Nani kasema hakukuwa na matangazo neshno
wakati wa gemu la Taifa Stars na Brazil? Hii nini??

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 07, 2010

    hayo matangazo ya kwenye hio screen ndio iliosababisha tufuje dollar mil 2.5? acha kutetea mkuu hakuna cha maana kilichofanyika kusaidia kutangaza vivutio vyetu vya utalii. tulicho kifanya ni kwamba tu tanzania imecheza na brazil tumefungwa kesho dunia ikiamka wanaendelea na maisha.hakuna mtu atasema nataka kwenda tanzania kwa vile imecheza na brazil hapana watu wanaenda kutalii baada kuona vivutio vya nchi.


    tungeweza kutumia hio hela kulipia matangazo kule kule south africa ambako kombe la dunia lina fanyika kwani hela ni nyingi sana na ingetosha kabisa kutangaza utalii kule.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 08, 2010

    jamani lets do something on that advert board, kwa kweli wachina matapeli...hiyo screen haijawi kufanya kazi hata siku moja ....i mean kuonyesha replays zozote za match zinazochezwa hapo taifa...nakumbuka first day kufunguliwa uwanja...walitaka kuonyesha ,teams line up ikaganda kabisa...hadi leo haijawahi kufanya kazi

    ReplyDelete
  3. ANKAL UNALIZA HICHO NI NINI? HICHO HAPO KINAONESHA WAZI KUWA HATUJUI NINI TUNACHOKIFANYA BADALA YA KUTUMIA KUTANGAZA RASILIMALI ZETU ILI WATU NA WA WAWEKEZAJI KWA UJUMLA WAFAHAMU RASILI MALI ZETU TULIZONAZO BADALA YAKE IMEWEKWA RAMANI YA UWANJA!!
    ILIBIDI TUTUMIE NAFASI HII ADHIMU KUTANGAZA RASILI MALI ZETU ZILIZOJIFICHA NA KUJULIKANA KUWA NI ZA NCHI JIRANI KAMA MLIMA KILIMANJARO, SERENGETI, ZANZIBAR NA KISWAHILI AMBAPO WATALII WENGI WANAJUA KUWA VIPO KENYA COZ KENYA WANATUMIA KWENYE MATANGAZO YAO!!
    PIA TUNGETUMIA NAFASI HII KUTANGAZA SIMBA WETU MWEUPE NA VIFARU WETU WEUPE AMBAO SOUTH AFRICA WANATUMIA KUJITANGAZA KAMA NI VIVUTIO VYAO!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 08, 2010

    wote wenye akili zao pamoja na wachangiaji hapo juu wamegungua tumepoteza pesa na hatujatangaza nchi hata kidogo, watanzania ni wajinga sana hata kama mtachukia mabango ya uwanjani hayasaidii kivile hapa dili lingekamilika kama tu nasi tungekuwa na matangazo mbalimbali ktk site zilizokuwa zinaonyesha gemu hili,walio wengi wamecheki gemu hili kupitia site mbali mbali ambazo hazikuwa na tangazo lolote la tanzania sasa hapo nchi imetangazwa vipi, hilo bango la neshno ndo unasema tumetangaza nchi mmeona tu nyie mlio bongo kwa taarifa yako. the whole thing mmepoteza hela na ndo shinda ya kukurupuka hata lengo la hii gemu halikuwepo, kama nia ilikuwa kutangaza nchi mmekula patupu

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 08, 2010

    kwa kweli Ankal huyo mtu ambaye anahusika anatakiwa kufukuzwa kazi! alitutia aibu sana, nilikaa karibu na mapaparazi wa kizungu basi walikuwa wanapiga picha screen wanangu ilikuwa aibu! mara screen inaonyesha kichina, mara documents zote like tender evaluation, payments za kujenga ujanjwa, mara ramani ya uwanja, yaani hakukua na tangazo lolote! inaonyesha kuwa walikuwa hawajajipanga. mechi imeanza mpaka baada ya nusu saa ndio wanaanza kucontrol alafu mautumbo matupu bora pale alivyoweka video ya nyimbo za asili.
    mimi naona watafute watu wenye uwezo wa control hiyo screen jamani!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 08, 2010

    Scoring Summary
    Tanzania Brazil
    Jabir Aziz (86) Robinho (10)
    Robinho (33)
    Ramires (53)
    Kaká (76)
    Ramires (90)

    Match Stats
    Tanzania Brazil
    Shots (on Goal) 18(9) 20(7)
    Fouls 13 15
    Corner Kicks 7 6
    Offsides 6 4
    Time of Possession 39% 61%
    Yellow Cards 0 1
    Red Cards 0 0
    Saves 2 8

    Match Information
    Stadium: National Main Stadium
    Attendance: 35,000
    Match Time: 15:00 GMT

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 08, 2010

    ile ni aibu kubwa sana, jamaa alikuwa anacontrol ile screen ni mjinga na hajui nini alikuwa anafanya au alikuwa hajajiandaa....mbaya zaidi wimbo wa taifa unaimbwa yeye kaweka makhirikiri....hii ni akili kweli?mbele ya rais? ni dharau na fedheha kwa rais wetu.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 08, 2010

    One day tutakuja jua Kamau alisema ukeli though naipongeza TFF kwa kutuletea kiburudussho, tuambieni mapato, hizi faida za kusema ujio wa Brazil ni faida napinga hizi ni faida fikirika/za kusadikika, kwanza kisoka hakuna faida yoyote ukichulia wachezaji wengi wa Stars wana maximum ya miaka miwili kusukuma ndinga hata kama wamedanganya umri.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 08, 2010

    Tanzania tunaringa na uwanja huu kama vile tumejenga wenyewe.....tushukuru Wachina kila siku.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 08, 2010

    yani tunasadiwa kutangaza nchi hadi na wazungu wenyewe kwa kweli naangaliaga national geographic hapa canada huwa mara nyingi sana wanaonyeshaga mbuga za wanyama serengeti kwa sana tuu yani inatia raha utadhani hizo mbuga ziko huku wakati tv za bongo hakunaga hata kipindi kinachoonyesha maisha ya wanyama huko ngorongoro ni vipindi vizuri sana na pia viahamasisha watalii wa ndani kwenda kutembelea mbuga badala yake tv zetu zimekolea kwenye isidingo baborita sinema za kinaigeria. zipeni mbuga zetu kipaumbele

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...