MAREHEMU HASSAN M.MBULALINA (1946-2010)

Familia ya marehemu Bw.Hassan M.Mbulalina, tunatoa shukurani zetu za dhati kwa wote waliojitokeza kutusaidia na kutufariji wakati wa kumuuguza na hatimaye katika kipindi cha msiba wa baba yetu mpendwa aliyefariki 30/09/2010 na kuzikwa 1/10/2010 mjini Dodoma.
Familia inawashukuru madaktari na wauguzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road kwa juhudi walizofanya kunusuru maisha ya baba yetu.

Aidha familia inatoa shukurani za pekee kwa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (NAO). Kwa kuwa si rahisi kumtaja kila mmoja hivyo basi tunaomba wote mpokee shukurani zetu za dhati na Mungu awajalie mafanikio katika shughuli zenu za kila siku.
Arobaini itafanyika 14/11/2010 nyumbani kwa marehemu kilimani-Dodoma.
“INNALILAH WAINALILAH RAJIUN”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. jamani poleni kwa msiba wahusika, michuzi lete matokeo ya uchaguzi bwana nini lakini...au machozi yanakulenga ccm inaelekea kubaya...huku nje hatuoni local news,tunakutegemea habari motomoto utupatie bwana ah!

    ReplyDelete
  2. wewe mtoa maoni wa hapo juu jaribu kuheshimu msiba wa wenzako ..usiandike masuala ya uchaguzi wa kipumbavu kabisa kupitia msibani wewe mjinga mmoja na huko kuweko nje usione ni kitu kikubwa au cha ajabu

    wenzako tumeshakaa huko na tumerudi kwetu wewe usijigambe kukaa nje wewe ni mtumwa tu na utabakia kuwa mtumwa wa watu

    kwani huna tabia wala heshima mjinga mkubwa wewe

    ReplyDelete
  3. huyo jamaa kweli kakosea, hapo suala la uchaguzi haikuwa sehem yake lakini haikuwa na haja ya kutoa matusi yote hayo kwani inaonesha ujinga wa huyo mtoa matusi,huu uchaguzi sio wa kipumbavu kama ulivyosema,ungemrekebisha tu.tunaombwa tusibadilishe mada jamani bado tunamsikitikia mzee wetu.

    ReplyDelete
  4. yani mi nadhani huyo wa kwanza ni jini labda,manake katika hali ya kawaida huwezi ukaunganisha mautumbo yako ktk swala la msiba.he or she is stupid.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...