Msanii wa Bongo Flava Mr. Blue ameigiza katika movie yake ya kwanza akiwemo waigizaji maarufu kama Lucy Komba, Mzee chilo, Idriss(kwenye movie ya fedheha). Movie hiyo ambayo bado haijaanza kuuzwa mtaani, inaenda kwa jina la "PRETTY TEACHER". Director wa movie ni Goodluck Komba
Mr Blue na waigizaji wenzie
Mr Blue akiwa lokeshen



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 17, 2010

    Hivi wabongo wenzagu mkiweza kuzipa majina ya kiswahili hizi muvi zenu mtapungua wapi? jina ni la kidhungu matamshi ya ndani kiswahili ! wapi na wapi mbona wahidi wanaweka majina ya kihindiii?? zindukeni wacheni ushamba

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 17, 2010

    Mmh! Tasnia ya filamu imeingiliwa. Kila anayeshindwa kwenye fani yake anahamia kwenye filamu. This is too much maana wengine hawana vipaji wanaenda kuuza sura!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 17, 2010

    Jamani...Hivi huyu Mr. BLUUU si alikuwa mwimbaji,!! Sasa nini kimetokea huko hadi anawaingilia kina "KANUMBA-The GREAT" katika fani zao...Unajua hili ndilo tatizo la wasanii wa Bongo..hakuna shule ya kuwapa uelewa wa namna ya kuchagua fani, leo atakuwa mwanamuziki, kesho maigizo, keshokutwa sarakasi ....then taarabu nk.nk,
    Haya "BWANA BULUUU"

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 17, 2010

    jamani wabongo wenzangu je umajua maana ya mwanamme kuvaa herini sikio moja? au mnafanya fashion tuu, na kuiga majuu, wenzenu huku majuu wamechanganyikiwa kinoma noma na ukiangalia hawana ustaarabu kama tulio nao sisi na mila na tamaduni zenu na kulelewa vema na wazazi wawili.

    so jamani angaliyieni sana mambo ya kuiga style na ma fashion ya majuu..

    hamuwaoni wenzenu wachina,wajapani wahindi, hawaigi igi ovyoo vitu vya kijinga jinga, hasa hasa wachina na wajapani.

    mkeni wasani,waugwana wenzangu. shauri yenu.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 17, 2010

    Thu Jun 17, 09:26:00 PM umeongea point lkn ulipoanza kutaja hizo nchi umetapika point zote, wahindi nionavyo ndio wanaongoza kwa mahereni,china, japan wanapenda sana uzungu na wanavaa sana hayo madudu

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 18, 2010

    HERENI??
    ACHENI USHAMBA JAMANI. KUNA TATIZO GANI MTU KUVAA HERENI? NI FIKRA POTOFU ZILIZOPITWA NA WAKATI SAWA NA ZAMANI WALIPOKUWA WANASEMA MWANAUME HAPAKI MAFUTA WALA LOSHENI USONI.
    MRU KAMA ANAONA ANAPENDEZA NA AVAE CHOCHOTE ANACHOTAKA ILI MRADI HATEMBEI UCHI.HAO WAMASAI WALIOJITOBOA KILA MAHALI MBONA HAMUWASEMI?
    ACHENI USHAMBA, JIPAMBE UPENDEZE NA KUFURAHIA MAISHA YAKO KABLA HUJAFA. LIFE IS ONCE, ENJOY NA PIA UMKUMBUKE MUNGU WAKO!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 18, 2010

    Hi Lucy, hongera sana, we support you billions times, we adore you, we support you, we love you, you are my susper star, says shefuuu.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 18, 2010

    siku hizi msanii wa bongo flava akishindwa fani anakimbilia kwenye uigizaji kuuza sura tu. hakuna lolote wanaloigiza zaidi ya kuuza sura, tumechoka nao.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 18, 2010

    'Nifanye nini, Uniwlewe?', 'Nikepe nini ili niwe na wewe?'.

    'Usiku silaaali!, nakuwaza wewe!'.

    Maisha ni kujaribu dogo, so keep it up! GET RICH OR DIE TRYING!

    Nakutakia kila la kheri.

    Kama napo kwenye hiyo fani ya filamu hautatoboa kihivyo, no worry, jaribu na fani nyingine tena, say, ya taaluma, n.k, n.k.

    Mmetoka chicha sana hizo picha zenu.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 18, 2010

    wewe Bruuuu, cjui bluuuu naenda kuesabua mpaka tatu na ninataka kwenye tatu huwe tiali umesharudi kwenye fanii yako ya kuimba...Jamani ya vi watu vyengine havijui maana ya "Specialisation" yani you specialise in what you do best and leave others to do what they do best" fanii ya ugizaji niya kina kanumba na wewe yako ni kuimba mapozi na we, we na mapozi na we.!we mbona kanumba hajawai hata siku moja kuenda kwenye fanii ya music..kwasababu hanajua ku specialise...Shauri Zako dogo, utajiabisha bure kwenye Africa magic plus na english yako am sure 0%...Ushauri wangu, nenda ukajicheck vizuri...je, ni nini ninacho kitaka....??u-barman, kuimba, kusoma kama umeshindwa basi Hokoka dogooo....Kila la kheri kwenye kujisearch carrier yako...

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 19, 2010

    Blu anachofanya ni sahihi jamani, msimshambulie na kumkatisha tamaa. Dogo, wewe kaza mwendo tu, hata wanamuziki wa mamtoni tunawaona kila kukicha kwenye movies. Kama vipi tuo wimbo uuite "Blu diversifies" kuwaelimisha hawa wanakupinga. Mi nadhani wanakuonea wivu au pengine wanakugwaya tu, achana nao.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...