Ridhiwani Kikwete

*Kikwete asema sababu za kumpa jukumu ni rahisi kumpata
*Awaomba madereva kutokwenda kasi wakati wa kuomba wadhamini

MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete , Ridhiwani Kikwete amekabidhiwa mikoba ya kutembeza fomu za kusaka wadhamini katika mikoa 10 nchini akishirikiana na baadhi ya viongozi wa Jumuiya ya Baraza la Kuu la Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) na wanafunzi kutoka Vyuo Vikuu nchini.

Kwa mujibu wa chama hicho ni kwamba Ridhiwani ndio atakuwa mwenyekiti wa kamati hiyo akishirikiana na Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Beno Malisa ambao watawaongoza vijana wngine 32 kuzunguka katika mikoa hiyo ambayo imegwanywa katika kanda nane ikiwemo Kanda A ya Dar es Salaam ambayo kiongozi wake ni Ridhiwani pia.

Tukio la Ridhiwani kukabidhiwa fomu za kuomba wadhamini lilifanyika Mjini Dodoma leo mchana, baada ya rais kukamilisha tukio la kuchukua fomu asubuhi ambalo lilifanyika Makao Makuu ya CCM na kasha kufuatiwa na kukutana na wadhamini 250 wa Mkoa wa Dodoma.

Akizungumza mbele ya Rais Kikwete , Katibu Mkuu wa UVCCM, Maltin Shigela alisema vijana hao ambao viongozi wa jumuiya, makada na wanachama makini watazunguka katika maeneo hayo ambapo kila mkoa wanatakiwa kupata wadhimini 250 na hiyo inatokana na kwamba mgombea wao kutokana na majukumu kuwa mengi hivyo hataweza kutafuta wadhimini yeye mwenyewe.

Alisema katika mgawanyo huo wa kanda kila kila itakuwa na vijana wanne ambao watashirikiana kuhakikisha wanalifanikisha suala hilo kwa wakati lakini pia kwa umakini mkubwa.Wakiwa huko maeneo ya mikoani watapata ushirikiano mzuri kutoka kwa wanachama.

“Katika kutafua wadhamini, chama kimeamua kutoa jukumu la kufanya kazi hiyo kwa vijana wetu wachama nkutoka jumuiya yetu lakini pia tunao wasomi kutoka vyuo vikuu vyote nchini ambapo walipatikana kwa utaratibu maalumu.Mwanzoni walikuwa 90 lakini tumeamua hao 32 ndio watafanya kazi hiyo,”alisema Shigela.

Kwa mujibu wa taratibu za chama Rais Kikwete aliamua kukabidhi fomu hizo kwa Ridhani ikiwa ndio ishara ya kuanza safari ya kwenda huko mikoani kwa ajili ya kutafuta wadhamini hao.

Rais Kikwete akizungumzia sababu za kuamua kumpa fomu Ridhiwani ili ashirikiane na vijana wenzake, alisema sababu kubwa inatokana na kwamba akimpa Ridhiwani itakuwa rahisi kuwasiliana naye na atakapomuhitaji itakuwa rahisi kumpata tofauti na mtu mwingine.

Alisema kazi ya kuomba wadhamini ni kubwa na inahitaji muda wa kutosha na kwa muda alionao sasa na majukumu yaliyopo mbele yake ndio maana ameamua kuomba vijana hao wasomi kuifanya kazi hiyo ambapo anaamini itafanyikla vizuri kwa sababu vyuo vimefungwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 21 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 22, 2010

    mambo ya kina Clinton na bush haya !! hope mmenielewa wazalendo !! tutakika kweli

    ReplyDelete
  2. PETER NALITOLELAJune 22, 2010

    RIDHIWANI TUNAKUSUBILI KUCHUHANA NA NABII YOHANA MASHAKA. RAIS WA2015 KWA HIYO KAMA UNAANZA KAMPENI LEO HII, YEYE NI MUSOMI WA MUZUMBE NA ALISHAANZA KAMPENI ZAMANI SANA. UNAJUA HAWA WATU WA MUZUMBE WASOMI KAMA MASHAKA, JK, HASHEEM NA MICHUZI NI WATU WAJNJA SANA. WAPO MEBLE ZETU KWA KARNE KADHAA KWA HIYO NA WEWE INABIDI UENDE KULE CHUO CHETU KIKUU CHA KULE MOLOGOLO UKAPATE DIGILII YA UCHUMI ILI UMSHINDE NABII 2015 HETI. YULE MUTOTO NI MAKINI SANA, KWA HIYO INABIDI UANZE KUJIFUNZA SELA ZA DHIDHIEMU MAPEMA TU, MIMI YANGU TAYALI KWA SABABU MIMI NDIO WAZIRI WA UCHUMI 2015 KWENYE SEREKARI YA MASHAKA WA MUZUMBE NA SHAYO WA WEST BANK UNIVESITY

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 22, 2010

    Chama kimegeuka Kingship...

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 22, 2010

    Ankal you know what??!!!. Unapoweka maoni yetu kupini unakuwa haumsaidii mjadiliwa bali unakuwa unammaliza kabisaa. Kwsababu sisi tunasema ukweli pale tunapoona hapajaenda sawa kwa mjibu wa maono yetu,ili awamu ijayo aweke mambo sawa zaidi, hata yeye mwenyewe analijua hilo na kulipokea kwa mikono miwili.Tunampenda ndiyo maana tunampa huo ushauri,ni kwa uzuri tu Ankal.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 22, 2010

    To me, it looks like 'Introduction to Biology'!

    ReplyDelete
  6. The approach used by his excellence is no doubt a rational because to get a needed number of sponsors, and feedback of what is goin on in the whole process,ya need to have the closest person you can get;here comes is son who happens to be an active young talented politician of our time.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 22, 2010

    DUH!!!! HUYO NDUGU PETER NALITOLELA KWA KWELI INABIDI ARUDI DARASANI.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 22, 2010

    JK katudanganya kuwa kumpata Rizi ni rahisi kuliko mtu mwingne,ina maana watu anaofanya nao kazi daily wanamzingua linapokuja suala la mawasiliano. mfano hiyo kazi angenipa mimi jana pale ddm sidhani kama ningemyeyusha kimawasiliano.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 22, 2010

    umepotea njia Rais wangu hata mfanyeje hapa si zanzibar,umetawala wewe kwa kuwaficha mafisadi huyo mwanao unapoteza muda tu na ataishia huko huko CCM wanakofuata upepo. tushajua janja ya nyani rais mzima eti sbb ni raisi kumpata. we ni raisi bana yeyote yule ukimtakaatapatikana kwa wakati. SASA WEWE MISOOP NA WEWE UBANE HII MAANA TUSHAKUSTUKIA NA WW UNAFANYA KAMPEN HUM GLOB YA JAMII

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 22, 2010

    Huyo Mkware Miraji Kikwete, aliyeoko nyuma ya Ridhwan, ameoa? Anaonekana yuko cool sana. Ameoa?

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 22, 2010

    wana nchi wa tanzania ni ma cowards !wazalendo walisha kufaga! ujinga kama huu nchi kama kenya au ... wawawezi kukubali ujinga !! uncle kamau uko wapi ?? boss michuzi usinibanie hila mimi na uchungu wa nchi yangu na watu wanaogopa kuongea ukweli tunapo kwenda sipo!!watalamu na wasomi awataki kurudi nyumbani nchi hinabaki kutawaliwa na mafisadi !!

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 22, 2010

    THIS NEWS IS VERY GOOD.First comes family for such important job.It is a very wise decision.Wish you all the best.CCM needs patriots not traitors.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 22, 2010

    Yale Yale ya viongozi wa kisiasa kutoka kutawala nchi kama family business yao.

    Baadaye huyu Ridhiwani naye atakuja kugombea urais wa Wadanganyika.

    ReplyDelete
  14. "NEPOTISM" is my greatest fear!

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 22, 2010

    mdau wa kwanza na kupata, kuhusu ankal kwa kweli huwa anaboa sana hii mambo ya kubana meseji anapenda hasa mtu ukiwa muwazi kwani hii blogu ni ya mafisadi? mbona za matusi unaachia??

    ReplyDelete
  16. chakubangaJune 22, 2010

    Here we go again, I am getting impression it is an attempt to turn a democratic republic country into a monarchy, just like what Kabila and Bongo seniours did in Congo and Gabon respectively.
    We need to be careful and very open to each other, other wise we will end up into deep trouble.

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 22, 2010

    DUNIA SASA IMANI IMAKWESHA NDIOMAANA NIMEAMUA KUMTUMA MWANANGU UCHAGUZI ULIOPITA OHHH MLINIPAGA SANAAA

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 22, 2010

    I am worried about country's destiny.....naona tusikae kimya...hebu tupigane jamani...hii ni hatari. Sio nnchi ya kifalme hii.Uozo namshangaaa mtoto wa MKULIMA kuwa katikati ya kundi la MAFISADI..Inaniumaaaa saaaana mjomba.

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 22, 2010

    huyu kwanza hapa nauzwa, lakini muda wake ukifika, hatafulia dafu. kuna watoto wa wakulima makina kishenzi ambao hawawezi hata siku moja. huyu sidhani anaweza kupata kura hata moja akisimamishwa na mashaka john. wakulima hacheni kupiga makelele, mtayarisheni mtu wenu ili wamkabili dogo badala ya kelele, vinginevyo mtamuona anapewa ufunguo wa pale kivukoni huku mnatizama

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 22, 2010

    ukoo wa wanasiasa
    kikwete
    pera
    mbilimbi
    nyanaya
    babu
    baba
    mtoto
    mjukuu
    kitukuu
    kitunguu
    kikwete again.

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 22, 2010

    mtake msitake jk ni raisi tu hata hizo fomu akabidhiwe nani?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...