




Hellow Kaka Michuzi!
Kwanza nikupe pole kwa kazi ngumu ya kutupatia habari za uhakika kupitia globu yetu hii ya jamii,pia nikupongeze kwa kazi nzuri inayokubalika na jamii yote ya Watanzania.
Kaka Michuzi mimi ni mdau wa globu ya jamii nafanya kazi huku Masasi -Mtwara,na wiki endi iliyopita nilipata bahati ya kutembelea Daraja la Umoja "Unity Bridge".
Kwa kifupi tu kaka ni kuwa daraja hili linavuka mto Ruvuma na lipo eneo linaloitwa Mtambaswala (Mpakani mwa Msumbiji na Tanzania) .Daraja hili ndo linaunganisha nchi yetu ya Tanzania na majirani zetu Msumbiji,na limejengwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Msumbiji.Kaka Michuzi daraja hili limeshakamilika tunasubiri tu sherehe za ufunguzi.
Kaka Michuzi daraja hili ni muhimu sana kwa sababu sasa linatuunganisha wananchi wa nchi mbili hizi,matokeo yake ni kuwa tunategemea mabadiliko makubwa kiuchumi,kibiashara na kwenye nyanja nyinginezo kama michezo.
kaka Michuzi sasa safari yetu ya kwenda kwenye fainali za Kombe la Dunia mwezi Juni hapo Afrika Kusini imerahisishwa kupitia daraja hili la Umoja.
Mwisho kaka Michuzi kwa niaba ya wadau wote wa Ukanda huu wa Kusini mwa Tanzania nifikishe shukrani za dhati kwa viongozi shupavu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Msumbiji.
Ahsante
Mdau
Eng.Jimmy Wilbard-
Ingerosec Corporation
The Project for Improvement
of Masasi -Mangaka RoadThe Project for Improvement
kweli uchaguzi unakuja du ni kiboko ndugu zangu
ReplyDeleteHu ni uchaguzi tu akuna jingine mkuu wetu michuzi vipi kure kusini sio nyumbani kweli ?
ReplyDeleteUchaguzi uchaguzi uchaguzi............ tu apa akuna jipya
ReplyDeleteANSANTE MHESH. RAIS MSTAAFU BENJAMINI MKAPA: BADO MBEGU ULIZOPANDA WAKATI WAKIPINDI CHAKO SASA ZINZIDI KUTOA MATUNDA; DARAJA SAFI: BARABARA KUU DODOMA TO MWANZA; MTUKULA KAGERA TO BURUDI KUPITIA BUKOBA: BAHATI MBAYA KAZI ULIYOWAACHIA BARABARA MBAGARA WAMESHIDWA KUMALIZA; WEWE ULIKUWA MTU WA VITENDO NA SI MPIGA MDOMO! UBARIKIWE SANA.
ReplyDeleteTuombe Mungu hili daraja lisiwe sehemu nyingine ya kupotezea maisha ya wananchi wa pande zote mbili. Maana kila siku twasikia ajali ajali ajali zinazosababishwa na uzembe wa madereva.
ReplyDeleteAnkali Asante kwa kutuhabarisha, madau asante kwa kutuma picha kwani hata siku nyingine nikiona picha kama hizi nitakumbuka hili ni daraja letu la Muungano na wala sio lango la kuingilia jiji la Mombasa. na wao wana pembe kama daraja letu sema za kwao zimeunganika. shukran Mdau ugaibuni
ReplyDeleteSioni ofisi za uhamiaji jirani. Kumbe kwenda Msumbiji huitaji kuwa na passport? inapendeza sana.
ReplyDeleteEng.Jimmy Wilbard,hakuna kunywa bia wala kuhama mpaka mkamilishe Tunduru-Masasi na Songea-Tunduru Road,Mdau wa south.
ReplyDeletehili ndio daraja alojenga mkapa,lile la mwanzo likaitwa mkapa brige ni la mzee ruksa ndo alojenga,kila kiongozi wa tz atakumbukwa kwa kazi zake.
ReplyDeleteASANTE SANA ANKAL KWA TASWIRA NZURI.HAPA HAKUNA SUALA LA UCHAGUZI BALI NI MRADI UMEKAMILIKA KWA KALENDA YAKE.SASA NAOMBA WADAU MNIJULISHE KUPITIA DARAJA HILI SAFARI ZA MABASI NA MALORI YA MIZIGO KATI YA TANZANIA NA AFRIKA KUSINI ZITAKUWA ZIMERAHIRISISHWA KADRI GANI?
ReplyDeleteSAFI SANA MH. MTUFUFU RAISI KIKWETE KWA KAZI YAKO NZURI YA KUSIMAMIA WATENDAJI WAKO MPAKA KITU KEELEWEKE.
ReplyDeleteHAYA NDIO MAENDELEO KWANI DARAJA HILI LITAFUMUA MLIPUKO WA SHUGHULI ZA KIUCHUMI NA BIASHARA.
ASANTENI MAIINGINIA VILEVILE.
KIKWETE UNA KULA YANGU BILA YA WASIWASI WOWOTE.
M/MUNGU AKULINDE NA UENDELEE KULITUMIKIA TAIFA LETU.
nawapenda hawa jirani zetu wapole, sijasikia vurugu nao, great neighbors, hapo pia dili ya magari inakua poa, badala ya kupitishia bandari ya dar, i might try msumbiji then drive hapo darajani, poa sana.
ReplyDeleteooh Mkapa hakufanya kazi....vitu alivyofanya vinaonekana. Vingine vimemalizikia tu awamu hii. Angeendelea kubaki madarakani tungekuwa mbali zaidi kuliko ilivyo sasa....Maoni yangu tu!... Michuzi usibanie hii
ReplyDeleteWajumbe ukiwa na gari bishi unaweza kwenda kucheck world cup SA kutokea TZ kiulaini. Dar Masasi km 596, Masasi-Maputo haizidi na haipungui 2300km, Maputo J'burg 605km. Kwa km hizi world cup haujaliona bado?
ReplyDeleteMdau wa Sat Mar 13, 03:13:00 AM,
ReplyDeleteKu-plan, Consultancy Services za Ku-design, mpaka construction ni miaka! Kujenga 720m Concrete Bridge kwa Uchumi wa Tz sio fast kama unavyofikiri ni uchaguzi! Fikiria zaidi kila wakati!