sherehe za ufunguzi za kombe la dunia 2010 zilishuhudiwa kila mahali
wadau kibao walikusanyika Savannah Lounge jijini Dar
kushuhudia gemu la ufunguzi la Bafana Bafana na Mexico

vuvuzela zilitolewa na DSTV kwa wadau kibao walioshuhudia
gemu la ufunguzi Savannah Lounge
savannah lounge palikuwa hapatoshi
gemu likiendelea
wengine ilibidi wakae chini...
wadau wakipiga chabo kwa nje kushuhudia gemu
kwenye luninga la club billicanas







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 12 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 11, 2010

    Kwa mtizamo wangu, Mexico walistahili kushinda ile mechi, sema ndio hivyo tena mpira dakika 90, kwani walicheza mpira wa kiwango cha juu zaidi kulinganisha na Africa Kusini. Africa kusini walionyesha kulemewa kiasi, hata lile goli lao halikuwa la kitaalam kama goli walilofunga Mexico, pamoja na kuwa 'man of the match' amekuwa ni yule aliyefunga goli la Africa Kusini. Africa kusini walizinduka kidogo tu hapa mwishoni.

    Pole kwa Mzee Madiba kwa kufiwa na kitukuu kwa ajali ya gari.

    By the way Wadau, JABULANI maana yake ni REJOICE, nimeinyaka hiyo nikaona sio vibaya ku-share. Naona huo mpira wa Jabulani haukuwaathiri sana wa-Mexico na wa-Africa Kusini.

    Leo nili-Jabulani sana baada ya kumuona Khaled wa Algeria na R. Kelly wakitumbuiza katika sherehe za uzinduzi wa mashindano hayo ya Kombe la Dunia.

    ReplyDelete
  2. ZeroBrainJune 11, 2010

    MIJITU mingine bwana!

    Sasa hao waliojazana hapo mpaka wengine kukaachini kwani majumbani kwao hawana tiivii au?

    Tiivii ziko mpka za mitumba siku hizi hata elfu 50 tu unapata tiivii.

    Khaa!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2010

    We mdau wa Friday Jun 11, 10:31pm! "eti mijitu mingine bwana"! nadhan unajiamin sana kuwa unajua wakati hujui km hujui! unakurupuka tu! afu yaelekea upo nje ya nchi, so ushazoea ukiwa, maisha ya kwenda kubeba box na kurudi kwenye kiota cha ndege(apertment)ukiwa peke yako! Bongo watu kwa raha zao! si km watu hawana TV km akili yako ya kivivu inavyokutuma! watu wanafata company! wewe endelea na maisha yako ya upweke! Raha ya mpira mtizame wengi, mnakuwa km mpo uwanjani live, huyu aongee kile yule aongee lile, ndo raha ya mpira mama/baba! kalaghabao!

    ReplyDelete
  4. wewe unayecoment watu kuwaita mijitu kwahiyo hata hao waongea kingereza (uk)hawana tv mbona wasimama lundo hivyo jibu watu wanafuata company ya watu ili kukuza urafiki mijadala ya hapa na pale kuhusu kome ili la dunia Watch out.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 12, 2010

    wewe mdau wa Fri Jun 11, 10:31:00 PM, uliethubutu kuwaita watu majitu una matatizo ya akili, pia hujui lolote juu ya mpira.

    Kwanza unadhani kila mtu tanzania anauwezo wa kumiliki tv? jee kwa kuwa hawamiliki tv ndio uwaite majitu? huna ustaarabu hata kidogo, na una akili za kitoto sana.

    Nitakusaidia kidogo tu raha ya mpira ni kutizamwa katika mkusanyiko mkubwa na ndio maana wapenzi wa mpira duniani kote (sio kama wewe) huenda kwenye viwanja kuona live au hukusanyika kwenye vilabu, bar au hata maduka ili kuenjoy. watu wamesafiri kutoka mabara tafauti kuja kuona, unadhani hao wote hawana tv makwao?

    Jinga kubwa wewe!!!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 12, 2010

    duh naona kila pembe ya dunia zimemwagwa vuvuzela kwa kwenda mbere.mii mwenyewe nikizama boksini huuua siliaachi vuvuzela langu.nalipiga hadi kinaeleweka udumu ushirikiano mshikamano wa waafrica sote tupo nyuma ya timu zilowakilisha balaa la africa hapo bondeni.AFRICA UNITED OYE OYE OYE

    MDAU KIGALI MAKAZI BOKSINI KUSAKA CHAKE

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 12, 2010

    ZeroBrain umejipa jina limekufaa sawa sawa maana nina hakika bichwa lako ni maji tupu. GROW UP

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 12, 2010

    Michuzi umezidi utani bwana utasemaje wadau wakipiga chabo kila mtu anajua maana halisi ya chabo na huipigiki hadharani kabisa!!!!!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 12, 2010

    Acheni kutoana macho jamani!!! Kwani bars, pubs, za nini??? Uingereza soka linafurahiwa kwenye pubs pamoja na kwamba wote wana wall mounted 50 inch high resolution TVs. Naangalia gemu la south Korea na ugiriki pub hapa! Acheni hizo tu-switch discussions zetu katika kumsisitiza ankal atuwekee pajazzzzzzzzzz na matitizzzzzzzz. Yani nikipata hii kitu sitalala! Nitajishughulisha usiku kucha!!! Yamejaaaa n sina pakuyaweka!!! Help me plz guyz tell ankal tu puti kitoweo!!!!! Ahsanteni sana wote!!!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 12, 2010

    weweeee raha ya mpira company bwana watu tulikuwa tunaacha lcd zetu zimening'inia nyumbani tunaenda paleee q bar manuu inacheza na bwawa au washika binduki ha ha haaa nyomi hiyo nitoleee utadhani tulikua old traford yani ni shangweeeee kwa sana yani natamani kweliiiii namisi hizo shangwe sana ebu na wewe jikusannyeni mahali utakubali raha ya mpira ni kampaniz

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 12, 2010

    kampani fulu shangwe,go go goooo AFRIKAA gooooooo

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 12, 2010

    Nimegundua kuwa mara nyingi majadiliano yeyote kuhusu issue ya nyumbani na nje ya nchi wanaokuwa wanajibishana ni wakuja waliopo uk na waliopo nyumbani wanaotamani kwenda nje lakini wanashindwa!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...