Marehemu Evaline Gembe

Familia ya Bwana na Bibi Gembe wa Upanga-Dar-es-salaam na Tabora, wanasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Evaline Gembe(pichani) kilichotokea hapo juzi tarehe 30.3.2010 huko Toronto,Canada.Evelyne amefikwa na mauti katika hospitali ya St.Michael’s ya Toronto alipokuwa amelazwa.

Taratibu na mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda nyumbani Tanzania kwa mazishi zinafanyika nyumbani kwa dada yake, Julie huko huko Toronto,Canada.

Ukiwa kama mtanzania,ndugu,jamaa au rafiki, unaombwa kuchangia fedha,hali na mali kwa ajili ya kuwezesha kuusafirisha mwili wa marehemu kurudi nyumbani kwa mazishi mapema kadri iwezekanavyo kwani kama wengi wenu mnavyofahamu, mwili unavyozidi kukaa Funeral-Home,gharama ndivyo zinavyozidi kuongezeka. Mwili utasafirishwa punde tu zitakapopatikana fedha za kutosha kwa ajili ya kulipia gharama husika.

Unaweza kutuma mchango wako kwenye Account maalumu ya wafiwa kama ifuatavyo:

BANK : CIBC (Canadian Imperial Bank of Commerce)

ACCOUNT NUMBER: 5681839

TRANSIT NUMBER: 00902

INSTITUTE NUMBER: 010

SWIFT CODE: CIBCCATT

Vilevile unaweza kutumia E-mail Money Transfer kwa Sania Esmail.Anuani yake ni saniae@yahoo. ca au kuwakilisha msaada wako kwa kutumia anuani hii:

1025 SCARLETT ROAD,

APT 606,

BUZZ # 178
TORONTO ON,

M9P 3V3.

Kwa mawasiliano zaidi unaweza
kuwasiliana na wafuatao:
Julie +1 416-247-8318
Esmail Manambi- +1 647- 299-2572
Victor Wambura- +1 647-428-4118
Prosper Luteganya- +1 905 626 3764

Tafadhali chukua muda kuwafariji na kuwaombea ndugu,jamaa na marafiki waliofikwa na msiba huu. Tunatanguliza shukrani kwa misaada yote iliyotolewa na itakayotolewa. Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.

Amen.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. poleni sana ndugu zetu wa canada maana tunajua ilivyo ngumu ukifiwa ugenini,inasikitisha sana na inanikumbusha sana kaka yangu mm alifia nje ya nchi.Mungu awasaidie mkamilishe kila kitu.
    ndugu yenu wa uk

    ReplyDelete
  2. Natoa pole nyingi sana kwa Ndugu wa marehemu kwani Sister Eva namjua vizuri sana,mwaka 2002 wakati anaondoka bongo kwenda canada nami nikaondoka kwenda ugiriki,yaani tunajuana kwa karibu ,nimeshtushwa sana na msiba wa huyo dada
    BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIBARIKIWE
    RAHA YA MILELE UMPE EE BWANA,NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE,APUMZIKE KWA AMANI
    AMEN

    ReplyDelete
  3. Mdogo wetu Evaline, tulikupenda ila Mungu kakupenda zaidi. Tunakuombea Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi. Tutakukumbuka siku zote kwa upendo na ucheshi wako.

    ReplyDelete
  4. Eva,
    You will be greatly missed. May the Almighty rest your soul in eternal peace...Amen

    ReplyDelete
  5. Wafiwa poleni sana. Napenda kufahamu uhusiano wa marehemu na Ndugu Peter Gembe au Leppie Gembe. Ni binti yao? AU mdogo wao? Tafadhali nijulisheni.

    ReplyDelete
  6. poleni wafiwa,
    Nilizisoma taarifa za kuugua kwa huyu binti mpaka taarifa ya kifo chake kule Jamiiforums (JF) na nimeguswa sana.

    Michuzi, Asante kwa taarifa hii yenye accounts za kuchangia, pia ningeshauri iwepo na accounti kwa sisi tulio Tanzania kuchangia, au ata nambari ya simu ya wahusika wa hapa nyumbani.

    RIP Eva Gembe.

    ReplyDelete
  7. Maskini....a true African beauty. INNA LILLAH WA INNA ILAHI RAJI'UN. (To him (God) we belong,and to God is our return).

    My condolence to the family and friends.

    May this loss be our reminder; sooner or later we will all meet our Creator, we better be ready.

    ReplyDelete
  8. Jibu kwa Patrick Eva ni binti yao (mtoto wa kaka yao). RIP Eva

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...