Ankal akionesha wasanii namna Youtube inavyofanya kazi wakati wa mkutano wa kila Jumatatu wa Jukwaa la Sanaa katika ukumbi wa BASATA Ilala Shariff Shamba jijini Dar. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Utafiti, Habari na Mafunzo wa BASATA Bw. Godfrey Mungereza Lebejo
Kiongozi wa Kilimanjaro Band 'Wana Njenje'
Waziri Ally akichangia mada ya libeneke

Mmoja wa wasanii akitoa yake ya moyoni
Wasanii wengi wanahudhuria Jukwaa
la Sanaa kila Jumatatu ukumbi wa BASATA

Na Aristides Kwizera wa BASATA
Ankal amewashauri wadau wa sanaa hasa wasanii kuanza kuingia kwa kasi kwenye matumizi ya teknolojia hiyo kwani ni njia kubwa ya kujitangaza na kuuza kazi za sanaa kote duniani. Mwenyewe anaita kuendeleza Libeneke.

Akizungumza kwenye Jukwaa la Sanaa jana katika ukumbi wa BASATA huku Ilala Shariff Shamba jijini Dar, Ankal aliweka wazi kwamba blogs zimekuwa zikitembelewa na watu mbalimbali duniani hivyo wasanii hawana budi kuzitumia ili kujitangaza, kusambaza kazi zao na hata kujitambulisha katika masoko ya kimataifa.

Alisema kwamba, blogs tofauti na aina nyingine za vyombo vya habari inatumiwa kuhifadhi picha nyingi na kazi mbalimbali, kupata taarifa kuhusu tasnia ya sanaa, kupokea mawazo ya wateja wa kazi za sanaa na hata kuwa na wasaa wa kuwasiliana na wasanii wengine na hivyo kupanuka kimawazo na kiujuzi.

Akizungumzia historia ya blogs,Michuzi alisema kwamba ni teknolojia mpya hapa nchini na kwamba,ilianza kwa kuandika habari za kawaida lakini leo hii ni tegemeo katika kupasha habari kwa uharaka zaidi, kuwafikia watu wengi kuliko vyombo kadhaa vya habari na kimbilio la jamii kwani imekuwa kama sehemu ya jamii katika masuala mbalimbali.

Kwa ujumla Michuzi aliwataka wasanii na wadau wa Sanaa kuamka na kuanza kutumia teknolojia hiyo kwani wasanii mbalimbali duniani si tu wamekuwa wakitumia blog katika kujitangaza na kutambulisha kazi zao bali pia wamekuwa wakimilki mitandao na technolojia mbalimbali za mawasiliano.

Katika kuonesha kwamba teknolojia hiyo ni muhimu Michuzi ameahidi kuwapa mafunzo ya bure wadau wa Jukwaa la Sanaa juu ya kufungua na kumiliki blog ambayo yataendeshwa Ijumaa ya Desemba 10,2010 kwenye Ukumbi wa BASATA.Wadau wote wa Sanaa mnakaribishwa.
Pitia intavyuu ya Ankal katika BabKubwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Safi mara moja moja kuelimishana ni jambo la msingi ila waelimishwe na haki zao za msingi ikiwa pamoja na sheria za mirahaba.

    ZAUNUNU-AMSTERDAM

    ReplyDelete
  2. Oyaa Dollarman acha kuwapiga watu kamba.

    ReplyDelete
  3. mimi shati la ankal tu nilidhani bustani ya mnazi mmoja

    ReplyDelete
  4. Asalaam alaykhum ancal,

    Hongera sana kwa darasa ulilotoa naimani wameelewa na watayafanyia kazi. Ukweli muziki unahitaji kujitangaza sana kazi ya msanii haitoshi kujitangaza katika TV au Radio station tu libeneke linasambaa dunia nzima kwahiyo ni njia bora sana ya kujitangaza ili kupanua uwigo wa soko.

    Thanks wajina

    Chef Issa ( MDGSCA)

    ReplyDelete
  5. Big up Ankal, sote tumefata nyao zako na mafanikio yanaonekana, naimani somo ulilotoa wameelewa na watafanyia kazi ili watangaze sanaa yao.

    Asante sana libeneke lisonge mbele

    Chef Issa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...