
Vifaa hivyo vilikabidhiwa na Bwana Nassoro A. Uzigu, Meneja wa Benki hiyo Tawi la Zanzibar kwa Profesa Ali Seif A. Mshimba, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar.
Shughuli hiyo ilifanyika katika Chumba cha Mikutano cha Taasisi ya Kiswahili na Lugha za Kigeni ya Chuo Kikuu hicho.
Vifaa hivyo vinategemewa kutumika katika shughuli mbali mbali za kimichezo za Chuo yakiwemo mashindano ya Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki yanayotegemewa kufanyika baadae mwezi Disemba, 2010 huko Kenyatta University, Nairobi – Kenya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...