Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda na Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta, wakimsikiliza kwa makini Mwakilishi wa Mchungaji wa Kanisa Katoliki Tabora, Brother Mburu ambaye pia ni kiongozi wa msafara wa kwaya Toka Urambo tabora waliyotembelea Bunge leo.
Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta, akisalimiana na Mgeni wa Mhe. Abdukarim Shaah Mbunge wa Mafia (Kushoto) alipotembelea viwanja vya Bunge leo.
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Samuel Sitta, akifurahia jambo na Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi Mhe. Mwantumu Mahiza, mara baada ya kipindi cha maswali na Majibu Bungeni, Mjini Dodoma. Wanaoangalia pembeni toka kushoto ni Mhe. Halima Mamuya, Mbunge Viti Maalum Arusha (CCM), na Mhe. Lediana Mg’ong’o Mbunge Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM)Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta, akizungumza mabalozi wapya walioteuliwa kuiwakilisha Tanzania Nje mara walipofika Ofisini kwake Dodoma kumuaga leo. Kutoka Kulia Ni Balozi Radhia Msuya, alieteuliwa kuwa balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini na Balozi Patrick Sere anaekwenda Malawi.
Mabalozi wapya walioteuliwa hivi Karibuni, Balozi Radhia Msuya, (kushoto) alieteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini na Balozi Patrick Sere anaekwenda Malawi wakiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi wa Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa wa Bunge. Ndg Jossey Mwakasyuka mara walipo mtembelea Ofisini kwake Bungeni Dodoma baada ya Kumuaga Waziri Mkuu na Spika.
Balozi wa Rwanda nchini Mhe. Fatuma Ndangiza (Kulia) akizungumza na Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta katika Ofisi yake mjini Dodoma. Balozi Ndangiza yupo Bungeni Dodoma kwa shughuli za kikazi.
Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo(kulia) akibadilishana mawazo nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi Ramadhan Khijjah (katikati) pamoja na Naibu Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango Clifford Tandari( kushoto) mara baada ya uzinduzi wa mchakato wa majadiliano ya Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania(MKUKUTA) ambazo zoezi hilo limeanza jana na linaendelea nchini kote.
Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo(katikati) akibadilishana mawazo nje ya Ukumbi wa Bunge mjini Dodoma na Mbunge wa Jimbo la Busega wilayani Magu, Mkoani Mwanza, Dk. Raphael Masunga Chegeni(kushoto) pamoja na Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Lucy Owenya ( kulia) mara baada ya kumalizika kwa kukusanya maoni ya wabunge juu mchakato wa majadiliano ya Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania(MKUKUTA) ambazo zoezi hilo limeanza jana na linaendelea nchini kote.Lucy owenya.

(Picha na Tiganya Vincent/Owen Mwandumbya wa Bunge)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. LETS GIVE CREDIT WHERE.....

    Ankal,
    Naomba nichukue fursa hii kwa kumpongeza PR officer wa ofisi ya bunge, kama sikosei atakuwa ni Owen Mwandumbya.
    Huyu mtu ametokea kunivutia kwa jinsi anavyojua kutumia opportunities alizonazo ndani ya uwezo wake.
    Sitaki kusema mengi sana leo lakini nadhani wenye akili timamu wataelewa nasema nini.
    Hawa ndio ma-PR wanaostahili kushika nafasi ktk ofisi za serikali na taasisi zake. Waliobakia wanalala au wanafanya kazi bora liende

    Mdau Kilimahewa

    ReplyDelete
  2. Anon hapo ulieelewa, hebu tufafanulie na sie wengine ambao tupo mataa kiasi. What is the hidden meaning?

    ReplyDelete
  3. mhh we unaongea una uhakika na unachokisema.tunahitaji ma-PR wa aina hii lakina kuna matukio kibao mazuri huyo Owen wako ameyamiss. consistency muhimuuuuuuuuuuuuu

    ReplyDelete
  4. Duh,
    Lucy Owenya nae si haba.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...