Marehemu Elizabeth Mlilingwa enzi za uhai wake
Marehemu siku ya harusi
Marehemu na wanae wakati wa uhai wake
Familia ya Mlilingwa inasikitika kutangaza kifo cha mama yao mpendwa Bi.Elizabeth Mlilingwa kilichotokea huko katika hospitali ya TMJ Dar es salaam Tanzania Juni 15,2010 saa 3.30 asubuhi.
Bi Elizabeth alizaliwa December 25,1961.

Hivi sasa watoto wa marehemu wapo Atlanta Georgia wanatarajia kwenda kwenye maazishi Dar es salaam Tanzania siku ya Ijumaa iwapo michango itakamilika.
Ili kufanikisha safari yao hii kutakua na Fund raising siku ya Alhamisi Juni 17 katika kanisa la Believers Celebration Center, 1492 Roswell Rd.
Marietta Ga 30062
Unaweza pia kutuma mchango kwenye akaunti namba ni 330 2635 4506 Bank of America.
Kwa taarifa zaidi unaweza kuwasiliana na:
Neema Maleto 770 827 078
Mary Matuja 678 472 6320
John Kazilwa 678 362 8238
Togo 678 313 1805
Joyce Mbeyela 678-415-3667.
Sisi tulimpenda lakini Bwana alimpenda zaidi.
Bwana ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
-Amen.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. AMEN.

    Poleni wanafamilia, ni habari ya kusikitisha. Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 17, 2010

    Dada yetu Eliza tulikupenda lakini Bwana alikupenda zaidi.
    Tunakuombea kwa Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Wewe umetangulia tu, sisi sote tupo safarini.
    Jina la bwana na lihimidiwe.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 17, 2010

    Upumzike kwa amani KABURINI mpaka siku ya kiama kwa Neema ya Bwana akufufue. Poleni sana wafiwa.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 18, 2010

    POLENI SANA. MUNGU AMLAZE MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI.
    USHAURI KWA WENZETU MLIOKO MAJUU. MKO MBALI NA NYUMBANI BASI NUNUENI BIMA ZA VIFO/MAZISHI ILI IWERAHISI KUGHARAMIA GHARAMA ZA USAFIRI NA MAZISHI BALADA YA OMBA OMBA. SISI HUKO HOME TUKO HOI. GHARAMA ZA KUSAFIRISHA KUTOKA HUKO NI ZAIDI YA BEI YA NYUMBA SINZA HAPA HOME SINZA.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 18, 2010

    mdau wa Fri Jun 18, 09:02:00 AM kwanza kabisa kwani wewe umesoma wapi elimu yako? huoni kama tangazo hili linasema kabisa kama kifi kimetokea nyumbani tanzania?

    Michango inayoitishwa ni kuwasaidia wafiwa ili waweze kufika nyumbani haraka.

    Na hiyo bima unayoishauri inunuliwe wapi? yaani unataka kuniambia kuwa mtu awe na insurance ya kuwa akifa asafirishwe nyumbani, unadhani bima ya namna hiyo kama ukiipata unadhani itakuwa rahisi?

    Watu nyumbani ndio huwa wanasisitiza sana miili ya marehemu kurejeshwa nyumbani, lakini nadhani ni rahisi zaidi kama watu wakiwa wanazika huko huko kunakotokea kifo ikiwa wafiwa hawana uwezo, hakuna umuhimu sana wa kuleta mwili nyumbani. kuna msemo unasema "unapofia ndipo palipo udongo wako" ukimaanisha mahali/ nchi unayokufa ndipo palipo kaburi lako.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...