
Chama cha wanafunzi wa vyuo vikuu wanaotoka wilaya ya Rorya wamejipanga kufanya mdahalo tarehe 18 mwezi huu kwa watangaza nia wa jimbo la Rorya
Mdahalo huo utakuwa juu ya kueleza mikakati ya watangaza nia wa Rorya kwa jinsi watakavyotekeleza masuala ya maendeleo pindi watakapopata nafasi.
Masuala hayo yatakuwa katika maeneo ya Elimu, Afya na Ustawi wa jamii, Kilimo na ufugaji, Maji, Miundombinu, Uchumi, Utawala Bora, Michezo na jinsi ya kuhimiza uwekezaji wilayani.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanafunzi wa Vyuo Vikuu wanaotoka Wilaya ya Rorya, Martin Owour alisema kuwa lengo lao ni kuona kuwa wilaya hiyo inasonga mbele.
“Tunataka kuona wilaya yetu inasonga mbele katika masuala mazima ya kimaendeleo,” alisema.
Aliongeza pia wanafunzi wamejipanga kufanya shughuli mbalimbali za jamii kama kuelimisha juu ya masuala ya maendeleo.
“Uelimishaji huu unalenga kuwaelekeza wanajamii kujua masuala` ambayo wangetaka wanaogombea wayatekeleze,” alisema.
joni mashaka upo??????????????
ReplyDeleteSasa mbona hii inachekesha...."Wakiongea na waandishi wa habari ambao hawapo kwenye Ukumbi"...sasa hao waandishi wa habari wako wapi? Au ulimaanisha akiongea na waandishi wa habari ambao hawapo? Au wakiongea na waandishi wa habari ambao hawapo pichani? Mbona ninyi watu mnatuchanganya lugha?
ReplyDelete