JK akiweka sahihi kwenye kitabu cha maombolezo cha msiba wa Hayati Elvis Musiba, mtunzi wa riwaya na kiongozi wa wafanyabiashara aliyefariki jumapili iliyopita kwa saratani ya mguu jijini Dar Jumapili iliyopita. Shughuli hii imefanyika jioni hii katika viwanja vya ukumbi wa Karimjee kabla ya kusafirishwa kwenda kwao Musoma
JK na Mama Salma Kikwete wakitoa
heshima za mwisho kwa Hayati Elvis Musiba

JK akimtambulisha Mama Salma mgombea urais kwa tiketi ya chama cha TLP Mh.Muttamwega Mgahywa ambaye pia alikuwepo kwenye shughuli hii.
Hayati Elvis Musiba atakumbukwa na wapenzi wa riwaya za stelingi Willy Gamba katika vitabu kadhaa alivyotunga kama vile Kikosi cha Kisasi, Nitakufa naye na kadhalika. Pia alikuwa mwenyekiti wa chama cha wakulima na wafanyabiashara (TCCIA)




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Nimesoma vitabu vyake sana nikiwa std 5, 6 and 7 . Nakumbuka dada yangu alikua secondary na alikua anavinunua sana na mimi nilikua navisoma halafu usiku silali basi mama alikua anamwambia dada yangu uvifiche asivione. Na mpaka sasa nakumbuka hizo hadithi..

    RIP

    Forever gone but your legacy will always stay with us...

    ReplyDelete
  2. Thank you Mr. Musiba for making my youth bearable. I used to read your books with my brother, you made us close. I will treasure the memories forever.

    ReplyDelete
  3. rest in peace musiba, jamani vile vitabu acheni tu njama, kikosi cha kisasi, kufa na kupona nk, vilikuwa kama movie za kina james bond kweli tutakukumbuka daima, kapumzike kwa amani

    ReplyDelete
  4. .......Aiseh ! mwenyezi Mungu amrehemu, wakati nasoma vitabu vyake nilikuwa najiuliza hivi kuna mswahili anaweza kuandika vitabu vikali namna hii! Naamini vitabu vyake vinaweza kutengenezwa sinema (MOVIE).......kwakweli amenifanya nashindwa kusoma vitabu vya wandishi wa sasa, hakuna utamu unaweza kuupata kuulinganisha na yeye. Pengine kitabu cha mwisho baada ya vyake kilichonivutia ni cha EDDY GANZEL (Kijasho chembamba)basi!!

    ReplyDelete
  5. .....Nashauri familia ijaribu kuona kama vile vitabu vinaweza kutengenezwa movie, tena level ya Hollywood!Pengine inaweza kusaidia dunia kuona mchango wetu wa ukombozi kusini mwa Afrika.

    ReplyDelete
  6. Ushauri wa Movie ni mzuri ili swala hili si kwa wanafamilia tu hata wewe mchangiaji mada unaweza kulitekeleza. Unaweza omba rights za hadithi (mwenye rights anaweza kuwa publisher na si mwanafamilia) kuandika script then unaweza kutafuta funds za kutengeneza movie. Tuwache jadi yakufikiria wengine tu ndio watafanya.

    RIP Musiba, mimi definately nitatafuta rights za ebooks.

    ReplyDelete
  7. Rest in peace Elvis you have been the great guy and very helpful in anyway Amen

    ReplyDelete
  8. Hakika aliweza kufikisha fasihi vyema.pumzika kwa amani.Amen

    ReplyDelete
  9. Rest in Peace Kaka Elvis Musiba.

    We'll remember you forever for those Willy Gamba aka. The Black James Bond stories.

    ReplyDelete
  10. Musiba umeacha pengo ambolo litachukua mda kuliziba!RIP you will be always be the greatest!!

    ReplyDelete
  11. RIP Elvis Musiba is had to believe you are gone. Pole nyingi ziwafikie familia yako, haswa wanao Lisa,Zumbi, Evans na wengine wote. Nephews zako Festo, Elias na mkubwa wake Festo i dont remember his name. Utakumbukwa daima kwa mchango wako wa vitabu kwa jamii.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...