Danford Mpumilwa

Dear Bro Michuzi
Nimefikishiwa maulizo mengi k
utoka kwa wadau na wapiganaji wengi wakisema
wamesikia kuwa nimetangaza nia ya kugombea ubunge mwaka huu kupitia CCM
kwenye jimbo la Njombe Magharibi. Napenda kuwajulisha kuwa ni kweli ingawa
ukiacha gazeti moja na habari chache tu ndio vilivyoandika habari hizo. Kwa
sababu mtandao wako unafuatiliwa na wapiganaji wengi ambao wameniulizia juu
ya habari hizo nimeona kuwa niwajulishe rasmi kuwa kweli nagombea kwenye
kinyang'anyiro hicho. Kwa wale ambao hawanijui kwa undani wanaweza kupata
maelezo yote kwenye libeneke langu:

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 30, 2010

    Nimejaribu kuweka commenti kule nikashindwa. Ninashukuru kwa kazi nzuri lakini jaribu kufanya / kuweka tafsiri ya kazi zako ni nzuri sana mzee ili wengine waliosoma st. Madenge PS waelewe na wapiga kura wako wengi wako ktk kundi hili

    ReplyDelete
  2. Swahiba wangu, kaka yangu Dan Lutte..mimi nadhani ni busara ukaanzisha taasisi kubwa tu ya habari ya kimataifa ambayo walau itakuweka kwenye chati ya media zaidi kuliko huo uvuvuzela ambao ndugu yangu ukiwatoka wananchi japo kwa siku kadhaa kwenda a-town kula ndafu watakushikia bango..njombe magharibi muachie mzee wa majembe..bado majembe yake makali na yanalima kisawasawa...we haya tu

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 30, 2010

    MIMI BINAFSI ANAEGOMBEA KWA TIKETI YA SISIEMU NAONA NI WALEWALE

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 30, 2010

    Ni nini kimekuvutia hasa mpaka ukaamua kujitosa kugombea ubunge hali ukijua ni kazi nzito na ya wito, kwani Njombe ninayoijua mimi watu wanashindia mlo mmoja kwa siku. Utaleta mabadiliko gani na kwa njia zipi na fedha utazitoa wapi?

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 30, 2010

    Nilimfahamu Danford miaka 40 iliyopita nilpokwenda kusoma Form 5 Mkwawa High School, Iringa. Yeye alikuwa "O" level, (nadhani form 3). Hata hivyo, nilimzoea zaidi kwa kuwa yeye alikuwa katika jazz band ya shule iliyokuwa ikiitwa Orchestra Mkwawa na alikuwa mwigizaji na "crooner". Baadaye, tukakutana UDSM. Najua kuwa alikuwa Daily News, TTC na kisha AICC, Arusha. Nilipokuja Arusha nikamkuta mahakama ya UN ya Rwanda akiheshimika kwa utendaji wake wa kazi (professionalism) katika Tribunal. Lakini watu wengi wa Arusha wanamjua kwa kujihusisha kwake na utamaduni (muziki na michezo {Wazee Club}). Kama ataitumia ari, uzoefu na 'energy'yake kuwawakilisha watu wa jimbo lake kama anavyotoa mchango wake hapa Arusha kwa njia mbalimbali, basi litakuwa jambo la manufaa kwa watu wa jimbo lake. Aidha, naamini kuwa mara nyingi ni vizuri kumchagua mtu ambaye kwa zaidi ya miaka 30 amefanikiwa katika kazi alizozifanya kuliko mtu anayetaka kufanya uwakilishi kuwa "mradi". A. Inkishafi.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 30, 2010

    Nakubaliana na Inkishafi. Ni bora kuwa na mbunge ambaye walau ana afueni kimaisha.

    ReplyDelete
  7. s.ibrahimJune 30, 2010

    mmmmh wazee wetu nao hawako nyuma kwa kupenda kuuza sura...you look like FISADI!!STAY home n help yo wife care the family.TUNAHITAJI VIJANA.Alaaah..huna hata hayaaa.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 30, 2010

    HIVI TANZANIA HAKUNA NJIA NYINGINE YA KUSHIRIKI KWENYE HARAKATI ZA KULETA MAENDELEO KAMA KWELI WATU WANA NIA YA KULETA MAENDELEO KWA WANANCHI? SASA KILA MTU ANATAKA KUWA MBUNGE.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 30, 2010

    Malafyale Danford Mpumilwa hongera kwa kuweka wazi nia.
    Kura uangu na kula vile vile unayo,
    Nduguyo wa siku nyingi-lawerence

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 30, 2010

    Mzee Mpumilwa kwa sasa sioni kama unaye mpinzani,utapita kwa kishindo bila ya upinzani.
    Maendeleo ya jimbo la Njombe baada ya uchaguzi ndilo litakuwa tatizo la upinzani mkubwa kwako.
    jimbo hilo aidha limesahauliwa kwa muda mrefu au huyo utakayemridhi hakupewa nafasi ya kumalizia maswala na matatizo ya kilio cha wakazi wa jimbo,elimu ya msingi bado inayumba yahitajika marekebisho,kilimo cha vijijini hakijapata mipangilio ya mafunzo ya kilimo cha kisasa na mikopo kwa wakulima, mazahanati na usafiri wa wagonjwa katika jimbo hilo yanahitaji marekebisho ya teknologia za kisasa kina mama wengi bado wanazalia watoto majumbani,vijana wengi baada ya masomo ya kati wanakosa kupata ajira na hakuna mipangilio ya mikopo kwa kujituma ibinafsi,wengi hufuatilia njia fupi za kukimbilia miji mikubwa kutafuta ajira.

    Hata hivyo nina imani mafanikio yako ya kupita uchaguzi,utafanya mabadiliko makubwa jimbo la Njombe.
    KILA LA KHERI

    Mickey "MIKIDADI" Jones
    GLOBAL ADVANCE TANZANIA NETWORK

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 01, 2010

    Hahaaa ankal bwana eti vuvuzela dahhh inachekelesha

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 01, 2010

    Kila la heri, tutaonana Bungeni.

    (US Blogger)

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 01, 2010

    Inkishafi, Mimi pia nilikuwa Mkwawa High "A" levels 1970. I'm sure ukitumia jina lako ambalo si nickname nitakufahamu. Mimi pia namfahamu Dan, na ijapokuwa mimi si MwanaNjombe, najua atawasaidia sana watu wa jimbo lake kwa kuwa, kama ulivyosema, yeye mwenyewe ni mtu ambaye kila alikofanya kazi amefanikiwa including hapa UN (Nalijua hili kwa kuwa mimi pia niko hapa UN Arusha). Inatia moyo kuona kuwa kuna watu ambao wamefaulu kimaisha wako tayari "to give back to their communities" badala ya kukaa tu na kutumbua.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 01, 2010

    We S. Ibrahim, usiite watu ambao huwajui mafisadi. Huyu Uncle Dan huko UN anapata mshahara ambao ni mara kumi au zaidi kuliko wabunge wa wetu. Sasa wacha akatoe mchango wake kwao. J. Gombanile.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 01, 2010

    Mjomba Lutengano, sisi huku Njombe tunasamini mchnngo wako na kukuombea Mungu akulinde. Amen. mimi Atanasi.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 04, 2010

    ankal Dan, kila la heri...ndugu zetu kule nyumbani wanahitaji viongozi, overseers, ili mawazo yao yatekelezwe..tunachokosea wengi ni kudhani wale wote wa kule ni 'hamnazo'. Na tunaodhani hivi, kwa bahati mbaya sana, tumezaliwa kule, kukulia kule na kupata kijibahati cha kuja mijini!Wametufikishaje tumefikaje hapa tulipo kama hamnazo! Go, Dan, go...wasikilize na uwaongoze. Lusungu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...