Stars United F.C.(kandanda safi kiwango cha T.B.S.)inawatakia wote HERI YA MWAKA MPYA. 2010 uwe mwaka wa upendo na mshikamano. Stars United imeisha washa indiketa kulekea Sweden,

Salaamu zetu za mwaka mpya kwa Sweden ni kwamba mkae mkao wa kula,Stars United haiji kutembea,mjiandae vyema,sasa hivi tupo kwenye mazoezi ya kufa mtu,tunajua Sweden wana timu nzuri,tunajua tutapata upinzani mkali,lakini vijana wangu wamenihakikishia ushindi wa Sweden kwao itakua suluhu,wanaongea sana,wanapenda kucheza mpira na mdomo,

pamoja na kuwa na wachezaji wazuri,msisahau Stars United ni mkusanyiko wa wachezaji wa Marekani nzima sio kucheza mpira tu pia huzingatia kipaji cha mchezaji kwa maana nyingine kuanzia kipa mpaka wachezaji wa kusubiri ni MA-PELE. Yaani kontroli kuanzia ukucha mpaka unywele. Sasa sijui aanze nani asubiri nani. Nawaoneeni huruma sana. Sweden punguzeni mdomo na kuwatisha wachezaji wa Stars united. Msione wamekaa kimya, kumbe wanakuangalieni kihindi,mwezi wa saba sio mbali. Mmsije lia na kusaga meno.
Meneja
Stars United FC

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...