Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Liberia anaeondoka madarakani,Bi Elizabeth Mlangwa akimkabidhi bendera ya Taifa Afande John Minja ambaye amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya watanzania nchini Liberia.
Baadhi ya watanzania waishio na kufanya kazi nchini Liberia katika picha ya pamoja na viongozi wapya waliochaguliwa hivi karibuni.
Na Meshack Mfugale wa Globu ya Jamii,
Monrovia - Liberia
Watanzania waishio na kufanya kazi nchini Liberia wamepata viongozi wapya katika uchaguzi ulifanyika hivi karibuni katika eneo la Coconut Plantation jijini Monrovia, Liberia.
Katika uchaguzi huo uliojumuisha watanzania wanaofanya kazi katika taasisi/mashirika mbali mbali ya kimataifa nchini Liberia, Bw. John Minja kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jijini Dar es Salaam ambaye kwa sasa anafanya kazi na Umoja wa Mataifa jijini Monrovia alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania nchini Liberia, nafasi iliyokuwa ikishirikiwa na Bi. Elizabeth Mlangwa.
Dk. Bwire alichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa jumuiya, nafasi iliyokuwa ikishirikiwa na Bw. Deusdedith John Kitambi.
Nafasi ya ukatibu mkuu wa jumuiya ilichukuliwa na Bi. Judith Mshiu. Awali nafasi hiyo ilikuwa ikishikiriwa na Bw. Salumeza Kanuti.
Bw. Athman Sharif alichaguliwa kuwa Mweka hazina wa jumuiya.
Viongozi wapya watakuwa madaraka kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Juni 2010 hadi Juni 2011.
Shughuli ya kuchagua viongozi wapya ilienda sambamba na kuwakaribisha watanzania waliowasili nchini Liberia siku za karibuni pamoja na kuwaaga watanzania wanaotarajia kuondoka nchini Liberia hivi karibuni.
Watanzania waishio na kufanya kazi nchini Liberia wamepata viongozi wapya katika uchaguzi ulifanyika hivi karibuni katika eneo la Coconut Plantation jijini Monrovia, Liberia.
Katika uchaguzi huo uliojumuisha watanzania wanaofanya kazi katika taasisi/mashirika mbali mbali ya kimataifa nchini Liberia, Bw. John Minja kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza jijini Dar es Salaam ambaye kwa sasa anafanya kazi na Umoja wa Mataifa jijini Monrovia alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania nchini Liberia, nafasi iliyokuwa ikishirikiwa na Bi. Elizabeth Mlangwa.
Dk. Bwire alichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa jumuiya, nafasi iliyokuwa ikishirikiwa na Bw. Deusdedith John Kitambi.
Nafasi ya ukatibu mkuu wa jumuiya ilichukuliwa na Bi. Judith Mshiu. Awali nafasi hiyo ilikuwa ikishikiriwa na Bw. Salumeza Kanuti.
Bw. Athman Sharif alichaguliwa kuwa Mweka hazina wa jumuiya.
Viongozi wapya watakuwa madaraka kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Juni 2010 hadi Juni 2011.
Shughuli ya kuchagua viongozi wapya ilienda sambamba na kuwakaribisha watanzania waliowasili nchini Liberia siku za karibuni pamoja na kuwaaga watanzania wanaotarajia kuondoka nchini Liberia hivi karibuni.
Ankal hivi kuna nchi ambayo wabongo wanakosekana hapa duniani kweli?Naomba upost na umoja wa wabongo wanaoishi Afghanistan najua wapo wengi tu huko.
ReplyDeleteSafi sana !
ReplyDeleteAsante Ankal kwa kutuhabarisha. Poa kweli, Wabongo wamezagaa kila kona ya duniani !
ReplyDeleteHaya ndiyo mambo yanayotakiwa,siyo wale walioshindwa maisha wanafungua matawi ya CCM.
ReplyDelete