Meneja wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule (wa pili kushoto)akifurahia jambo na wauguzi wa hospitali ya Wilaya ya Iramba iliyopo Kiomboi Mkoani singida baaada ya kukabidhi msaada wa Vyandarua 1,300 katika mkoa huo vyenye thamani ya shilingi Milion 10 katika hospitali hiyo.
Meneja wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule (kushoto) akimkabidhi moja ya kati ya Vyandarua 1,300 Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Iramba iliyopo Kiomboi DK.Anthony Mburu (katikati)Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iramba Peter Mwagiro akishuhudia upokeaji huo wa Msaada ambao watagawiwa wagonjwa wote waliopo eneo hilo. Meneja wa Vodacom Foundation Yessaya Mwakifulefule akimkabidhi moja kati ya 1,300 Esta Aron akiwa na mwanae mwenye umri wa miezi 6 Peter William ambaye ni mmoja wa Wagonjwa waliolazwa katika Wodi ya akina mama katika hospitali ya Wilaya ya Iramba ilioko Kiomboi Singida mfuko huo ulitoa msaada wa jumla ya Vyandarua 1,300 katika mkoa huo.
Baadhi ya Wauguzi katika hospitali ya Wilaya ya Iramba wakibeba magunia yaliyosheheni Vyandarua 1,300 baada ya kukabidhiwa msaada huo na Vodacom Foundation kwa ajili ya kujikinga na malaria kwa wagonjwa wanaopata matibabu katika Hopitali hiyo iliyopo Kiomboi Mkoani Singida .




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...