Maelfu ya wananchi wa Mdida, Singida Vijijini wakiwa wamelizunguka gari la JK alipofanya mkutano wa kampeni kwenye eneo hilo
Wafuasi wa CCM, wakiimba na kucheza wakati wakimsubiri JK ambaye alipita kijijini hapo kwa mkutano wa kampeni na kusikiliza kero za wananchi hao leo.
Mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Singida Mjini ,Mohamed Dewji akielezea mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwenye Jimbo la Singida Mjini kabla ya hotuba ya JK leo.

JK akihutubia umati mkubwa wa watu kwenye mkutano wa Kampeni Singida Mjini leo
Umati wa watu uliojitokeza kumsikiliza mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alipohutubia mkutano wa kampeni kwenye uwanja wa michezo wa Namfua Mjini Singida leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Kwa kweli naona JK hana mchezo kama amefika hata Mdida. Huko ni kijiji sana. Maeneo hayo walikuwa wakiishi watu wa kabila la Barabaigi na wengi wao wamehamia Arusha na Morogoro. Mdida ni sehemu moja amabayo inategemewa na Mkoa wa Singida kwa kutoa mazao ya Mahindi na Alizeti. Na kuna semekana kuna dhahabu pia.

    ReplyDelete
  2. Michuzi hii blog yako inatema CCM tuu. Hebu jaribu kuwa fair, toa na picha za chadema, CUF na wengine wanavyoteka miji. upendeleo kwa CCM utapoteza umaarufu na maana nzima ya blog yako.

    ReplyDelete
  3. Kama alivyosema mtoa maoni wa pili hapa,Inaonekana kama vyama vingine bado havijaanza kampeni maana kila ukifungua blog hii ni ccm tupu,jamani tuache upendeleo na tutoe habari za kampeni za vyama vyote ili tuweze kuona kwa uzuri jinsi kampeni inavyokwenda,haipendezi kuona kila siku shughuli za ccm tu,inaonekana kama blog hii ni ya chama kimoja au inamilikiwa na ccm,
    mdau,Morogoro

    ReplyDelete
  4. fungua blog yako ya chadema tuachie sisi na michuzi tujidai na CCM yetu okey....

    ReplyDelete
  5. "fungua blog yako ya chadema tuachie sisi na michuzi tujidai na CCM yetu okey...."

    MTU MZIMA HOVYOOOOOOO

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...