JK akimkabidhi ufunguo wa trekta ya mkopo Bwana Abdallah Thani,Mkulima wa Lalago wilayani Maswa wakati wa hafla ya uzinduzi wa programu ya Kilimo kwanza wilayani Maswa, Mkoani Shinyanga. Katika hafla hiyo matrekta kadhaa na power tillers zilikabidhiwa kwa wakulima kwa mkopo nafuu chini ya ufadhilki wa kampuni ya Al Adawi.
Mwenyekiti Mstaafu wa UWT Mkoa wa Shinyanga na mmoja wa waasisi wa CCM Bi. Jennyrose Kigola akimsalimia kwa hisia kali Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya kuwasili ikulu ndogo mkoani Shinyanga leo. Kushoto pembeni ya Rais ni mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
JK akiangalia wananfunzi wa shule mpya ya Sekondari ya Masengwa katika wilaya ya Shinyanga wakifanya jaribio la kisayansi muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuifungua rasmi shule hiyo jana mchana.Shule hiyo imejengwa kwa ufadhili wa kampuni ya uchimbaji dhahabu ya Barrick Gold inayomiliki mgodi wa Buzwagi mkoani Shinyanga.
JK akikagua mojawapo ya darasa katika shule mpya ya sekondari ya Masengwa wilayani Shinyanga muda mfupi baada ya kuifungua rasmi leo mchana.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Hayo ndio matrekta ya Massey Ferguson yanayofaa kwa KilimoKwanza maana yanaweza kumudu kazi ngumu za shambani hata miaka 50 bila matatizo makubwa.

    Mdau
    WaKilimo Kwanza

    ReplyDelete
  2. WATANZANIA TUACHANE NA KIINGEREZA KWANI KINAONEKANA HAKIWEZEKANI. kama tunaoweza kuingia kwenye blog ndiyo hivi wale wasioweza itakuwaje?

    ReplyDelete
  3. Mama salma anavyangalia kwa makini hapo mumewe alivyohug na huyo bibi

    ReplyDelete
  4. anon 0814 kiingereza kimetoka wapi?

    ReplyDelete
  5. Wewe bwana 0814 kiswahili ni ,kiarabu,kiingereza na bantu dialec, hakuna swahili tribe
    thank you .

    ReplyDelete
  6. HABARI HII ILIPOTOKA KWANZA ILIKUWA KWA LUGHA YA KIINGEREZA NA SASA IMERUDIWA KWA KUTAFSIRIWA KWA KISWAHILI NA SI HII TU ZIPO NYINGINE PIA ZILIZOBADILISHWA KUTOKA KIINGEREZA KUWA KISWAHILI.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...