JUKWAA LA SANAA: MKOMBOZI WA WASANII NA KISIMA CHA MIJADALA YA KISANAA.

Kila Jumatatu kuanzia Saa 4 Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) limekuwa likiendesha Jukwaa la Sanaa ambapo wasanii na wadau wa sanaa wamekuwa wakipata fursa ya kujadili masuala mbalimbali yahusuyo kazi zao.
Aidha, katika Jukwaa masuala mbalimbali yamekuwa yakiibuliwa na kupata majibu na suluhu.Wasanii na wadau wa Sanaa wachangamkie fursa hii ambapo imekuwa ikiwaleta wadau mbalimbali wa sanaa nchini kwenye meza moja.Wiki hii (Jana Jumatatu) mada ilikuwa Mwelekeo wa Tunzi za Muziki Tanzania na Changamoto zake.

Wadau wanakaribishwa kwenye Jukwaa Jumatatu ijayo ya Tarehe 16.8.2010 ambapo mada itakuwa Mchango wa Vyombo vya Habari Katika Kulina Maadili Ya Mtanzania itakayowasilishwa na Mtaalam Kutoka Mamlaka ya Mawasililano Tanzania (TCRA).

Mkongwe katika sanaa za Ufundi,Mzee Nkwama Bhalange hakuwa nyuma katika kuchangia mada kuhusu Changamoto za Tunzo za Muziki.

Wadau wa Jukwaa la Sanaa wakimsikiliza kwa makini,Meneja wa Bia ya Kilimanjaro,George Kavishe wakati akiwasilisha mada kuhusu Changamoto Katika Tunzo za Muziki Tanzania Meneja wa Kilimanjaro lager ambao ndiyo wadhamini wakuu wa Tunzo za Muziki Tanzania, George Kavishe (Kushoto) akisisitiza jambo wakati akiwasilisha mada yake Jana Jumatatu. Kushoto kwake ni Katibu Mtendaji wa BASATA Bw.Ghonche Materego na Katibu wa CAJAtz,Michael Bumbuli. Mkongwe wa miondoko ya Reggae, Ras Inocent Nganywagwa, akichangia mada kwenye Jukwaa la Sanaa. Picha na habari na Afisa Habari wa BASATA,Alistide Kwizela



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...