
Aliekua mshiriki wa Tusker Project Fame,Aneth Kushaba akiongea na kutoa shukrani wa wadau wa SBL pamoja na Watanzania kwa ujumla waliokuwa wakimpigia kura katika shindano hilo mpaka kufikia hapo alipofikia na kuwashauri Watanzania waweze kumpigia kura mshiriki Mtanzania aliebaki katika kinyang'anyiro hicho kinachoendelea huko jijini Nairobi nchini Kenya.Aneth aliyasema hayo muda mfupia mara baada ya kuwasili nnchini kwa ndege ya Kenya Airways jioni hii katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa J.K. Nyerere.

Meneja wa Bia ya Tusker,Nandy Mwiyombella akizungumza jioni ya leo wakati wa kumpokea aliekuwa mshiriki wa Tusker Project Fame,Aneth Kushaba (shoto) katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa J.K. Nyerere jioni hii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...