IF YOU HAVE A PLOT WITH TITLE DEED
We are looking for individuals who have got plots with title deeds in and around Dar-es-salaam and with regular income.

We have teamed up with one of the reputable banks in Tanzania to construct one house which will be used as a sample house for a new construction technology.

If you would like us to construct a 78sq/m two bedrooms house on your plot please send us the following information about your plot:
The location
The size
Any other necessary information.
Please send the information on the following address
P.O Box 14131
Dar-es-salaam
Tanzania
Email: nyumba.bora@gmail.com
--------------------------------------------------------
WADAU WENYE VIWANJA
VILIVYO KUWA NA HATI MILIKI
Tunatafuta wadau wenye viwanja vilivyokuwa na hati miliki vilivyopo Dar-es-salaam na maeneo ya karibu na wenye vipato.
Tumeingia kwenye makubaliano na benki moja maarufu Tanzania kujenga nyumba ya mfano kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Kama utapendelea tukujengee nyumba kwenye kiwanja chako tafadhali tutumie ujumbe ukiambatana na vifuatavyo;
Sehemu kiwanja kilipo
Ukubwa wa kiwanja
Maelezo zaidi kuhusu kiwanja
Tuma kwenye anuani hii
S.L.P 14131
Dar-es-salaam, Tanzania, barua pepe:
nyumba.bora@gmail.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 14, 2010

    Wewe ndugu maeneo ya watu wenye vipato ndio kama yepi?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 14, 2010

    Dah Mdau hapo juu...ulikuwa unasoma kwa haraka nini... kma umeshindwa elewa kiswahili soma tafsiri ya kinyamwezi hapo juu

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 14, 2010

    vitu kama hivi huwa vinawekwa bayana tangu mwanzo, sio wewe unaanza kufucha hata bank mlioingia nayo mkataba, hii inaonyesha jinsi gani makampuni mengi ya bongo yanataka kuwaliza watu. Nashauri wenye plot wawe makini sana na hili suala.

    ReplyDelete
  4. mnaanza kuingilia kazi za NSSF


    kama mnataka muonekane mko serious toweni website yenu halafu haya mambo gmail au yahoo hakuna atakaye kupeni kitu

    huwezi kutuambia kuwa mnataka kujenga nyumba za kisasa kwa modernday technology halafu hamuna website
    http://www.wazalendoforums.com/index.php

    ReplyDelete
  5. Ngw'anakilalaJune 15, 2010

    Hawa jamaa matapeli, mbona hawana hata website wala credentials.
    Ukisikia watu wanataka kukutapeli mchana mchana ndo hawa!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 15, 2010

    jamani kwani mnashindwa kufungua hata ka website na mtoe details za kueleweka? kwa maelezo mliyotoa sio rahisi for any serious person kuwaamini,anything involve money lazima seriousness iwepo,toeni details zote kuanzia hiyo technology,the bank involved,where is your office/physical contacts,pictures etc na hayo yanawezekana kama mkifungua website yenu.kama mna nia nzuri mtafanya hivyo la sivyo hakuna mtu na akili zake anaweza kuwaamini...fanyeni kazi na muache blah blah za kupenda mikato sijui hata hiyo bank mlitoa maelezo gani mpaka mkapewa hizo funding...get serious!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 15, 2010

    Brother Michuzi,naona unaanza kuleta matangazo ya matapeli sasa; yaani watu wamepata pesa kutoka kwa benki moja maarufu isiyo na jina, na jina la kampuni yao ni nini? na wako wapi?
    Ndugu zangu wananchi, you have been warned, mkituma tu hivyo vi majina vyenu na mahala palipo viwanja vyenu mmekwisha.Watu wanabidilisha hayo majina pale ardhi zitatolewa title deed nyingine watu mbaki kulia tu.
    Jaamani eeh, there is nothing free in this world, absolutely nothing, mtakuja kulia humu.
    Brother Michuzi, huu ni utapeli na kama huamini tulia kuna watu watakuja humu wanakulilia wametapeliwa viwanja vyao.
    Mdau

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 15, 2010

    Samahan nilikuwa nnataka kufahamu baada ya hiyo nyumba kujengwa. Mwenye kiwanja anafaidika na ki2 gan>>?

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 15, 2010

    Ndugu, mimi nina shamba ekari mbili lipo kinyerezi kifuru na hivi majuzi halmashauri wameliingiza katika town master plan na wamefanya valuation.
    Je mnaweza kujenga hapo kwa makubaliano maalum juu ya gharama zote zikiwamo za kuandikisha ardhi na kupata hati?
    Napatikana kwa 071 321 1726

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 15, 2010

    Wezi hawa, wanataka kubadilisha mambo, michuzi, angalia mail za kutoa, maana hawa ni dhahiri matapeli

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 15, 2010

    DUUUUUUUUUUUUUUUU!! Yaani mradi wote huu hauna hata DOMAIN NAME mnatumia GMAIL!! Hapo ndio mashaka yanapokuja, huu ni utapeli flani jamani tuwe macho.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 15, 2010

    Nyumba ya mfano?? oote mbeee! ni watu gani hawa wana uwezo wa kumiliki kampuni halafu wanakosa sehemu ya kujenga nyumba ya mfano? na huo mfano wa nyumba ni mpaka ujengwe? heee mbona ramani inajitosheleza, acheni utapeli nyinyi kama mji umewashinda rudini kwenu, haa au ndio nyumba ya mfano kesho na keshokutwa kiwanja kinatembea. mna kichaa nini nyie?

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 15, 2010

    inaweza kuwa ni good idea, ila maelezo ni kama hayajanyooka vile, even if ur serious hembu nyooosheni maelezo kidogo ili mueleweke, naamini kila mtu anaweza akawa interesting na hako kamradi, ila watu wangependa jua ni vipi watafaidia ukijenga kwenye kiwanja yake, whats the process where is the physical adress, location....
    instead of giving us the Po Box is soooo tooo 1900 man we far away from those years, make things more legal and more formal PEOPLE NEED IT

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 15, 2010

    aiders and abaters in criminal transations are treated the same by our laws. Michuzi uwe makini, tutakufunga kwa kusaidia wizi. inakuaje hawataji bank? waliogopa hio bank itasema haina kitu kama hicho? DESA limeingia kwenye viwanja

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 15, 2010

    Bongo eeeehh!!!
    Bongo Darisalaaam,
    Utalia lia lia eeeh,
    Bongo Darisalaaam.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 15, 2010

    Jamani tatizo siyo Ndugu Michuzi tatizo ni Elimu, kuna kizazi kimekuwa hapo katikati elimu waliyoipata ni kuiga na kuangalia TV asubuhu mapaka jioni, wanaingia web kama wanapesa na wanaiga kila kitu. Hiki kizazi hakina msimamo wa maisha wakiona kitu wanaiga bila kujiuliza na ndiyo maana wanatowa matangazo ambayo hayana kichwa wal miguu. Kama unataka haya matatizo yasitokee na kutupa aibu zaidi kazana kupigania elimu kwa umma na siyo unapeleka watoto wako private ukifikiria kwamba umesomesha shida huna tena, umesahau kuna kizazi zaidi ya familia yako bado hawaendi hata darasa la kwanza. Elimi Elimu ndiyo inasaidia kuendeleza jamii na siyo kingine.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...