washiriki wa mchezo wa Pool table wakishindana katika mashindano ya speed pool yanayoendelea kufanyika mkoani Arusha.

Na Woinde Shizza,Arusha

Ikiwa mashindano yajulikanayo kama Safari Pool national champion ship yanatarajiwa kuanza kutimiua vumbi hivi karibuni na fainali zake zinatarajiwa kufanyika mkoani Arusha kampuni ya bia ya TBL imeanza maandalizi kwa ajili ya mashindano hayo

Kampuni hii imeanza kutoa hamasa katika sehemu mbalimbali za mjini hapa ikiwemo katika bar ambazo zina washiriki wengi ambao wanapenda mchezo huu.

Kwa mujibu wa taarifa ya mmoja wa wahamasishaji wa mashindano hayo alipoojiwa na blog ya jamii kuhusiana na hamasa hiyo alisema kuwa wameanza kutoa hamasa kwa kufanya promosheni kido kidogo ya kuwataharifu wakazi w amkoa huu kuwa mashindano haya yanafanyika mkoani hapa.

Alisema kuwa kuna baadhi ya zawadi ambazo wanazitoa kwa ajili ya kuhamasisha watu na pia alibainisha kuwa pamoja na kuwahamasisha watu pia wameandaa mashindano.

Alisema kuwa mashindano wanayafanya kwa sasa ni yanajulikana kama speed pool ambayo yanachezwa kwa kutega sekunde na mshindi anayepatika anagaiwa zawadi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 20, 2010

    Hiyo ship ya Champion inaingia lini bandarini? duuh leo mnenichekesha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...