Bwana Michuzi
Tafadhali nirushie hii pamoja na picha yake
Kama Mdau nakuleteeni salamu nyingi kutoka hapa Buenos Aires, Argentina. Ni siku ya sita hivi nashiriki katika kongamano la World Federation of Hemophilia (WFH). Imechukua takribani masaa 18 na 20,000 Km kufika hapa kupitia Doha - Quarter na Sao Paulo Brasil.
Pamekuwepo na maonyesho na presentation nyingi za kitaalamu au kisayansi. Tanzania ni miongoni mwa nchi 115 zinazoshiriki.
Tarehe 15 Tanzania itajiunga na shirika la WFH rasmi na kuwa mwanachama kamili. Nitawaletea taarifa kamili baadae. As you may know hemophilia is a blood clotting disorder which afffect mainly boys. The rare case or haemophilia B affect women as well.
Hapa Argentina hali ya hewa ni baridi na mji wao ni mzuri , well planned with majority of people speaking spanish. Utamaduni wao ni kama uonavyo kwenye picha. Kila kona kuna viwanja utiriri vya football na picha za wachezaji wao maarufu .

Beside being away from Bongo it has been a pleasure to learn about political development especially the choice of Mgombea mwenza. Nimefika hapa kwa karata ya chama chetu cha Hemophia Society of Tanzania, kina ofisi DSM hapo Muhimbili.

Wenu Richard Thadei
President of Haemophialia Society of Tanzania

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 13, 2010

    Kaka, chagua lugha moja, aidha Kiingreza au Kiswahili. Unatuchanganya sisi wamatumbwi. Pili, tukitaka kujua Argentina, tunatumia Google siku hizi, hata kwa Kiswahili.

    Safari njema na msalimie sana Maradona na mpe pole yetu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 13, 2010

    Mdau, tumia bora Kiswahili ili wadau wakuelewe vizuri.

    Siku hizi tuna internet, kwa hivyo tukitaka kujua Argentina wanakula nini au wanaongea lugha gani, huwa raisi sana kujua, hata picha za mitaa yao tunaona laivu katika Google Map.

    Hasta Luego.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 13, 2010

    Acheni kumkandia Thadei, wekeni post zenu na nyinyi basi. Ukware tu au ndo kazi za boksi zinawachengua?

    Mbweha

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 13, 2010

    jamani,huu ni ushamba sasa akhaaaaaa
    kero, kero,kero,kero,kero

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 13, 2010

    Hatuweki post zetu kwa kuwa ni ushamba...kama alivyosema mdau hapo juu.

    Pia, kazi za boksi hapa ni poa tu. Pia tuna umeme wa kutosha, maji safi ya bomba, madaktari wa kumwaga, barabara sita kwa mstari mmoja, amani na elimu bora. Na likizo yangu ya mwezi wa nane naenda Uingereza kupitia Ufaransa na Hispania (bila ya kuomba omba viza). Lakini hutaona picha zetu hapa... limbukeni ni limbukeni tu. Jinyon'ge sasa huku unakula vumbi la kamba.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 13, 2010

    mmeniwacha hoi wadau mnavojibizana hapa...
    kweli mu wajuaji/wajuzi wa mambo mengi

    hahahahahHAHAHAHA

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 13, 2010

    Mdau wa Tue Jul 13, 12:23:00 PM, waambie hao waliokosa visa. Wanakuwa na dharau za kipuuzi wakati hawana lolote. Wakikosa visa wanabakia kununua degree tu.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 13, 2010

    Hii dunia huru, mwacheni Thadei ajilie raha! haogeshi vibibi kama nyie mliojilipua.


    Hahhha!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 13, 2010

    THADEI ULIVYOANDIKA NI KWAMBA KAMA UMEHALALISHA KUWA WATANZANIA WOTE NI MBUMBU HAWAJAWAHIKUSIKIA JUU YA ARGENTINA, KWA TAARIFA YAKO KARIBU NCI ZOTE ZA AMERIKA YA KUSINI LUGHA ZAO ZA TAAFA NI SPANISH UKIONDOWA BRAZIL TU INAYOONGEA KIRENO HAYO YOTE ULIYOYAELEZA NI MAMBO WATANZANIA WENGI WANAYAJUWA

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 13, 2010

    THADEI ULIVYOANDIKA NI KWAMBA KAMA UMEHALALISHA KUWA WATANZANIA WOTE NI MBUMBU HAWAJAWAHIKUSIKIA JUU YA ARGENTINA, KWA TAARIFA YAKO KARIBU NCI ZOTE ZA AMERIKA YA KUSINI LUGHA ZAO ZA TAAFA NI SPANISH UKIONDOWA BRAZIL TU INAYOONGEA KIRENO HAYO YOTE ULIYOYAELEZA NI MAMBO WATANZANIA WENGI WANAYAJUWA

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 13, 2010

    Bora kuogesha vibibi lakini unalipwa hela halali. Nyie mpaka mkaibe hela ya umma au kupokea mlungula na mizinga mingi ya kutaka kusaidiwa. Baada ya mkutano huo, anarejea bongo kula vumbi na kuhadithia kijiweni, "Nilivyokuwa Argentina, niliona barabara pana na umeme masaa 24 kwa siku..." Waogesha vibibi wanaona ni kitu cha kawaida tu.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 13, 2010

    Jamani acheni kuua kama hamtaki kujua kuhusu Argentina si msisome... Maisha kokote ila mimi nalifagilia boksi kuliko kula hela za mradi wa vyandarua. Ndugu mdau Doha ni Qatar au kuna Doha nyingine ya robo? eeh, haya, tuwakilishe vyema lakini na asante kwa kutupa habari usiwamind wasiopenda maendeleo...
    Mdau, Boston, U.S.

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 13, 2010

    Wabongo kweli sisi tunasikitisha katika katika dunia hii ya kisomi,nimesoma comments zote hakuna hata moja iliyokuwa interested na haemofilia,hivi ni kuwa hatuelewi umuhimu wake au mabishano ya Argentine ni bora zaidi kuliko huo ugonjwa?
    Anyway,bro thadei nimekuwa impressed na juhudi ya organization yenu,mungetengeneza website yenu ili izidi kuintegrate na international society zingine.

    mdau wa istanbul

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 14, 2010

    Teh tehehe wacha mimi nicheke tu manake malumbano mengine yameenda kombo kuliko madhumuni ya habari yenyewe...Yaani kuna comments zimepinda mgongo humu sio mchezo.....

    Najua unaenjoy huko sana tu nilishafika huo mji kitambo kidogo lakini nilifurahishwa na majumba yake ya zamani lakini ni marefu na yamepangiliwa vizuri sana utazania yamejengwa juzi kumbe miaka zaidi ya 100....I love that city mtu asikwambie kitu kama umeshatembelea miji mingi ulimwengu nadhani aliyefika huu mji atakuambia the same thing..

    Well hebu tueleze zaidi kuhusu huo ugonjwa....achana na comments za watu wengine....Najua madhumuni yako ilikua kuweka awareness ya hii ugonjwa...

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 14, 2010

    Kweli watanzania hawana dira. Hoja ya msingiu ipo bayana, hakuna anayeichangia au kuizungumzia. Badala yake wadau wanazungumzia mambo mepesi. Ndo maana mnaibiwa na EPA na kungamua wenyewe wamekwisha yeya au kufa. Poleni Wabongo. Nawashauri mpeleke watoto shuleni muachane na viboksi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...