Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Idd Kipingu, akizungumza wakati wa kufungua semina ya wahariri wa habari za michezo iliyoandaliwa na kampuni ya Keen Arts na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania, kwenye ukumbi wa hoteli ya Giraffe Ocean View Resort, jijini Dar leo.
Mkuu wa Udhamini wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania, George Rwehumbiza, akitoa mada juu ya udhamini wao katika michezo mbalimbali nchini, wakati wa semina ya wahariri wa habari za michezo iliyoandaliwa na kampuni ya Keen Arts na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania, kwenye ukumbi wa hoteli ya Giraffe Ocean View Resort. Sehemu ya wahariri wa habari za michezo wakifuatilia semina Super Coach Sylvester Mziray akiwa na wahariri wa habari za michezo wakifuatilia semina

Mtaalamu wa Mambo ya Habari wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu, akirekodi majadiliano yaliyokuwa yakiendelea wakati wa semina ya wahariri wa habari za michezo iliyoandaliwa na kampuni ya Keen Arts na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania, kwenye ukumbi wa hoteli ya Giraffe Ocean View Resort Wahariri toka ITV
Wahariri wa michezo Bw. Mbugun wa Majira na Grace Hoka wa Mtanzania

WADHAMINI wakuu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, wamesema wanatarajia kuweka wazi mkataba wao mpya watakaoingia na Shirikisho la Soka Nchini (TFF), kabla ya kuanza msimu mwingine wa ufadhili wake.

Vodacom inatarajia kumaliza mkataba wake wa miaka mitano wa kudhamini ligi hiyo mwakani.

Akizungumza jana katika semina elekezi ya Wahariri wa Habari za Michezo, iliyoandaliwa na Kampuni ya Vodacom Tanzania, Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania, George Rwehumbiza, alisema nia ya kuweka mkataba huo wazi ni kutaka kuifanya ligi hiyo kuwa na uwazi kwa klabu shiriki pamoja na wadau wengine wa soka.

Rwehumbiza alisema kumekuwepo na maoni mbalimbali juu ya kuwepo kwa uwazi wa mkataba wake wa ligi hiyo kusema hivyo ni lazima mdhamini aheshimu maoni ya wadau wake ambazo ni nguzo ya maendeleo ya soka kwa ajili ya kuimarisha.

Alisema baada ya kuweka wazi udhamini wake, klabu zitapata nafasi ya kujua zinapata na kupokea nini kutoka kwa mdhamini wao huku TFF nayo ikipaswa kujua mipaka ya kazi zake na umuhimu wa mdhamini katika ligi hiyo.

Alisema mbali ya hilo, wanatarajia kufanya marekebisho baadhi ya vifungu katika mkataba ujao ikiwa ni pamoja na kujadili mapungufu ambayo yamejitokeza katika mkataba utakaomalizika.

Alisema ni kweli kuna mapungufu katika mkataba wake wa sasa lakini mapungufu hayo ni lazima yafanyiwe marekebisho kwa kuwa kila kitu kinahitaji kukosolewa kabla ya kuboresha zaidi.

Katika semina hiyo, waandishi walitoa maoni mbalimbali juu ya udhamini wa kampuni hiyo huku wakitoa ushauri wa jinsi ya kuboresha michezo mingine kwa ujumla na kutambua umuhimu wa ushirikiano baina ya mdhamini na vyombo vya habari.

Semina hiyo ya siku mbili ilifunguliwa rasmi na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Taifa(BMT)Idd Kipingu na lengo likiwa ni kuwapa wahariri wa habari za michezo kujua wajibu wao wa kazi pamoja na kutambua umuhimu wa michezo katika jamii.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 08, 2010

    Huyo dada picha ya mwisho anahaingaika na simu matokeo yake yataonekana kwa yatakayoandikwa ktk gazeti lake!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 09, 2010

    Namuona sapa kochi anaandika makala ya kumlaumu kocha mpya wa staz kabla hata hajaanza mzigo. Maximo oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 09, 2010

    Wahaariri wawili hawajatulia katika semina!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...