Big Brother All Stars housemates enter house

ankal na wadau walipogongana sauzi wakati
wa uzinduzi wa Big Brother All Stars
ankal akiwa na mtangazaji Kobelo wa M-Net

Ankal ndani ya nyumba ya Big Brother

ankal na mdau toka ethiopia wakivinjari uwani mwa jumba la Biggie
ankal akiwa na waandishi wa kutoka nchi mbalimbali za afrika waliokuwa sauzi kushuhudia uzinduzi wa Big Brother Africa All Stars ambapo walipata nafasi ya kulala kwa usiku mmoja na kupata vionjo vya nini kinajiri wakati washiriki 14 toka nchi 14 watavyoishi humo kwa siku 91 kabla mmoja wao kuibuka mshindi na kunyakua kitita cha dola 200,000. Ukiingia humo mjengoni huruhusiwi kuwasiliana na dunia ya nje kwa namna yoyote ile. Hakuna cha simu, cha TV wala cha redio humo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 20, 2010

    Ankal natamani sasa kukuona ulivyokuwa unaoga humo ndani bwana. Ama Biggie ametubania?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 20, 2010

    Hongera Ankal kwa kuweza ku-enjoy walau kwa siku moja humo mjengoni. Tabu yangu Ankal ni hako kafulana ka bwawa la maini ulikokavaa ndani ya koti hakabanduki toka ulipoenda Bondeni! Hivi Ankal ungevaa fulana ya Mlima Kilimanjaro si ungetusaidia kukuza utalii wa Bongo!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 20, 2010

    wewe mdau wa Tue Jul 20, 06:45:00 AM unaetaka uncle avae fulana ya kuutangaza mlima kilimanjaro uhali gani?

    uncle anavaa jezi hiyo kwa hiyari yake na kwa upendo wa timu yake. Ikiwa tanzania inamtaka yeye au yeyote awatangazie kilimanjaro au lolote lile basi na mumlipe.

    umeona wapi watu watumiwa kutangaza kwa bure? Michu ni mtu maarufu na tanzania kama wanataka kuutumia umaarufu wake basi ni lazima wampe malipo!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 20, 2010

    daah kweli unajua ankal kuvaa hujui jitahidi kupata ushauri kwa watu huoni tofauti na wenzako

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 20, 2010

    ni kweli badala ya kuvaa mt.kilimanjaro,ruaha national park nk
    eti bwawa la maini?ovyooooooo

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 20, 2010

    mnajuaje labda standard charted bank wamemlipa

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 20, 2010

    Tatiana kujishebedua kwingi mpaka aibu kutizama.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 20, 2010

    Ninasoma na waangola kujishebedua ndo kazi yao! .Hata mkiwa wote sehem hua wanataka kuonekana kama wao ndo wao kama huyohuyo Tatiana. m2 mzima ovyoooooooooooo..hata mie kanichefua!!!!!!!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 21, 2010

    Re: "Tatiana kujishebedua kwingi mpaka aibu kutizama".

    Hajajishebedua, she was just being friendly. Wanawake wa nchi tofauti wana act tofauti. Huoni kuwa yeye ndio alichangamsha nyumba? Zaidi ya Tatiana na huyo mwingine, ni kama kulikuwa na wasichana wawili tu.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 21, 2010

    Wewe Mdau wa July,20,3:32 utambue na uelewe si kila kitu kizuri unachoifanyia nchi yako ni lazima wewe mwenyewe mhusika upate basi hiyo faida. Ingalikuwa kama ni hivyo usingeikuta Tanzania hii ya leo. Inabidi kila tunapopata forum ya kuonekana kimataifa na hasa ukiwa Public Figure kama Michuzi uwarejeshee angalau kidogo watanzania kwa huo umaarufu waliokupatia.Unamwona Mwisho Mwampamba alivyotinga na mambo ya kimasai hayo ndiyo mambo yanatakiwa.Angetaka angeweza kupiga uzi wa Arsenal au Man Utd lakini inamsaidia nani? Kuna wakati wake wa kuvaa hivyo vitu! Lakini siyo katika Forum ambayo macho ya Afrika au Dunia yote yanakodolea BBA.Tubadilike Watanzania! Pale BBA mjengoni siyo barabarani au mtaani jamani wala siyo kwenye Bar.Angalau Ankal ungefanya promo ya Blog yako kwa kuvaa zile Tshirts zenye jina la Blog yako.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 21, 2010

    Ankal hongera lakini punguza show off wewe mtu mzima sasa mambo mengine yapaswa uwaachie wanao. huoni aibu kupigana mieleka na wanao kila uendako.loh

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...