Afisa Utetezi wa UAM,Anna McCartney-Melstad akizungumza katika mkutano na wahariri wa habari uliofanyika katika ukumbi wa DICC ndani ya jengo la PPF Tower.
Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF,Said Kawembe akifungua mkutano huo.

Ili kuhakikisha wachezaji wa timu ya Kilimanjaro Stars wako imara na wana afya bora wakati wa mashindano ya CECAFA, TFF itawalinda wachezaji hawa dhidi ya ugonjwa hatari wa MALARIA.

Hivi karibuni wakati wa mazoezi yakujiandaa na mechi kati ya Liverpool na Chelsea, mwili wa mchezaji Didier Drogba ulipoteza nguvu kwasababu ya ugonjwa wa MALARIA na akashidwa kucheza mechi hiyo. Cha kushukuru ni kwamba dalili za MALARIA ziligundulika mapema, akatibiwa na sasa amepona anaendelea kucheza kama kawaida.

Sasa timu ya Chelsea, kwa kushirikiana na mshirika wao mkuu wakutoa misaada “Right to Play” wameamua kuusaidia kampeni ya United Against Malaria (Tushirikiane Kutokomeza Malaria). Kampeni ya Tushirikiane Kutokomeza Malaria unajumuisha viongozi maarufu, wanasiasa, mashirika mbalimbali na wachezaji maarufu. Watu hawa waliungana pamoja kabla ya mashindano ya Kombe la dunia-Africa ya Kusini ili kupigana vita dhidi ya ugonjwa wa MALARIA unaoua mtoto mmoja wa Afrika kila baada ya sekunde thelathini.

CECAFA imechukua kampeni ya Tushirikiane Kutokomeza MALARIA kama kauli mbiu yao kwenye mashindano ya mwaka huu.

Kuhakikisha ugonjwa hatari wa MALARIA haushambulii kambi ya Kilimanjaro Stars, TFF itagawa neti za kuzuia mbu wa MALARIA kwa kila mchezaji katika kambi yao. “Kuanzia sasa sisi TFF tutaanza kupanga utaradtibu wa kupambana na MALARIA tukishirikiana na UAM na wa Watanzania wenzetu” alisema Sunday Kayuni. Neti hizi zitakazotolewa na TFF zimetolewa na kampuni ya AtoZ.

Nae mchezaji Didier Drogba alisema “Neti ya mbu inaweza kuonekana kama kitu kidogo lakini neti huweza kuokoa maisha ya watu wakiwa wamelala kutokana na mbu waambukizao MALARIA. Neti ni muhimu sana kwenye nchi ambazo zinasumbuliwa na ugonjwa hatari wa MALARIA”.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mimi bado sijaelewa ni vipi watu wawili walio chumbani mmoja akiwa amelala na mwingine ameketi akijisomea mbu anamuacha aliyeketi na kumuuma aliyelala au akimuuma aliyeketi hatamuambukiza malaria bali atakayeambukizwa ni yule aliyelala! Bado ninaamini kuwa kuwauwa mbu huko waliko kwenye mazalia yao ni muhimu zaidi kwanza kisha chandarua. wataalamu nielewesheni mimi.

    ReplyDelete
  2. huyo jamaa anaitwa SAAD MAARUFU KAWEMBA

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...