MAMBO YENYEWE KAMA NI HIVI UKIMWI UTAKWISHA KWELI???
IT WAS SHOCHK FOR ME!!!

Mimi ni mdada wa miaka 36 na sijaolewa lakini nina watoto wa kike wawili ambao kwa uwezi wake Rabuka ningeependa niwalee katika maadali mema, na pia kwa sbb bado niko kijana ningependa siku moja na mimi nipate mwenza wangu wa kuishi naye.
Miezi kama miwili iliyopita nilipata kazi katika ofisi moja hapa jijini ni project about 5 yrs, Wakati naanza kazi pale ofisini kuna kaka mmoja na yeye ndio anamalizia notice yake ya kuacha kazi, Kijana huyu ni msomi wa hali juu sana, basi ofisi iliamua tumfanyie a very small party ya kumuaga, nia tulifanya hivyo, basi ghafla yule kaka akawa ananipigia simu na kunisalimia mimi nikawa nashangaa sana kwa sbb sikumzoea kabisa kwani nilikaaa naye muda mfupi kabisa, ghafla akapata skype yangu nahisi kutoka kwa mtu pale ofisini mbaye ni mshikaji wake, basi tukawe tunachat unajua tena vijimaswali vingi na mimi nampa majibu yote anayoyataka.
Sasa Ijumaa ya tarehe 08-10-2010 akaniambia mimi nimpe offer lakini nikamwambia haitawezekana kwa leo, basi akapropose kuwa yeye anataka kuongea na mimi kwa kirefu na ingekuwa vinzuri tuonane jumamosi, nikamwambia nitakujibu hiyo jumamosi, basi asubuhi jumamosi akanipigia simu 3:30 na kuniambia kuwa anaelekea kwenye hotel mmoja hapa jijini kuna kazi anafanya pale kama ninaweza niende hiyo saa 05:00 mmh! nikashangaa sana, lakini niliwambia haiwezekani mpaka jioni kwenye mida ya saa 12 nitamfahamisha kabla ya hapo.
Lakini nikamwambia kwani ni maongeze gani hayo mbona hunaonekana huna haraka sana????? ebu nipe hints ili nijue nakuja kuongea nini? alishindwa kabisa kunipa jibu ya hili swali, basi jioni baada ya kunismumbua sana nikasema ngoja nikamsilikilize kwani mm ni mwanamke mkubwa chochote ni uamuzi wangu mimi.
Nilipofika pale Hotelini nikampigia simu ya kumfahamisha kuwa niko reception ni hotel kubwa lakini mazingira ya pale hayakuonyesha wapi pa kuongelea, Mara ananijibu panda juu chumba no 505 mmh! nilimjibu kuwa mimi nimekuja kuongea na siyo kuongelea chumbani, na nikamwambia kuwa naondoka akanijubu sawa, nilikuwa na maswali mengi ya kujiuliza nafsi yangu huyu kaka hajui kutongoza?? au ndio siku nzima anakodisha chumba kutuingiza kwa zamu??? au mimi ndio mshamba, na ukumbuke huyu kaka amesoma eti ndio ametoa ujinga - JAMANI NIPE USHAURI WENU, NATAKA KUSIKIA MAONI YENU
Mdau wa HapaHapa Dar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 47 mpaka sasa

  1. Mhh wewe dada iyo kali sanaa,huyo jamaa ninashindwa kumuelewa,kwa nini kama alikuwa na nia nzuri tu ya kuongea na wewe ata tukisema kama alitaka kukutongoza kwa nini asichague sehemu nzuri tu amabayo isingekupa wewe wasiwasi,may be alitaka uende huko aingize voko ukimchomolea basi akumalize hukohuko kwa nguvu,hata kama udomo zege zat is too much,ila ungempa nafasi ya kujieleza zen ungemsikia anataka nini,

    ReplyDelete
  2. Nafikili wewe ulishamuelewa nini anataka,najua ww ni mtu mzima ,may be alikuwa na kigugumizi cha kukuambia si unajua kutongoza nako ni sanaa,je baada ya kumwambia naondoka alikupigia tena,je anaendelea kuwasiliana na wewe kama mwanzo? hapo hotelin je hapakuwa na sehemu ya wazi ambapo mngekaa na kuogea vizuri tu? Pia kumbuka elimu yake na mwaswala ya muhusiano ni vitu 2tofauti huo ni uwanja mwingine,ningependa sana tungewasiliana ili nikupe more information ,am a sexiologiste by professional na nina dili na maswala ya ushauri wa mahusianao in general ,zat is ma mail danielmtanda@yahoo.com

    ReplyDelete
  3. michuzi na wewe unapost hizi non sense????

    ReplyDelete
  4. wanaume wengine bwana ovyo kweli,sasa dada anakuja na ni yeye ndio aliyemuomba watoke sasa mtu anakuja bado analenda mapozi, au ndio udomo zege!!, naona jamaa alikuwa hajiamini

    ReplyDelete
  5. dada, labda nikuambie tu wewe ni mkubwa sana kusoma alama za nyakati sijui ni majibu gani uliyokua unamjibu mwanzo mpaka akaona haitoshi au akashindwa kukuelewa na kukodi chumba! just be a straight forward person thats about it! ala!

    ReplyDelete
  6. dada yangu wanawaume siku zote usiwape chance, we ignore them tu kuanzia mwanzo. hii ndiyo sheria usiongee na mwanaume kwenye simu zaidi ya dakika kama ukiona hana la maana au kumaliza yote haya mwambie huko chini pameoza utaona kama atakusumbua. mimi shangazi yangu aliniambia hivyo na pia libaba likinifuata naliita jizi..... mijanaume mijehu sanaaaaaaaaa hii. ndio maana nimefika chuo mpaka napata na Phd yangu. michu upooooooo halafu michu mwenyewe hana mke labda ndio zake hizi ha haha ha

    ReplyDelete
  7. Ulifanya cha maana kuondoka huju mwanamee ni mshenzi, alifikiria utampaaptikia! Angekuwa na heshima na wewe asinge panga makaongelee Hotelini!! Achana naye utakutana na mtu mwenye kukuheshimu. akizidi kukupigia simu badilisha number au mtolee uvuvu asikusumbuwe!! you know what you deserve better!!!

    ReplyDelete
  8. Mhh huyo jamaa vipi,yani alishindwa kushuka chini ili kuliimbisha ilo zigo,maana zigo lilijileta inabidi angeshuka zen zigo lingepanda tu,yani jamaa bwege alingoja hadi zigo lipande juu haaaa,domo zege sana huyo!
    Achana nae huyo!

    ReplyDelete
  9. Mapenzi hayana cha usomi dada,inategemea wewe tu usanii wako maana mapenzi ni kama sanaa sasa!naona mdau ju hapo amejaribu kuuliza maswali ya msingi ebu mjibu zen tuone nia yake hasa baaday kutokea tukio ilo je anazidi kuwasilina na ww au ndio ame cut off mawasialiano

    ReplyDelete
  10. kwanza kabisa hata wewe dada yangu umekosea, kwanza watu hawakutani hotel, kuna sehemu kama za lunch au naweza kutoka kwa matembezi tu mkaongea sasa kwanini ukubali kwenda hoteli? ila ulifanya vizuei sana huyo jamaa ni limbukeni na inawezekana kabisa akawa mgonjwa na ndio alikuwa anataka kukuambukiza je unajuwa sababu ya yeye kuacha kazi hapo? outpac3@yahoo.co.uk

    ReplyDelete
  11. inategemea pia maongezi mliokuwa manongea nae ,nahisi ndio maana akapata mbichwa wa kuchukua chumba aim eti kwenda kuua mhh bila makubaliano,alibuki huyo,pia kama kweli alikwa anataka kukutongoza na kuishi na ww ina maana anakueshimu sasa iweje akupeleke huko kote,inamaana hapo eshima ni F, tubadilike bwna,

    ReplyDelete
  12. Dah! hongera sana Dada yangu kwa kuukwepa huo mtego, na pole kwa ma-swahibu yaliyokupata.
    Huyo kaka ni mzinzi tu hana lolote, ameshazoea machangudoa so alijisahau akijua na wewe ni hivyo.
    Na kama inawezekana mwendee hewani umchambe kabisa akome.
    Usiwe na harada tulia Mwombe Mungu atakupa mwenza mwema sio hao wanaoringia elimu wakijua ndio kila kitu.(Eliza)

    ReplyDelete
  13. aluu!! Dada una watoto wawili. hivi ulitaka utongozwe vipi zaidi ya kukuambia njoo room namba fulani.

    hadi Msomi kafikia kufanya hivyo kashasikia wewe ni cheaaaap

    ReplyDelete
  14. Sasa wewe unataka kuwalea watoto wako kwa maadili mema wakati mwenyewe uliwapata nje ya ndoa? Watoto wanaishi kwa Modeling...sasa wewe unatoa mfano gani wakati hawaishi na baba zao? Mtoto wa Nyoka chance kubwa atakuwa nyoka na yeye...!!!

    ReplyDelete
  15. oh yeah, yaani mpaka kufika kuitwa hotelini na hukujuwa anachotaka? usitudanganye hapa! ulijua fika alichotaka, awe anajua au hajui kutongoza, angalau aliweza kukulainisha mpaka ukaamua kwenda hapo hotelini. Kosa lake hakushuka chini tu kuja kukuchukua, lakini naamini kama angelikufata hapo reception jamaa angelipata mchezo!

    Kama ulivyomaliza maelezo yako, naamini kilichokufanya ubadili mawazo yako ni kuwa ulihisi utakuwa peke yako, lakini ukagundua kuwa jamaa kakodi chumba siku nzima, ukahisi akikumaliza wewe kuna mwengine anafuata.

    Suali la kuwa msomi au sio msomi halihusiki hapa.

    ReplyDelete
  16. Wewe anonymous was Oct 11 07:08:00 PM kwani lazima utoe comment?

    Kwa nini unamdhalilisha mwenzako? Aliye cheaaaap ni huyo msomi aliyejipeleka chumbani kwa matarajio yasiyokuwa na mapatano.

    Hongera dada kaza buti, pengine tayari ameukwaa huyo anataka kusambaza tu!

    ReplyDelete
  17. N wewe ni changu doa tu, uliwezaje kumfuata mtu hotelini? Ulitegemea nini ukifika huko?

    Unapokosoa usomi wake, unahusikaje na mambo ya mapenzi?Hujui mapenzi ni upofu na hasa kama alikuzimia basi usijibaraguze na kumkashifu na usomi wake.

    Wewe mwenyewe umesema una watoto wawili, halafu unatuambia ukimwi utaishaje hivi?kwani hukuliona hilo ulipokuwa unawatafuta hao watoto wawili?au walipitia mdomoni?

    Wewe mtu mzima kabisa ulijua tangu mwanzo ukiongea naye kwa simu na alipokuwa akikusaka kwa udhi na uvumba ulijua alichokuwa anataka, sasa iweje umemfuata mahali panaitwa hotelini, halafu utuletee upuuzi hapa kumsuta jamaa?? Aliyekupeleka hadi hotelini nani?na ulifuata nini huko kama si usanii tu unatuzingua nao hapa?

    Hata mtoto mdogo anaweza jua nini kilikuwa ndani yako.Hata huyo anayesema anapata Ph.D.Inahusika nini na mapenzi dada?Ph.D zingine za kuchota kama maji ya bwawani tu.Unataka kutuambia Ph.D ndiyo mapenzi yako ya sasa ya kujibinafasi nayo?

    Wewe uliyeleta maada hii hapa nakuomba ufikiri mara kadhaa kabla ya kuleta upuuzi kwa watu wakati kitendo umekifanya mwenye hadi hotelini halafu unamzuzua jamaa hapa kwani alikubeba ulikotoka?

    ReplyDelete
  18. we dadangu nadhani we mwenyewe ulimzimia vile vile ,ndio usemi ule ule cheaper..uwezi kuongea namtu si mara moja au mbili kutomjua mtu anakuhitaji kwa nia gani?ebu kwanza weka suala wazi vp? ulikubali kuenda hotel na unajua hoteli ni mambo yote?kama unavosema mwenyewe we si mtoto ni mtu mzima unaelewa kila kitu ,sasa jibu unalo mwenyewe ikiwa mpaka kuonambona ana haraka hivi ?amependa ulivo na vile vile huenda kijana amekuona mzuri wakuvutia ..hebu usimwage mtama kwenye kuku wengi jifikirie kijana mwenzako anakuhitaji kivp?je hao watoto wawili uko nao baba yao yuko wapi?na yeye amekupenda ana mke na watoto..ulizaneni kiutu uzima dadangu na mwenzako kijana.mdau ulaya

    ReplyDelete
  19. Dada yetu mie naona jamaa dau lake lilikuwa dogo , je ungeingia chumbani na kutembea naye ungetueleza habari hizo ? na kama kweli ulikuwa huna nia basi ungemstopisha jamaa toka mwanzo alipokuwa anaanza kukupigia simu na kukuletea maneno ya ubazazi sababu wewe ni mkubwa tosha wa kuelewa jamaa alikuwa anataka nini.
    mdau Babu Maumba.

    ReplyDelete
  20. Je baada ya kuondoka alikupigia tena?je mnaendelea kuwasiliana kama mwanzo? KUmbuka mapenzi na elimu ni 2things tofauti sanaa;ebu tusaidie hapo kwanza na labda huyo sexiologiste hapo juu atakusaidia

    ReplyDelete
  21. Hatuwezi tukamlaumu huyo dada kwa kwenda kule,yeye si aliambiwa kuwa anaitaji kuzungumza nae,yeye aliitikia wito,hakufanya kosa,kosa ni la huyo jamaa aliye kataa kushuka chini na kumpa ujumbe wake huyo dada,
    hivyo ni vijimambo,
    by sexiologiste

    ReplyDelete
  22. Dada nashukuru sana kwa huu umbeya maanake you made my day, habari ndo hii. Saa nyingine mtu hutaki kusikia habari za uchaguzi, kifo, ajali, wizi nk.
    Kwenye suala lako uzoefu wako hapo ulicheza. Mijitu mengine ikiwa na kisomo sana au hela skills za kuongea zinapotea. Halafu mtu kama huyo ungelala naye siku ya pili wala heshima asingekuwa nayo. Kwahiyo ulijilindia heshima.
    Mpaka uliamua kufunga safari ulikuwa na nia njema ya kumpa chance lakini kwa uzuzu alioonyesha ulichukua ushauri wa maana. Na magonjwa haya miaka hii sio suala la kulala lala ovyo

    ReplyDelete
  23. Wabongo mnaonyesha mlivyofuzu kwa ngono. Kunatolewa maada za maana zitakazo athiri maisha ya sasa na vizazi jivyo lakini watu hawaongei chochote au wanaongea utumbo. Mmewekewa ngono basi kila mtu anahoja. Kazi ipo hapa.

    ReplyDelete
  24. Look, bwana ee...we unatuyeyusha hapa. Wwe ullijua tangu mwanzo jamaa alikukoma. Sasa kama hukumkoma basi tulizana. Kukuita hotelini...kabla hatuja jump into conclusion, cha kufanya ni kumwambia tu kuwa ungedhani hiyo ni inapropriate. Na kuwa awe wazi anachotaka. Kama anataka sex, and that's it...say NO or YES.As simple as that.

    Kitendo cha wewe kuweka hii story ndeefu katika blog...that's childish, and waste of space. You are no different from him, probably that's why he picked you to "TALK" to. 36 tears old?! for real!

    Come on Michuzi....really?!

    ReplyDelete
  25. Dada wewe unachekesha kweli. yaani umeona hiyo ndiyo habari ya kutupatia wasoma globu?. kama uliweza kufika mpaka reception ya hoteli hiyo kilikushinda nini kupanda room 305 na kumsikiliza.umri wako isingekuwa rahisi akubake bali mngeridhiana. Lakini unataka kutuchafulia tu wanaume wote. halafu unakuja na gia ya ukimwi utakwisha.je unamjua mwathirika kwa mialiko tu? Nilitaraji ungekuwa jasiri wa kuwaambia wenye hoteli kuwa nakwenda room 305 kwa maongezi naomba muwe na tahadhari kama nitapiga kelele ya kubakwa mje mnisaidie.na huyo kaka ungeweza kabisa kumshauri mwende mkapime afya zenu. hapo ungekuwa rafiki mwema kwake na kwa wnaume wote. lakini kwa kitendo chako hicho umekuwa adui nambari wani...pole dad wee..hatudanganyiki kwamba wewe ni mtakatifu jinsi hiyo

    ReplyDelete
  26. huyo ni mjinga tena mpumbavu asiyejua vibaya kwanza sijui niseme ni fataki kijana au nimuitaje mi sijui au m'bakaji dada yangu kwa kuwa umeshakuwa mkubwa achana nae ukiona anazidi kukusumbua peleka kwenye sheria hiyo mtu aisee amenikera kweli kweli

    ReplyDelete
  27. huyo dada aliyesema ana PHD ni mjinga sana anataka kuniambia hajabilkiliwa mpaka sasa aache uchinga maprof wangapi wanafanya mapenzi kama kawa,na mara nyingi hawo wanaojifanya wasoma ndio wanaangukia pabaya,dada ongea na mwenzako zaidi asikudanganye mtu mapenzi ni popote,jamaa naye pia mpuuzi huwezi kukutana na demu siku hiyo umchape,labda km anataka wa chap chap aende kinondon makabulini au hongera bar wapo kibao,

    ReplyDelete
  28. huyu dada anajaribu kutuambia nini hapa? anajaribu kujisafisha na nini? kwamba kutongozwa na kukataa ni jambo la ajabu? Ana uhakika gani kuwa kuingia chumbani ni kufanya mapenzi tu?! mbona anataka kuwafanya wanaume wote kuwa wabakaji? Yeye na ukubwa wote huo hakuelewa message tangu mwanzo? Au shida zake za kutafuta "mwenza wa kuishi nae" kama anavyodai ndio zilimpeleka hotelini? She is desperate nadhani! Anataka tumuone malaika kwa kuukimbia "mtego", hana umalaika wowote kwani hao watoto kawapataje na baba yao/zao hakuwashtukia mtego wao eti ndio aje kuwa mjanja sasa!! wako wapi hao baba za watoto wake?! Asitafute umalaika kupitia kwa watu wengine kwa kutaka watu wamuone "anaogopa". Hana lolote na alishachelewa na maisha yake yanajieleza wazi.

    ReplyDelete
  29. Acha hizo bibi, wewe ni mdada miaka 36 with 2 children?????? hao watoto uliwapataje nje ya ndoa? basi phd yako ni ya kusoma ila hijaelimika kama yule alikuzalisha na hajakuoa huyu ulimwogopa ni nini? sema hakufika dau angekulamba....

    ReplyDelete
  30. .....mpaka umri huo na watoto wawili unajifanya hujui umekoswa na mishale mingapi! jamaa aliku valuate akaona hiyo ni njia muafaka ya kumalizana na wewe! jamaa alifanya mistake moja tu yakuto fuata mzigo chini! Hao wengine uliozaa nao, walitumia mitego gani halafu wakasepa!!!!!!?
    Mdogo wake Ankal.

    ReplyDelete
  31. Wewe mdau unayesema huyo dada anaishi na watoto wake mwenyewe hivyo hawatakuwa na maadili mema sio kweli kwani kuna watoto wengi sana ambao wamezaliwa ndani ya ndoa na hawana maadili mema rekebisha usemi wako wa kuwadharau watoto waliozaliwa nje ya ndoa wewe mwenyewe una uhakika gani kama umezaliwa ndani ya ndoa? Pengine mama yako alitembea na mwanaume mwingine akakuzaa wewe kwa sababu baba yako halijui hilo akabambikiziwa.

    Pia ndoa ni cheti tu, wengi wapo kwenye ndoa lakini hawajiheshimu, hawafati maadili ya ndoa yanavyotaka kukicha wako kwenye mabaa, nyumba za kulala wageni wakitoa uroda kwa wanaume mbalimbali na wala hawana muda wa kuzungumza na watoto wao na huyu dada ambaye hayuko kwenye ndoa akawapa matunzo na maadili mema watoto wake.

    Dada usivunjike moyo watunze watoto wako na uwapende, ndoa hailazimishwi siku ikifika utampata wa kukuoa na hata usipompata endelea kujiheshimu wanaume kama hao wanataka kutumia nafasi hiyo ili wakupotezee muda wa kukaa na watoto wako na kuwapa matunzo yanayostahili.

    ReplyDelete
  32. pole sana mdada. Najaribu kufikiria kwa nini mkaka huyo alikuita kwa room na hisi labda ndipo alipokuwa anafanya kazi kwa muda huo. Lakini je ulijaribu kuuliza mapokezi kama yeye kaingia kama nani mule ndani ya hotel?. Namna nyingine ya kufanya mtext kumuomba miada then ndo umuulize alikuwa anasemaje kwa siku aliyokuuita kwa hotel

    ReplyDelete
  33. Hii kali hii dah...dada zetu tunawaita mazigo...eti zigo limejileta lenyewe...damn...gender communities ziko wapi????? Im feeling like crying...mfffffhaa!

    ReplyDelete
  34. Hivi wewe dada chizi??? Halafu nyie watu wengine mnao msapoti huyu dada kweli mko sawa? Angalia stori yake ana watoto wawili, kwanza kawapate hatujui, labda kawapata kwa njia hii hii ya kuitwa hotelini, huwezi kuniambia siku zote jamaa anachombeza wewe hujui anachotaka, yeye dhahiri anashida kwanini usingemwabia aje upatakako??? au ulikuwa unabeep?? Isitoshe umeitwa Hotelini unategemea nini? Kula Chips au? Tena unabahati ungebonywezwa vizuri...

    ReplyDelete
  35. HUYU ALITAKA KUANZISHA MJADALA HUMU NDANI KWA KUSEMA KUWA HAJAINGIA. UKWELI NI KUWA ALIINGIA NA OFCOURSE WALIFURAHIA KUWA MLE NDANI YA 505.PERIOD!

    ReplyDelete
  36. Dada kwa ushauri tu next time usiende kama ukibahatika kuitwa tena, na huyo jamaa si mtu mzuri kwa nini ajifiche ndani ina maana ana wengi zaidi ya wewe pia uwe macho sana anaweza akakutumua mtu mwingine aje kukutongoza kupitia mtu mwingine. Angalizo mimi sikushauri vibaya endelea kutunza watoto wako mungu ni muweza atakupa mwanaume mzuri mwenye kheri na wewe.

    by monac7777@yahoo.com

    ReplyDelete
  37. We mwenyewe mzinifu hadi umezaa nje ya ndoa, bora ungesema uliolewa halafu ukaachika. Hivi msomi mzima na mama wa watoto unashindwa wawili unashindwa kujua alichokuitia? Na wewe mdau unaeringia PhD mbona zipo za kuokota tu na wala PhD haitokani na kutongozwa au kutokutongozwa

    ReplyDelete
  38. Wewe sexologiste (sexologist?), Naona ndo wale wale akina midomo mizito maana hata email (danielmtanda@yahoo.com)umeitoa hapo juu eti uandikiwe, kumbe nawe unataka kutumia gear hiyo kutongoza kizamani. Mwombe michuzi akutumie email iliyotumika kumletea article hii.

    Dada naye alienda ku test zali. Maana hawa wasioweza imba mashairi kwa kuhonga hawawezekani. hivyo asitake kuongopa hapa, alikuwa disappointed ndoo maana anaandika hapa.

    ReplyDelete
  39. hana lolote cheaaaaaaaaaap

    yeye kashasema ni mtu mzima na ana maamuzi yake Haya kwanini asiende chumbani kisha tuone kama maamuzi yangekuwa yake au la.

    huna watoto 2 nje ya ndoa kisha unataka uambiwe i love you.hakuna hatayekutongoza kwa aina hiyo,wewe ni wa kushika mkono tu na kuelekea chumba cha sindano.

    ReplyDelete
  40. Huyo kaka anaonekana alikuwa haana nia nzuri na wewe kwani ulivyommwambia upo mapokezi alishindwa kushuka na ungeenda huko cha moto ungekiona poleeeeeeeee sana

    ReplyDelete
  41. huyu jamaa amezoea kurukia ndo maana aliona rahisi. Cha msingi watu wajitambue tu hii khali ya maiisha sio kama zamani kurukia na kurukiwa hovyo ukida ngoma ndo tamati yako. TUBADILIKE!!

    ReplyDelete
  42. JAMANI EEH MSIDANGANYIKE JAMAA MWENYEWE NAMJUA FIKA KANIPA STORY YOOTE JINSI ILIVYOKUWA NA NIMEMPAKA VILEVILE JUU YA USHAMBA WAKE. HIZO COMMENT ZOTE ZA KUMPAKA HUYO ETII CHEEEAP SIJUI NINI KAZIANDIKA MWENYEWE. NI RAFIKI YANGU LAKINI ZOBA NA MAZOBA WAKO WENGI HUMU. NI KWELI MTAKUFA SIKU SI ZENU SI KILA KING'AACHO NI DHAHABU. WAKWARE WAKUBWA NYIE

    ReplyDelete
  43. JE NA WEWE HUU NDIO USOMI WAKO KULETA UPUUZI WA HUYO JAMAA KWENYE BLOGU? UNA UHAKIKA GANI KUWA YEYE HASOMI KATIKA BLOGU HII PIA.



    KWA NINI SHULE YAKO ISIKUFUNDISHE NAMNA YA KUWASILIANA NAYE MWENYEWE AU MKIWA NA MWINGINE ASIPOSIKIA ILI UMPE USHAURI NASAHA KISOMI.

    TUNAKUSHUKURU KWA UTUNZI WA HII HEKAYA

    ReplyDelete
  44. Huyu dada anatuzengua tu hapa. Keshakanyagwa huyu. Na pengine kagundua jamaa yuko +ve sasa anahaha! Machangudoa bwana!

    Watoto wawili tena wasio na baba bado hujui mwanaume anapokuita hotelini anataka nini? Please!

    ReplyDelete
  45. We dada usituyeyushe kwanza umesema una watoto wawili halafu hujaolewa hii inamaanisha haya mabo unayapenda saana nadhani kilichokufanya usipande juu chumbani ni kwamba hukutangaziwa mapema dau itakuwa shilingi ngapi.
    namshauri huyo bro atangaze kabisa dau nadhani bidada utanyamaza na hutatupotezea muda hapa ktk blog yetu.

    Dada huna ugeni kabisa na mabi haya.

    ReplyDelete
  46. mjinga nini wewe, unajifanya hujui kilicho kuwa kinaendelea. acha kujishaua huna lolote. kwa nini usinge kataa kwenda hotelini. u r desparate, unaongea kama mtoto wa miaka kumi. kwenda zako u r just desparate. we lea watoto wako. kwani hao watoto uliwa pataje?

    ReplyDelete
  47. Ukisikia wanawake wanakuwa raped ndo kama hapa. Ungeingia tu chumbani ungebakwa halafu kama watu wanavyosema hapa ni kwamba mlikuwa mmekubaliana. Ushaidi upo tu tosha na mawasiliano ya simu na a kila kitu. Be careful

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...