
Hi ankal,
Leo asubuhi pale barabara ya kilwa road hapa Dar! Kwenye kipita shoto cha JKT Mgulani, jamaa aliona anachelewa kuzunguka! Akakunja hapo hapo kwenye tuta na kuaruka chwaaaap! Akawa kafika. Bongo Tambarare kama wanavyosema FFU wa Ughaibuni chini ya afande mkuu Ras Makunja. Na hapo hafanywi kitu...
Wape wadu hyo!
Mdau
Ekonjo
Sent from my BlackBerry® smartphone
Leo asubuhi pale barabara ya kilwa road hapa Dar! Kwenye kipita shoto cha JKT Mgulani, jamaa aliona anachelewa kuzunguka! Akakunja hapo hapo kwenye tuta na kuaruka chwaaaap! Akawa kafika. Bongo Tambarare kama wanavyosema FFU wa Ughaibuni chini ya afande mkuu Ras Makunja. Na hapo hafanywi kitu...
Wape wadu hyo!
Mdau
Ekonjo
Sent from my BlackBerry® smartphone
Huyo jamaa mwendawazimu bila shaka atakuwa ameamka na konyagi kichwani.maana chui chui haiwezi kumpagawisha kiasi hiki....dah kwa style hii lazima tuendelee kufa kama mbu.
ReplyDeletemdau Ekonjo, jinsi ulivyoelezea tukio hili, mie mbavu kushneh kazi yake. Kweli wachekeshaji mpo wa kutosha! LOH ha ha haha!
ReplyDeleteKwanini uogope kuvunja sheria wakati waharifu hawaadhibiwi? Alichofanya huyu driver ni kitu cha kipumbavu sana, na wadau wengi humu hawataipenda hii.
ReplyDeleteKwa akili ya kukurupuka, ningesema kwamba huyu dereva asiruhusiwe tena kuendesha gari, afungwe jela na apigwe viboko, na pia agharamie matengenezo yote ya uharibifu aliousababisha.
Lakini pia akili yangu inanisuta kwamba; kumpa huyu dereva adhabu kali wakati kosa lake ni dogo sana ukifananisha na makosa ya watendaji wakuu wa serikali yetu; raisi mstaafu, waziri mkuu aliyelazimika kujiuzulu, mawaziri walionunua rada kanjanja, viongozi wa EPA na RICHMOND na kadhalika. Kama wote hawa hawaadhibiwi, jee kumuadhibu dereva huyu itatosha kuleta "law and order" katika nchi yetu?
Jibu ni kwamba hapana.
Ingawa ukweli ni kwamba huyu dereva atapewa adhabu kali sana kwa sababu yeye siyo mtendaji wa serikali na wala siyo mteule wa rais kikwete.
Kwa mwenendo huu hatutafika kamwe
kwa kweli inavyo onekana ni kuwa hili lori lilikuwa linapita kwa kukimbia mizani halafu pili linaharibu njia mpya ambayo kwa kweli watanzania tutalipa mpaka vitukuuu vyetu haya madeni ya kujengewa barabara uhalali wa hapa ni kuwa gari litaifishwe na pili Tanroads wanatakiwa wachukue Insuarance ya gari hilo kwa malipo ya ukarabati wa hiyo njia maana baada ya lori kutolewa lazima pafanyike matengezo.
ReplyDeletemvunja nchi ni mwananchi,halafu kesho watu wanalalamika brbr zetu hazidumu,namna hii hatufiki popote
ReplyDeleteHizo "shoti-kati" zinatokea kila barabara bongo na nikila siku. Wenyewe (wabongo) wamezoea "kufaulisha"
ReplyDeletehahahaaa mi nilihisi tu lazima ukipita utai-snap hili lori. Nilipita late sana pale JKT nikalikuta, dah kweli pombe ya mnazi sio chai jamani..
ReplyDeleteEddymak
Aaaaii!!Imeniuma jamani. Dududu!!Hata kuthamini uzuri wa barabara? Natamani kutukana. Kudadadeki?**^""xx##
ReplyDeleteBongo kweli tambarare ukiwa na shs10,000 tu mfukoni unaweza kuingia na gari lako mpaka kizimbani mahakamani na polisi na hakimu watakuwa wanachekelea ulaji tu.
ReplyDeleteNIMEPITA MARA KADHAA SEHEMU HII NA HII BARABARA NI KATI YA BARABARA MBOVU KABISA KUJENGWA KATIKA MIAKA YA KARIBUNI JIJINI DAR ES SALAAM.
ReplyDeleteTAZAMA VIZURI NA UTAKUTA MZUNGUKO HUO NI MDOGO KWA LORI LA AINA HAPO JUU.VILE VILE VIZINGITI VYA MATOFALI(KERSTONES) NINDOGO SANA NA FUPI.
ZAIDI YA HAPO USIKU KWA VILE HAKUNA TAA, HAKUNA MABANGO YOYOTE YA KUONYESHA MBELE KUNA MZUNGUKO.
WIZARA YA MUINDO MBINU/TANROADS WAMEKABIDIWA BARABARA BOMU AMBAYO HAIKUPATA USIMAMIZI WA KITAALAM TOKA KWA WAHANDISI WETU.
LINGANISHA NA BARABARA ZILIZOJENGWA NA KONOIKE MIAKA 15 ILIYOPITA BARABARA ZILE BADO ZINADUNDA.
ebwana eeh Bongo noma December nilikuwa likizo Bongo madereva wote wanaendesha style hii hii manake nilishindwa kudirve mdogo wangu akawa yeye ndo ananidrive alivokuwa anafanya anajua mwenyewe manake nilikuwa najisikia aibu nafumba macho nifumbua sioni drive mwengine anayeshangaa kumbe nivitu vakawaida kudrive in icoming lane kucomeka u turn nk drive bila kuvunja sheria haoni raha
ReplyDeleteWadau kabla ya kulaumu inafaa kuuliza hilo tukio lilitokea saa ngapi.
ReplyDeleteKama ilikuwa usiku na kama mnavyoona hiyo round about haina reflectors (viakisi) dereva anaweza asione kwamba kuna round about hapo.
Na hilo ni lori, barabara swaafi imenyooka, ina lami, na usiku huwa hakuna magari mengi kwa hiyo dizaini dereva alikuwa amechochea mwendo hivyo akashindwa kusimama ghafla, ndio akaparamia tuta.
Hii! kamanda wa ffu wa Ngoma africa,haya tazama sasa kazi ya bongo tambarale yako? kweli bongo tambarale
ReplyDeleteAma kweli!! Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza. Kwenye ITV leo 21/1/2010 saa 12 jioni dereva wa lorry amehojiwa akasema; yeye alitoka Tanga na mgeni wa hiyo njia mpya, kulikuwa na daladala linakuja akakwepa na kujikuta amepack kwa lazima hapo. Nampongeza kwa hilo hakuwa na jinsi kwani ameokoa maisha ya walikokuwa kwenye daladala. Tafakari,,,,, kama asingefanya hivyo ingekuwaje? Hiyo barabara itatengenezwa kwa kodi zetu.
ReplyDeleteNatumai TANROADS watakuwa wameona hii na watarekebisha kabla hayajatokea maafa makubwa.
ReplyDeleteNi kweli ile roundabout imebanwa sana na hili pia wanatakiwa kulirekebisha.
Dereva hana kosa. Hamna kiashiria chochote cha kuonyesha kuna Round about. Ukiangalia kwenye picha alijaribu kufunga breki akaachia (alama za tairi barabarani). Angekomaa na kukata kona basi angeangusha lori. Nampa big up dereva kwa uamuzi wake wa kupanda kizunguko.
ReplyDeleteTANROADS, Alama ziko wapi?!!!!!!!!!