Hi mwana libeneke pole na majukumu ya kutuandalia miseto mbali mbali mimi ninaombi moja uiwafikishie wadau kwa sisi wa kazi wa mbagala chalambe na majimatitu. Sisi tunapata shida sana na ndugu zetu TANESCO wamekuwa wakitusumbua sana kwa kutukatia umeme mara kwa mara kila ifikapo saa 1:00 asubuhi mpaka saa 12:00 kamili za jioni na kukata tena saa mbili mpaka saa 4:00 usiku au unaweza usirudi kabisa
Sasa kiukweli wamekuwa wakituongezea gharama kwa kushindwa kuhifadhi vitu kwenye majokofu kwani mara nyingi hupata hasara na hufanya hivyo bila hata kutoa taarifa hii inakera sana sasa kwa mujibu kwa wa kutaka kupata manufaa na kuongeza pato la serikali tutafika kweli hii haina tija kabisa wako mdau katika kufanikisha maendeleo ya taifa letu.
Mdau Mbagala Charambe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 01, 2010

    Tumia kura yako vizuri uchaguzi huu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 01, 2010

    FUATA HAYA MAMBO MATATU (3)
    1 - ACHANA NA UMEME WA TANESCO
    2- KAKATE NYAYA ZOTE ZA TANESCO NA MUWARUDISHIE MAANA HAZINA FAIDA KWENU ( sana sana zitawaletea hasara ya kuunguliwa na vitu mkapata maumivu zaidi)
    3- MCHANGISHINE MKANUNUE SOLAR NDO KILICHOBAKIA MIMI NITAWAFUNGIA MTAPATA UMEME BORA BILA YA KULIPA BILI TENA KWA MIAKA 20 KWA NYUMBA 100 NA KUTUMIA PASI KASORO JIKO NA AC-[KIYOYOZI]

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 01, 2010

    Mbagala ndio mnaongoza kwa kuibeba CCM na hayo ndo malipo yake naTANESCO wanampango wa kuwaongezeni muda wa mgao kwa siku badala ya masaa 4 sasa itakuwa masaa 14 ili sisi wa osterbay tusipate shida.Hivi huko mbagala kuna nini cha muhimu?.....CCM Oyeeee..Mdau Masaki.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...