Kutoka kushoto ni Reverand Margret May Dempsten kutoka Ontario, (Canada). Bi.Lysandra Padeken kutoka Hawaii ( Marekani), Bi. Joyce Kafanabo ( Afisa Ubalozi- NY), Bi. Mwajuma Alice Abok ( Kenya), Dkt. Augustine Mahiga Balozi wa Tanzania Umoja wa Mataifa, anayemfuatia Balozi, ni Bi Grace Mokiwa Dar es Salaam ( Tanzania) Bi. Hellen Grace Akwii Wangusa nyuma ya Balozi ( UN), Bi Irene Mhogolo mwenye koti la Blue kutoka Dayosisi ya Central Tanganyika Dodoma ( Tanzania) na Reverand Joyce Kariuki kutoka Kenya.

Hawa ni baadhi ya washiriki wa Mkutano wa 54 wa Kamisheni ya Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya Wanawake, hutoka katika makundi mbalimbali ya jamii yakiwamo ya Asasi zisizo za kiserikali pamoja na Mashirika ya Dini.
Pichani ni washiriki kutoka Young Women's Christian Association-Kanisa la Anglican, ambao walifika Ubalozi wa Tanzania kwa lengo la kubadilishana mawazo, kuhusu masuala ya elimu kwa mtoto wa kike, ajira, umilikaji wa ardhi kwa wanawake, biashara ya binadamu hususani wanawake na watoto, masuala ya wakimbizi na masuala mengine yahusuyo haki na ustawi wa mwanamke na mtoto wa kike. ziara hiyo ilikuwa ni sehemu ya ratiba ya Mkutano wa 54.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...