Ankal kwanza nakupongeza kwa kutukutanisha wabongo kutuhabarisha.
Mungu awe mbele yako siku zote ili libeneke liendelee. Mkubwa nina
tatizo kidogo naomba uniwekee kwenye blog yetu ili wadau waweze
kunisaidia. Nina gari aina ya Toyota Landcruiser GX automatic model U-HZ J77HV-PEU nyingine IHZ ya mwaka 1992. Tatizo lake ni kwamba huwa inapoteza nguvu inapokuwa kwenye miinuko mikubwa. Haishindwi kabisa kupanda ila huwa inapanda kwa kujirusha rusha. Nimejaribu kuwaona mafundi kama wawili hivi wakaniambia tatizo ni
pump. Pump roter inatakiwa kubadilishwa pamoja na parts nyingine ndogo
ndogo ndani ya pump. Fundi wa kwanza alibadilisha pump roter lakini
tatizo halikuweza kuisha. Baada ya kubadilisha pump roter gari ikawa
inatoa moshi mwingi na nguvu yake kwenye miinuko haikuweza kurudi.
Nikapeleka gari kwa fundi wa pili, yeye aliweza kukata kabisa moshi
lakini tatizo la kupoteza nguvu kwenye miinuko mikubwa liko pale pale.
Wadau, inawezekana miongoni mwetu akawepo mtu ambaye amewahi kupata
tatizo kama langu. Naomba mnisaidie kujua tatizo hapa ni nini hasa na
wapi hapa mjini naweza kupata fundi/mafundi wazuri ambao wanaweza
kumaliza hili suala?
Mdau Kaburu
Mungu awe mbele yako siku zote ili libeneke liendelee. Mkubwa nina
tatizo kidogo naomba uniwekee kwenye blog yetu ili wadau waweze
kunisaidia. Nina gari aina ya Toyota Landcruiser GX automatic model U-HZ J77HV-PEU nyingine IHZ ya mwaka 1992. Tatizo lake ni kwamba huwa inapoteza nguvu inapokuwa kwenye miinuko mikubwa. Haishindwi kabisa kupanda ila huwa inapanda kwa kujirusha rusha. Nimejaribu kuwaona mafundi kama wawili hivi wakaniambia tatizo ni
pump. Pump roter inatakiwa kubadilishwa pamoja na parts nyingine ndogo
ndogo ndani ya pump. Fundi wa kwanza alibadilisha pump roter lakini
tatizo halikuweza kuisha. Baada ya kubadilisha pump roter gari ikawa
inatoa moshi mwingi na nguvu yake kwenye miinuko haikuweza kurudi.
Nikapeleka gari kwa fundi wa pili, yeye aliweza kukata kabisa moshi
lakini tatizo la kupoteza nguvu kwenye miinuko mikubwa liko pale pale.
Wadau, inawezekana miongoni mwetu akawepo mtu ambaye amewahi kupata
tatizo kama langu. Naomba mnisaidie kujua tatizo hapa ni nini hasa na
wapi hapa mjini naweza kupata fundi/mafundi wazuri ambao wanaweza
kumaliza hili suala?
Mdau Kaburu


Nenda kwa dealers, sio mafundi wa chini ya mti.Unaweza kumiliki gari kama hilo, kulitengeneza huwezi?
ReplyDeletekwa mimi naona transmission yako inaanza kufa maana nilikuwa na tatizo kama hilo aina ya gari Acura ilikuwa inakufa nguvu nikipunguza mwendo na kwenye vimwinuko kidogowakafanyia computer diagnosis ikaonyesha transmission inashida kwa hiyo waambie waangalie hiyo
ReplyDeleteMiss GA-USA
KWANZA KABISA MTAFUTE FUNDI MMOJA ANAITWA HASSAN YUPO HAPO NJIA PANDA YA MAKONDE NJIA INAYOELEKEA MAGOROFA YA PPF UPANDE WA KUELEKA BAHARI, HUYU NI KIBOKO HASHINDWI KITU, KAMA HAPATIKANI HAPO KWA VILE KULIKUWA NA TETESI ZA KUFUKUZWA HAPO NENDA HAPO KITUO CHA MAFUTA JIRANI ENGINE MUULIZIE WATAJUWA HABARI ZAKE. NA KUISHA KWA NGUVU YA GARI ZIKI SABABU NYINGI TU.
ReplyDeleteMOJA INAWEZA KUWA CLUTCH PLATE IMEISHA.
MBILI CUMBELT IMEISHA, GARI ZINGINE HUWA NAYO YA MPIRA ZINGINE ZA CHAIN.
TATU RING ZA PISTON KWENYE ENGINE ZINAWEZA KUWA ZIMEISHA.
NNE INJECTOR PUMP KAMA NI DIZEL IMEISHA
NA ZIPO NYINGINE MUONE HASSAN ATAKUMALIZIA TATIZO LAKO. NI KIJANI WA MAKAMO NA ANAJICHO CHONGO UPANDE MMOJA. KILA LA KHERI MZEE
NJIA PANDA YA MAKONDE NI MBEZI BEACH BARABARANI KUELEKEA TEGETA KABLA NA KARIBU NA INTERCHICK NILISAHAU KUKUELEZA NJIA PANDA YA MAKONDE IPO WAPI, SAMAHANI KWA HILO
ReplyDeletepole sana nduguyangu kwanza hiyo gari
ReplyDeleteni enjaction ukae ukijua lazima
upate fundi wagari hizo sio wale
wa kujaribu.kuna chombo kama sikosei
kipo chini ya drow ya gari ndani
cheusi kibox. ndani kipo kama utumbo wa radio.basi ukibadilisha hicho
ninaimani litakwisha tatizo lako.
ahsante
Mdau umeongea kwa parables (mafumbo) au ulikuwa unamaanisha ulichoandika! Kama umeongea kwa parables hilo tatizo la gari yako, la kushindwa kupanda "miinuko mikubwa" au kupanda kwa kujirusha rusha litakwishwa ukimuona Dr manyangunyangu kutoka ufipa! Anadawa mujarabu wa matatizo kama hayo, au hata kama "hipigi stata" basi hapo umefika. Lakini unaweza anza kwa kunywa supu ya pweza (watu wa pwani twaita mwengo) na na karanga mbichi usiku. Kwa mchana mihogo mi bichi, shushia na juice ya parachichi...Halfu hiyo gari yako isjali rasmi kwenye mbio za magari,Formula 1 2010... Nakuhakikishia utakuwa bora kuliko Schumacher.
ReplyDeleteMdau nimekupata na tatizo lako naamini ni dogo sana ila mafundi unaowapata hawajui kitu wanajaribu kujifunza ufundi kupitia gari lako,sasa tatizo lako linaweza kutatuliwa pale mjini A-Town kwa fundi wa uhakika na anaeaminika East Africa nakupatia contacts zake ni 0754055168 na 0715175217 anaitwa Manyundo ukimpata mweleze tatizo la gari yako na atakupa ushauri nini cha kufanya,mwambie umepata contacts zake kutoka kwa Meneja Marekani,hope utafanikiwa.
ReplyDeleteAisee... If the car has a manual transmission, probably the problem is with the clutch assembly. Slipping of the clutch is the probably cause. I'm not in Tz so I can't help you finding the best mechanic.
ReplyDeleteTransmission problem hiyo.
ReplyDeleteMafundi wa kibongo, sorry to say, hawafai..especially kwenye magari haya ya 4x4. wengi wanabahatisha, kaka ningekushauri uende pale Mikocheni, kuna sehemu pamefunguliwa juzi panaitwa Tinys Garage, Old Bagamoyo Rd. Wanabango pale kwenye jengo. Nje nadhani kuna watu wanauza taa za nyumba, wako karibu na shule ya DIS-Dar es Salaam Independent School.
ReplyDeleteKaka matatizo ya gari lako inaweza ikwa inatoka na moja kati ya mawili kwa jinsi nielewavyo mie. Moja na la bei ya nafuu ni hilo la pump na mafundi wengi wanapenda kukimbilia kubadili vitu fulani fulani ili wasimtie mteja wao gharama kubwa. Ikiwa ndio hizo rota nozzle na vinavyofanana na hivyo. Tatizo la pili ni kukosekana kwa mgandamizo wa kutocha katika silinda. hii inaweza ikawa inatokana na vitu kama valvu kutoziba vizuri, cilinda kupanuka piston ring kuchakaa na yanosababisha hilo. Ushauri wangu peleka hilo gari International Motors wao ndo wakala wa Toyota Tanzania.
ReplyDeleteHabaru za huko nyumbani mdau.Kama gari lako mailage yake imezidi 100,000 nakishuri utafute gari lingine maana hilo limechoka.kurudi nyuma katika mtelemko wakati liko kwenye "D" maana yake gari limezeeka.utabadilisha pum hadi gharama za matengenezo zifikie thamani ya gari lakini litaendelea kurudi nyuma.nenda shwroom kachukue kitu.
ReplyDeleteBwana kaburu hapo watu wamekuchukulia tu hela wala pump haina ushirikiano na kupoteza nguvu kwa gari lako.Gari la automatic huwa inatakiwa kujibadilisha gears pale ikipungukiwa na nguvu kinajulikana kama (transmission control unit or TCU)na inawezekana kuna faults transmission solenoids zinazoleta shida kwenye gari lako.
ReplyDeleteKama unahitaji mtaalamu, piga simu namba +255754287069 muulizie fundi Kamala atakusaidia.
Mdau Fau.
Braza,
ReplyDeleteHiyo maanake gari limechoka. Acha ubahili na tafuta gari nyingine. Watu kama nyie ndio mnachangia ku-pollute mazingira. Asante
wote wamesema sawa hila kwa ushauri wa kitaalamu nenda
ReplyDeleteTOYOTA PALE PUGU ROAD KARIBU NA QUALITY GROUP AU MAARUFU BANDA LA NGOZI. kwa thamani ya gari yako inakubidi uende pale kwani wao wanawataalamu toka kampuni ya Toyota Japan usiende sijui kwa findi nani au nanai wote wanajaribu pale ndio haswa kazi yao.
Mdau Nautiakasi, Mar.13:03.00AM akili yako iko wapi? mbona ushauri wako na wawenzio uko tofauti sana.
ReplyDeleteIssue ndogo sana, weka vidonge 2 vya VIAGRA kwenye engine uone itakavyopanda hiyo milima. AS Well chukua tahadhari sehemu unapoipaki usiku maana unaweza kuamka asubuhi ukaikuta juu ya paa la nyumba!
ReplyDeleteHao mafundi wanabahatisha...siku zote mafundi wa chini ya mwembe huwa ni makini kuliko magereji makubwa(siku hizi wamekuwa wezi sana)..mi nimeshatumia gari yangu mwaka wa sita sasa (mileage over 110,000km) lakinibado inadunda fresh..ila regular service with genuine parts ni lazima...siri kubwa ni mafundi wangu wa chini ya mwembe(kwa manyota)..kama vipi tuwasiliane
ReplyDeleteMazee