washiriki wa kipindi kipya cha muziki kinachotarajiwa kuanza kurushwa na TBC-1 Jumapili hii wakirekodi mchuano wao ambapo nyota wa fani mbalimbali huchuana kwa kucheza na mapatna katika wiki 13 za kipindi hicho watazamaji watakuwa wanawachuja mmoja mmoja hadi mshindi apatikane akiwa yule aliyesalia mwisho. atalamba zawadi ya shilingi milioni 15

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. utumbo mtupu yani sijawahi kuona wote hawajui kucheza wataishia kutongozana tu lakini ni upuuzi hawajui kucheza wanataka kuiga mambo ya dancing with the stars haya yetu macho kaka michuzi usisahau kutuwekea mambo yanavyoendelea tena kwa video sie wambali tupate kujionea

    ReplyDelete
  2. Inakuwaje muziki unaotumika ni wa kilatino???? Kwani hatuna muziki wa nyumbani?? Watanzania vichwa maji kweli kweli. Kwa sie tulioa wageni utamwonyeshaje mkeo "dancing with the stars" ya kwetu afu kinapigwa kilatino!!!

    Mdau USA

    ReplyDelete
  3. Kilichobaki sasa, ni mcheze mziki tu sasa.hamna deal la kufanya.

    ReplyDelete
  4. Oyaa uncle.Najua utanibania kama kawaida yako.Mi sioni mshindi hapo.Hasa huyo jamaa mwenye shati jekundu.Vurugu kwenda mbele.

    ReplyDelete
  5. Haya tena Photocopy nyingine hiyoo!! Hivi jamani hata kama tuna copy na ku paste kila kitu cha unyamwezini tuwe tunajaribu kuingiza maadili yetu ili hata Babu na Bibi kule Lukuredi wawe wananufaika!! Kama swala ni mashindano ya kucheza la hao we " celebrities"" kwa nini wasishindanishwe kucheza Lizombe au Kasimbo yeye?? Mimi nadhani kwa kufanya hivyo ingekuwa inaleta maana zaidi kwa jamii yetu ya kitanzania kuliko kucheza Macharanga ambayo hayatuhusu!! Jamani kama ubunifu hatuna kabisa tujaribu KU-COPY, TU_PASTE halafu TU-EDIT kidogo walau tuonekana tunafanya kazi!! Mwe!

    ReplyDelete
  6. UTAMADUNI WETU UMETUSHINDA? SIJAONA KUCHEZA NGOMA ZA KWETU ZA MBEYA AU ZA KIZARAMO MDUNDIKO AU ZAKIMAKONDE AU KIDUMBAK CHA PEMBA AU NGOMA ZA BUKOBA TUNARUKIA MA SALSA NA RUMBA? SELEBUKA GANI HII BWANA. TUMEINAMA TUMEINUKA TUMEOKOTA KIDUDE EEEH KIDUDE MAMBO MAMBO KWA SOX EEEH KWA SOX HAKIPENDWI KITU NI POCHI TU.

    MRISHO MPOTO KASEMA TUNAUTUKUZA UENGEREZA SANA NA MAMBO YA NJE>

    KIMARO.

    ReplyDelete
  7. JAMANI VIPI MNANDA,MCHIRIKU,VANGA,MDUNDIKO NA MAGOMA KIBAO YA KIKWETU WASWAHILI;
    HAO WANANITIA KINYAA TU,
    bora kuweka ngoma za asili tu kuliko kuiga kitu tusicho kiweza,

    ReplyDelete
  8. Bwaa....nahisi kutapika.Kibaya zaidi ni kuwa hakuna hata anayejua kucheza aina hiyo ya muziki kati ya hao wote.Naona wanajizungusha tuu.Kwa huku ughaibuni mmoja anakuwa ni mtaalamu wa kucheza na mwingine anakuwa ni mtu maarufu ambapo huyo maarufu anakuwa anafundishwa na huyo mtaalamu.Hapo nimeshindwa kutofautisha...Mvurugano tuu.Bora wangechukuliwa wataalamu wa ngoma za asili kutoka vikundi kibao ambavyo tunavyo hapo Tz.Kama kile cha mzee jangala,Parapanda arts,
    n.k.
    Jonaa.

    ReplyDelete
  9. Michuzi nimeona, kwa leo sitacomment chochote, naomba uturushie kadri mashindano yatakavyokuwa yanaendelea.
    Tuombeane uzima.

    ReplyDelete
  10. mimi nampa ushindi mwenye suti nyeusi naona atakuwa Ali Baucha .he is the best

    ReplyDelete
  11. WANAZUONI WA BASATA NA BAGAMOYO TUONYESHENI KILICHOPO CHINI YA KAPETI LA MASHINDANO HAYA NA HIYO MANTIKI YA MSHINDI KUONDOKA NA TSHS.15,0000,000.00 BILA KULIPA MAPATO YA SERIKALI.TRA ELEKEZENI MACHONI HUKU KWENYE MAPESA NA MSIONE HAYA KUNYOFOA HALALI YENU.

    ReplyDelete
  12. miziki yetu tunaiua wenyewe..jamani tumieni miziki ya kitanzania please! tumechoka utumwa.. tumesoma ili iweje ndugu zangu?
    kamera yenyewe moja na imewekwa sehemu moja utajuaje kama mtu wa upande wa pili anacheza vizuri???

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...