata viza za Sweden mwakani.Vijana wako si mchezo kwa kutandaza soka,tuliwaona hapa Houston.

    ReplyDelete
  3. Stars United mupunguze kuparty.Siku 3 Safari kwa Dj Issa,Rex mpaka asubuhi.

    ReplyDelete
  4. kuparty muhimu lakini tukiweka boli tambarare we mean bussines...tunajua nyakati zetu usijali

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...