ankal othman aliyeikamata taswira hii maeneo ya kiwalani hana uhakika kwamba hii imekuja hivi ama kumetumika ubunifu. labda wadau japani watusaidie

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Hii imekaa vibaya, japo ubunifu umetumika. Tujiulize hii gari inabeba abiria usalama wao ukoje ndani ya gari hii walofanyiwa modification? Kwa upeo wangu mdogo naona hizo tairi za katikati zitakuwa zinaenda upande na kujiburuza wakati wa kuakata kona, kwa hiyo haiwezifanya kazi kiufanisi. me naona laweza hata kunyofoka hapo lilipoungiwa

    ReplyDelete
  2. HUKU KWENYE NCHI ZILIZOENDELEA NA ZINAZOJALI MAISHA YA RAIA WAKE, UBUNIFU KAMA HUU NI KINYUME CHA SHERIA.

    HAYO MAGARI YANATENGENEZWA KWA VIWANGO MAHSUSI NA MATUMIZI YAKE, HAO WALIOBADILISHA WAO WAMEFUATA VIWANGO GANI. WANAWEKA MAISHA YA ABIRIA HATARINI.

    MDAU, READING.

    ReplyDelete
  3. Hongera kwa ubunifu.
    mi sioni tatizo la urefu wa gari hii ukizingatia gari ndefu kama au kuliko hizi zipo na zina matairi zaidi ya yanayoonekana katika gari hii. Lamsingi la kujiuliza ni kuwa jee uunganishaji wa gari hii umezingatia taratibu za kiusalama? nakusudia umadhubuti wa kiungo. urefu na wingi wa matairi nadhani sio tatizo.
    hongera kwa ubunifu

    ReplyDelete
  4. Hii sio mpya mbona wajameni? Kwenye Mbuga zetu za wanyama, 4wheel drive nyingi zinazopeleka watalii zimeundwa kwa staili hii, nimeziona kwa macho yangu Landrovers kebekebe Ngorongoro tangia 2006

    ReplyDelete
  5. Hivi kuna askari ambaye hupitia kwenye mitandao na kuona haya?

    ReplyDelete
  6. Hapo hamna tatizo. Tena ni bora kuliko FUSO zinazobadilishwa kutoka lori uwa basi hapo Bongo. wengi pia hawajui kuwa ni mabasi machache sanamakubwa yanakuja kamili. Mengi yametengenezewa bodi kwenye garaeji tu za mitaani hapo Dar na Nairobi!!

    ReplyDelete
  7. Candid ScopeApril 16, 2010

    Tanzania hakuna sheria za udhibiti wa mambo muhimu kama haya. NI injinia gani aliyethibitisha ubunifu huo kwa usafiri wa umma kama unakubalika? Injinia gani aliyethibitisha uwezo wa injini ya gari hiyo ina uwezo wa kuvuta mzigo wote huo? UPUZI MTUPU NA HATARI TUPU. SERIKALI INAFANYA NINI?
    Kwa nini malori hayana matairi katikati isipokuwa nyumba na mbele tu?
    tumieni akili kwanza kabla ya kfanya kitu

    ReplyDelete
  8. Hii ni ubunifu mzuri sana. watu wanajifanya wanjua sana USALAMA. hata haya magari ayana DESIGN CONSIDERATION STRATEGEY. mfano design consideratin strategy ya Benz Model ya C ay E haiweizi kuwa sawa na Ya corolla au Maark II. C200 inaweka kipaumbele zaid kwenye usalama na uimara wa gari wakati MArk II strategy yao inakuwa kwenye cost ndogo. Hakuna system inayokidhi iwango vyote tusijidangaye.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...