GLOBU YA JAMII IKISHIRIKIANA NA MICHUZIPOST.COM IMEHAHA USIKU KUCHA KUSAKA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGU WALIOPITISHWA NA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CHAMA HICHO USIKU WA KUAMKIA LEO HUKO DODOMA. HADI SASA NI MAJINA YA WAGOMBEA WA MIKOA 13 IMESHAPATIKANA KWA KIANZIO. MAJINA MENGINE YANAFUATA PUNDE
Home
Unlabelled
MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE WA CCM 2010
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Dah!CCM wanammwaga Siraju Kaboyonga wanampa mtoto wa Saigon Aden Rage...kumbukeni kwa hila zenu na uwoga wenu wa kufanya kazi na watu mahili ndio utawaangusha,."bila CCM madhubuti nchi yetu itayumba"
ReplyDeleteUamuzi wa kumrudisha Ole Sendeka Simanjiro ni wa busara na mzuri
ReplyDeleteKwa Iringa Mjini CCM wamechemka, nakubaliana na Anonymous hapo juu kuwa Mama M Mbega kwa sasa hauziki(hana jipya), inambidi huyu mama asome alama za nyakati, na ninavyowajua wanyalukolo kumpa mpinzani ni jambo la kawaida kwao, ushaidi ni pale jimbo lilipokuwa chini ya NCCR mageuzi chini ya mbunge Kibaasa na chanzo kilikuwa kuwapa mtu wasiyemtaka, kitu kingine ambacho wanyalukolo hawakitaki ni hawa wabunge kupewa majukumu mengine na kusahau majukumu waliyonayo katika majimbo yao. Hapo CCM wana kazi ya kumnadi huyu mama
ReplyDeleteUmehaha kutafuta usiku kucha? Mbona list yote kamili imewekwa kwenye website yetu ya CCM? Sie wanachama hai tumekwishaiona zamani huko kwenye mtandao wetu, kuanzia viti maalum mpaka hao wakugombea majimboni wewe google ccm website utatupata.
ReplyDeleteKwa mtu ambaye ni mgeni na mkoa wa Iringa ni kuwa Mhehe hapendi dharau,KK CCM ilichokifanya ni dharau hivyo wajiandae kulipoteza jimbo la Iringa Mjini kama ilivyokuwa mwaka ule Mh. Mfaramagoha alivyoshinda na kuwa mbunge kupitia chama cha upinzani, hivi huwa hawaangalii historia! Kazi kwenu viongozi kumnadi huyu mama asiyenadika kwa sasa(hana jipya), Iringa mjini inahitaji mtu mwingine. Angalia ni mkoa gani ambao ktk kura za maoni zilizopita uliwabwaga wabunge wao wa zamani kama sio mkoa wa Iringa,CHADEMA jimbo hilo linawangojea.
ReplyDeleteIt is time now for we Tanzania to wake up and and understand what kind of political party CCM is, how dare they accept nomination of candidates who have been named and shamed as "mafisadi" with criminal proceeding still going on. As far as I know a so called "kamati ya madili ya CCM" has been going through candidates names are you telling they could not find anything wrong with all these hard core criminals ?, I am giving up with this country if my fellow Tanzania are you going to vote for these candidate again
ReplyDeletevijisenti na pesambili kazi ipo.
ReplyDeletekazi ipo kinondoni huyo idd azan hauziki hata kidogo hakuna cha maana amefanya jimboni haya tusubirie
ReplyDeletehongera kikwete unastahili sifa kwani sasa umeifahamu vizuri ccm tofauti na mwanzo ccm ina wenyewe na ndio hao kura za maoni ni zuga tu kwa wana ccm wajihisi kuwa nao wapo ila ccm ni NEC
ReplyDeletemichuzi nasikia mbunge wa chadema tarime kahamia cuf,kazi kweli kweli.tuletee hizo habari,sio unachagua habari hapa
ReplyDeleteMichuzi tunaomba angalao utudokezee hatma ya Globu ya Jamii baada ya kuanzishwa michuzipost.com. I am a bit confused.
ReplyDeleteRombo: Basil Pesambili Mramba, huy si ana kesi ya kuhujumu serikali mamilioni ya hela?
ReplyDeleteMonica Mbega aliyekuwa ameangushwa katika kura ya maoni na Frederick Mwakalebela katika jimbo la Iringa Mjini, ameibuka kidedea akimzidi kete Katibu huyo wa zamani wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambaye kuenguliwa kwake kunahusishwa na kashfa ya rushwa inayomkabili.
Sasa mtu mwenye tuhuma za kashfa (bado hajafikishwa mahakamani) na mwenye kesi (ipo mahakamani) yupo wa kumwengua kweli? Hapa naona chama changu cha CCM kinajichanganya
Ni ukweli ulio wazi kuwa CCM imejiua yenyewe na inajimix yenyewe, yaani pamoja na kupiga vita juu ya mafisadi na hadi kuwapeleka mahakamani bado inawarudisha wale wale kuendelea kuzichota pesa zetu tunazozihangaikia mashambani, sasa lengo la kumrudisha mtu ambaye kesi yake iko mahakamani maana yake ni nni? sasa akishindwa case yake na wakati tayari ni mbunge hamuoni kuwa mnapoteza pesa tena za kuitish uchaguzi mpya?? maana akishindwa case inambidi akanyee Segerea na apoteze ubunge wake, au ndio kutoonesha namna CCM mlivyo wababe ya kuwa hata sheria mmezishika nyie mkononi?? yaaani hamna adabu kabisa, mtatudharau sisi watanzania wachini tusio na kipato kwa kukumbatia hao mafisadi .ni aibu pia kwa nchi yetu kuongozwa na maboya., hivi wwe Kikwete na uongozi wako hamnaga washauriiiiiiiii????????????????????? hivi mbona mnafanya mambo kama hamkwenda shuleeeeeeeeeeee,jamani watanzania kwa dharau hizi mie ninaona sasa tuwaaibishe na nchi tuwape wengine wenye uchungu na taifa letu, lol inasikitisha sana, huu ni utumwa na manyanyaso ndani ya nchi yetu, nyie acheni ije siku tushike hatamu ,nyooooooooote kuanzia wwe kikwete ni kwenda Segerea tuu maana mnaudhi sasa, na wwe mithupu usiibanie hii iweke tuu wote wasome
ReplyDeleteMtu yoyote kabla hajaukumiwa hana kosa na anahaki zote.
ReplyDeletewatu wanasema mzee mbega ana undugu na makamba ndio maana mama mbega anabebwa, namna hii tutakuwa hatuendi kabisa
ReplyDeleteanony wa 08.25 ccm siyo NEC bwana ila mwenye chama hiki ni mzee makamba (mzee wa kupayuka)kwani hata wao wajumbe wa NEC kuna wengine waligombea na pia wametoswa lakini hakuna hata mmoja aliyejaribu kutetea mwenzake...
ReplyDeleteMzee makamba amehongwa pesa nyingi sana kutetea wale wote walioshika nafasi ya kwanza ili mradi mtoto wake january nae asalimike
january pia alikuwa na changamoto kubwa ya kushinda bumbuli na baba yake alihalalisha kila mtu mwenye kadi akapige kura hata asipokuwa na kitambulisho cha kupigia kura...
cha kushekesha zaidi hata jk amemlinda kwa hili...
siasa bwana....
HAYAAAA SWAGAAAAA CCM CCM CCM HAHAHA JUUU SANA SASA NAULIZA WAPI BAROZI WA JAMIII KULEEEE KINONDONI MBONA SIJAMUONA AMA VITI MAAARUMUUUU AMA NDO MAMBO YA BIZEEEE.........CCM CCM CCM HOYEEEEEEEEEE
ReplyDeleteuchunguzi wa kina unahitajika kuangalia elimu ya wagombea wote waliopitishwa maana nimeona kwenye website ya ccm eti wengine wamesema wana elimu ya kidato cha nne wakati hawakufikia hata kidato cha 3 ..heri ya wale waliosema ukweli kwamba wana elimu ya msingi
ReplyDelete