Timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 20 Ngorongoro Heroes usiku wa kuamkia leo imefungwa bao 1-0 na wenzao wa Ivory Coast kwenye Uwanja wa Felix Houphouet Boigny katika kuwania tiketi ya kucheza fainali za Afrika kwa vijana zitakazofanyika Libya mwakani. Iwapo Ngorongoro itashinda kwenye mchezo wa marudiano itakutana na mshindi kati ya Gambia na Sierra Leone ambapo itaanzia tena ugenini mwezi Septemba na kumalizia nyumbani Oktoba mwaka huu. Pichani ndilo goli lenyewe....Mdau Sammy-Kr


Sio mbaya wadogo zangu mmejitahidi, ila tufanye juhudi nyumbani tushinde maana tumebakiza hatua chache tu...Mungu Ibariki Tanzania.
ReplyDeletegud n bravo wana,najua tz hawatoki hao,mkirud mkaze makalio kwa tz mwanzo mwisho,home tunawanyuka hao,goli noja co ktu na inaonekana hawakutushika maskio hao,poa tz mbele tu mpaka mwisho!!!
ReplyDeleteSio mbaya madogo...bravo. Huo ni ushindi mwembamba sana kwao ukizingatia walikuwa nyumbani. Kwetu sisi bao moja ugenini linaweza kutubeba endapo hatutabweteka na hayo matokeo. Muhimu tukaze buti kweli...waalimu naamini wameona wapi tulikosea na watarekebisha ili huku tuwapige 3-0. TFF fanyeni kila liwezekananlo maandalizi yawe mazuri...wakati ni huu, tuutumie ili tusije juta baada ya mechi. Najiona nikishangilia timu yetu ikiwa Libya hapo mwakani kwenye mashindano....Tanzania kuwa kama Spain INAWEZEKANA
ReplyDeletehawa madogo they can take us very far ni wazuri kinoma kufungwa goli moja tu na ivorycoast sio lelemama hata kidogo.BIG UP ngorongoro haina noma kazeni msuli
ReplyDeleteNa twiga star wamekongoliwa 6-0 south. Yaan soka la bongo raha kweli kweli!!!
ReplyDeleteAnyway, kazeni buti madogo!
hivi timu ya twiga stars wameshinda ngapi naomba mnipe matokeo maana ile ndo timu tunayoitegemea
ReplyDelete