mkuu wa nanihii,vekesheni njema.
Kaka naomba tusaidie mawazo kuhusu hali ya usalama wa raia,vibaka wamezidi,maeneo ya jangwani darajani hapafai. Unakumbuka palikuwepo ulinzi baada ya mtu kukatwa shingo kwa waya aliyepita akiwa kwenye pikipiki.
Juzi tu nimepita hapo mnamo saa3 usiku nikakuta kijana kalala hoi analia baada ya kupigwa ngeta na kunyang'anywa kila kitu, na vibaka wanakimbia.
Sehemu nyingine ni mataa ya chang'ombe na batabara ya Nyerere road. Wananchi wanalizwa sana hapo. Je polisi na mgambo wa jiji hawawezi kusaidia?naomba kuwasilisha.
mdau -Dar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. DAWA YAO HAO NI MANYOYA TU!

    ReplyDelete
  2. Hapo kesi ya nyani inapelekwa kwa ngedere. Unauliza polisi na mgambo mko wapi.?!! Wanajua wenyewe walipo.

    Kazi ya watu hii . Ni mtu mwenyewe kujichunga asiingie mitego yao.

    ReplyDelete
  3. Mi hata sielewi! viongozi nchi imewashinda au? Mbona ni rahisi sana kuwamaliza hawa vibaka.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...