Align CenterNaibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, Dk. Maua Daftari (kushoto) akishuka katika ndege ya Shirika la ndege la Air Zara aina ya Ambraer 120 E ilipotua katika uwanja wa ndege wa Arusha ikitokea Dar es Salaam baada ya kuzindua rasmi safari zake katika miji ya Arusha na Zanzibar, ndege hiyo imetengenezwa nchini Afrika Kusini na inauwezo wa kubeba abiria 30.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Hapo hakuna ukweli kuhusu mahali ndege ilipotengenezwa.Embraer-nenda google tu utajua ilipotoka.Hongereni Zan Air.

    ReplyDelete
  2. Mdau wa kwanza si ungewaambia kimya kimya kuwa zinatoka Brazil, hata mimi nisingeona!!! Hongera Air Zara lakini msife mapema....

    ReplyDelete
  3. Hongera Air Zara. Lakini hizi Embraer 120 Brasilia(from Brazil) zina historia ya ku fail propeller kunakosababishwa na internal corrosion.Ndege mbili za zimeshaanguka kwa sababu hiyo, ingawa marekebisho yameshafanyika kuna uwezekano hizi ndege ni used na zikawa na matatizo hayo. Hivyo kikubwa ni inspection za mara kwa mara na kusiwe na uvivu kwenye matengenezo. Hongera sana

    ReplyDelete
  4. Msemo wa 'tunajifunza kwa makosa' umepitwa na wakati. Sasa hivi msemo ni 'jifunze kwa makosa ya wengine'. Air Zara jifunzeni kwa makosa ya Eagle Air, Community Airlines, Africa One (ile ya akina Musiba), Ile ya Zanzibar sikumbuki ilikuwa inaitwaje na ofcourse makosa ya Air Tanzania. Kwa nini kwa miaka 10 hadi 15 iliyopita Tanzania kampuni pekee ya kizalendo iliyofanya biashara ya usafiri wa anga masafa marefu Tanzania ni Precision Air peke yake? Mbona wengine wote niliowataja na niliowasahau hapo juu walishindwa? Wemgi akina Diallo walianza kwa makeke na mindege mikubwa bei poa safari za humu humu nchini ndani ya muda mfupi wakakwama na kuishia kimya kimya. Diallo sasa hivi kajificha huko Mwanza-Bukoba na kandege kadogo. Jifunzeni ka makosa ya wengine ili Precision apate upinzani bei zishuke huduma ziboreshwe zaidi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...