Mzee Michuzi,
Wakati wenzetu mnafikiria Flyovers, hii ndiyo hali halisi niliyoikuta katika barabara inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Rukwa, ambayo ni hodari wa kuzalisha chakula!!
Nina picha zaidi kama unaweeza nitafutie jamaa walio interested wanirudishie senti kidogo ya kunawia tope la Mkunda, Mpakani mwa Mpanda na Mbeya. Hilo basi ni la dereva aliyejitolea kupita njia ya hatari ili kuwahisha abiria wake! Hakuna greada bali kwa wanavijiji kukwamua magari inakuwa ajira yao ya msimu wa mvua!
Greetings
Sithole E. Mwakatage,
Mpanda.
emsithole@yahoo.co.uk
sanda mkobani...
hinya hinya...

safari yetu mbeyaaa..




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Wee Sithole, kweli wewe ni mkazi wa Mpanda!!! Watu wanazungumzia ya Dar es Salaam wewe unaleta ya Mpanda! Kama hujui utamu wa Dar tafuta jibu kwa nini hata serikali yenyewe imekuwa na kigugumizi cha kuhamia Dom baada ya yeye yenyewe kupitisha uamuzu huo takribani miaka 40 iliyopita!!! Ukipata jibu basi utakuwa umepata jibu la flyovers vs. njia za panya za Mpanda

    ReplyDelete
  2. NIMESAFIRI SANA HII BARABARA KAMA MIAKA 10 KABLA YA KUHAMIA DAR NA KISHA KUPANDA PIPA KUJA USA I AM VERY SAD ILA JE WALISEMA RAIS WA ZAMANI WA MAREKANI GEORGE W BUSH AMETOA PESA ZA KUJENGA HII ROAD ZIKO WAPI?

    ReplyDelete
  3. Mdau nĂ­ vizuri umetupa upande wa pili wa ROAD za TZ.Wengi wanaopendekeua flyovers hawajawai kutoka nje ya Kibaha.Kuna road muhimu zinatakiwa kujengwa kabla ya kufikiria flyovers.

    Hizo picha ziwasilishe ofisini kwa Pinda. wanaweza kukurudishia pesa za kunawa tope la mkunda:))

    ReplyDelete
  4. Mdau wa Sun Mar 14, 03:17:00 AM zile hela alizotoa G.W Bush zimetumika kulipia mishahara ya TRL na kununua hisa za RITES kwa hiyo wakazi wa Rukwa walie tu wataendelea kutaabika hivyohivyo hadi mjukuu wangu atakapokua mbunge umri sawa na Mzindakaya!. Maana Rukwa rami ipo kuanzia daraja la mto Lwiche hadi kule shule ya Kantalamba na toka stend hadi majengo kwa mzindakaya. Huo mkoa hautakiwi kuwa na rami kwani karibu nusu ya vijana wenyeji wa huko wamekua waganga sababu maisha magumu. We kwa mtaji huo unatarajia soda itauzwa bei gani? Au sementi toka Mbeya utaipata kwa bei gani ? Au nauli ya hilo basi la Sumry toka MBeya hadi Sumbawanga na Sumbawanga hadi Mpanda watakupiga shilingi ngapi kufidia hizo springi zao hapo? Na Mpanda si ndiko anapotoka Mheshimiwa Mizengo Kayanda Peter .....? Ila uongo si kazi Rukwa kuna kila aina ya Biashara unayoijua wewe. Kuanzia utalii, kilimo, uvuvi, madini, mbao,magendo kama ujangili,unga, wahamiaji haramu, wizi wa magari toka South Afrika,na bila kusahau uganga,na uchawi wa kulipizana visasi pia unapatikana kwa bei chee huko!.

    ReplyDelete
  5. huko mnatakiwa msikae tuhamie wote dsm, wabunge wajiuzuru wabaki wa dsm, huko tuombe japani watumie kutestia magari nadhani tutapata wawekezaji, jamaa hawana sehemu ya kutestia wale.

    ReplyDelete
  6. mdau tutangaze kuhamia dsm huko tutafute wawekezaji ili watestie magari bwana sio kuwekeza migodi tu, msosi tutaagiza AMERIKA, pia tutapata pesa ya kutosha na cha juu. SCANIA nathani wanaweza kuja au MAC INTERNATIONAL, VOLVO Hata japani najua hawana sehem nzuri ya test za magari yao AU wadau mnasemaje makofi tafadhari.

    ReplyDelete
  7. Mi sitoki Rukwa natokea uchagani ila naijua nje ndani kwa barabara rukwa!Hapa jamani serikali ione aibu ijenge hata mbeya-s/wanga tu,huko mpanda lyambalifipa,katavi kufate baadae!Tunduma na s/wanga kwa sasa inatosha!daah tangu uhuru hadi leo!..Jamani tuwe na utu,tuwafikirie wenzetu!HALI YAO NI MBAYA SANAAA

    ReplyDelete
  8. Hivi! ninyi woote hapo juu mnalalamika. Sisi wenyewe wa Rukwa hatuna shida. kwani mshasikia tunaandamana wala mji wetu unanuka kama huko dar! haya ni mambo madogo tu . Ninyi tulieni tuwalimie chakula mjaze xxxx vyenu. Huku tambarare hata Pinda amabye kwao ni huku hana shida . Ninyi na Dar yenu tuacheni na Rukwa yetu

    ReplyDelete
  9. NAKUPONGEZA WEWE ULIYEJITAMBULISHA KUWA NI MCHAGGA, UNAONEKANA NI MTU, KWANI UMESEMA TUONYESHE UTU NA KWA WATANZANIA WENZETU TUWAJENGEE ANGALAU BARABARA TU SI KILA KITU NI KAZIKAZINI TU, KILA KITU KILIMANJARO, ARUSHA, DAR ES SALAAM, DODOMA. TUWASAIDIE NA HAWA WENZETU WA MIKOA MINGINE, KWANI KUKIWA NA MAWASILIANO MAZURI HUWEZI JUWA TUNAWEZA KUPATA SOKA LA KWENDA KUFANYIA BIASHARA YOYOTE ILE HATA KUFUNGUWA DUKA KWA NYINYI WACHAGGA. SERIKAI ILIONE HILO JAANI

    ReplyDelete
  10. MICHUZI NILITOWA KOMENTI JUU YA HII BARABARA KWA VILE NILIGUSIA MAMBO YA UCHAGUZI MWAKA HUU, HUKUTUNDIKA HAPA. UNAVYOIPENDA CCM! MBONA MUOGA HIVYO! WEWE NI MWANDISHI WA HABARI NA SISI TUNASEMA SI WEWE!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...