LEO NI MIAKA 3 KAMILI TOKEA MH. AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIA (PICHANI) ATUTOKE. KIFO CHAKE, KILICHOTOKEA GHAFLA, KILITIKISA NCHI NZIMA NA WATANZANIA WOTE KWA JUMLA YAO WALIBAKI MIDOMO WAZI KWA KUONDOKEWA NA MBUNGE HUYU KIJANA ALIYEJIPATIA UMAARUFU KWA MENGI, KUBWA LIKIWA MSIMAMO WAKE WA KUPAMBANA NA JANGA LA MADAWA YA KULEVYA. NA LEO, IKIWA NI SIKU YA KUPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA, GLOBU YA JAMII INAJIUNGA NA WANAHARAKATI KAMA AMINA CHIFUPA KUADHIMISHA SIKU HII HUKU TUKIMKUMBUKA MWAHARAKATI HUYU.
ASUBUHI HII KUTAKUWA NA HAFLA YA KUADHIMISHA SIKU YA KUPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA KITAIFA ITAYOANDALIWA NA TUME YA MADAWA KUPAMBANA NA MADAWA YA KULEVYA ITAYOFANYIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA AMBAPO MGENI RASMI ANATARAJIWA KUWA WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU, MH. PHILIP MARMO. HAPANA SHAKA JINA LA AMINA CHIFUPA LITAKUMBUKWA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. KARUME JAMARIWAJune 26, 2010

    OOH JAMANI AMINA AMEFARIKI? JAMANI NINI TENA, OOH ALIKUWA MTU WA WATU NINI JAMANI KIMEMKUTA MARA YA MWISHO ALIKUWA AWATAJE WAUZA UNGA SIKUMSIKIA TENA NA HILI BOX LETU HAPA UFINI LILIKUWA GUMU SANA SASA LEO NAFUNGUA MICHUZI NAKUTANA NA HII HABARI YA KUHUZUNISHA SANA POLENI JAMANI KINA MEDI NA FAMILIA YA MAREHEMU

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 26, 2010

    Dah ni kama jana alipoondoka huyu dada.Anyway,ndo dunia kuna kuzaliwa na kufa.Life goes on.Misupu na wewe chunga usitake wakuchifupe kwa kuungana na mambo haya.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 26, 2010

    Ankal, Samahani kama nimekosea. kwa kumbukumba zangu Amina alifariki dunia mwaka 2007, yaani miaka mitatu iliyopita. Kama nimekosea naomba nisahihishwe. Amina, we will never forget you. RIP. Nachukua fursa hii kuwalaani wauza mihadarati/madawa ya kulevya. They will not get away with it! Amandla!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 26, 2010

    Ankal sio miaka 4 bana ni 3.Hebu rekebisha hapo juu.Anyway Amina jamani uliondoka bado mbichi kabisa, jamani kifo hakina huruma. Kila aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi hapa duniani ni chache. Hivyo jamani tukumbuke kuna kufa kesho hivyo tufanye matendo mema hapa duniani.RIP Amina chifupa.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 26, 2010

    Mdau karume wa ufini.Napenda kukupa taarifa na Mohamedi Mpakanjia nae ameshafariki.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 26, 2010

    mdau wa kwanza hapo juu ni kweli kipenzi chetu keshatangulia mbele za haki ni mda tu sasa, na mumewe medy hatunaye tena naye keshatangulia mbele za haki mwaka jana, Mungu awarehemu, amen

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 26, 2010

    Michu, jamaa yangu mmoja ni mkemia (chemist). yeye anashuku kuwa dalili zilizosababisha kifo cha Amina ni za zile ambazo kwa kingereza zinaitwa 'arsenic/heavy metal poisoning symptoms' ambazo hata huku USA haziwezi kutambulika katika maabara za kawaida. Kama alivyosema mdau wa tatu hapa juu, wauza unga ni watu ambao hawafai kabisa. tazama huko mexico na colombia wanavyofanya unyama. wauza unga ni watu wa shetani lucifer na wana laana. AMINA RIP.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 26, 2010

    R.I.P dear amina,Yako mbele yetu nyuma,tumuenzi kwa yale mema aliyopigania mendwa wetu,Mdau wa kwanza pole sana kwa kutopata taarifa mapema ila huzuni zaidi ni kwamab hata MED hatunae tena ametangulia mbele ya haki!wameacha mtoto yatima!Allah amlinde kwa kila jambo.Inshaallah!
    zawadi.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 26, 2010

    We KARUME huyo "Medi" naye uneyempa pole kafa. Sasa ndugu yangu ata kama Box uwe unapitia vyombo vyetu ata kwa vichwa vya habari, sie wenyewe tukirudi Box angalau dk 2 tunapoteza kuangalia yaliyojiri. Siku ingine utasikia ...kafa pia na usijue.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 26, 2010

    Ankal Mithupu umekosea bwana...usiseme tangu atutoke..ila tangu wamuondoe.....nadhani hiyo ndo sahihi kabisa..

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 26, 2010

    anonymous wa kwanza hapo juu pia Medi alifariki. RIP Amina and Medi

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 26, 2010

    Mwanamke shujaa, anayejiamini ambaye ndoto zake zimezimika ghafla na kutoweka katika uso wa dunia hii, kila nikisikia jina lake au kuona picha yake, moyo wangu unaumia sana, kamwe sitomsahau, mungu amsamehe mazambi yake na amuweke mahala pema.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 26, 2010

    tunamuombea ALLAH ampunguzie adhabu za kaburi inshaallah. Kila nafsi itaonja umauti tufanye maandalizi inshaallah

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 26, 2010

    Jamani nimesikitishwa sana na comment za huyu mwenzetu mbeba box wa UFINI kuhusu kifo cha dada yetu Amina Chifupa, napenda kumjulisha tu kuwa hata huyo Medi unayempa pole naye ni marehemu (RIP. Pole sana mtoto Rahman, pamona na kukosa wazazi wote Mungu atakusaidia.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...