WASANII JITOKEZENI TUPIGE VITA UKIMWI!

Pichani kushoto ni Prodyuza Braton (Backyard Records).

Napenda kumshukuru Mungu kwa kuendelea kuwa hai mpaka sasa.
Pia nawashukuru watanzania wenzangu kwa kushiriki na kufanikisha uchaguzi wetu mkuu. Masikio yalikuwa hoi sana kusikia habari za uchaguzi uchaguzi mpaka tumehitimisha kwa huru na haki ya kidemocrasia.

Shukrani zangu za dhati kwa media zote kwa kupoteza muda, mali hata kuatarisha afya zao ili hali kuhakikisha ujumbe na kampeni za uchaguzi zinatufikia. Shukrani za pekee kwa wasanii wote walio shiriki kwa njia moja au ningine kuhakikisha kila mtu anajua maana ya democrasia ya uchaguzi. Naamini kwa kupitia wasanii ujumbe umefika sana kwa kiwango walicho fanya na mchango umeonekana na naamini heshima lazima iwepo kwao.

Kwa kuzingatia hilo Backyard Studio tulitoa nafasi kwa wasanii kurecords bure nyimbo zinazo husu uchaguzi mkuu kuanzia tarehe 01/07/2010, mpaka week ya uchaguzi mkuu, nashukuru wito ulitimia kwani tulirecord nyimbo zaidi ya hamsini.

Wasanii tunaweza, kwa niaba ya Backyard Studio naomba nitoe tena fulsa ya pekee kwa Wasanii wote nchini iwe vikundi au mmoja mmoja kurecord nyimbo BURE kuanzia tarehe 30/11/2010 hadi tarehe 09/12/2010. Nyimbo hizo ziwe mahususi kwa ajili ya kusaidia, kuhamasisha jamii na kuelimisha kuhusu janga la Ukimwi linalo tukabili.

Dhumuni la Backyard kwa sasa ni kusaidia Jamii katika Majanga yote ya kitaifa kwa kupitia Sanaa. Tunaamini Ukuimwi ni moja ya Janga kubwa sana linalo pelekea Serekali na Jamii kutumia pesa nyingi, muda na maarifa katika kutaka kuogoa maisha ya ndugu na jamaa zetu sambamba na kutokomeza gonjwa hili. Wasanii ni watu muhimu sana na naamini wakiamua kupiga kampeni hii ujumbe utafika na yote haya yana wezekana.

Naomba nyimbo ziwe za kweli zenye uwezo wa kukaa kwa muda mrefu zaidi na ambazo zitavutia jamii kusikiliza na ujumbe kuwafikia pale walipo ndani ya kipindi chote si wakati wa maadhimisho haya tu.

Tuwasiliane hii ili tupeane utaratibu wa kufuata japo hakuna mashari. Ahsante

Braton (Backyard Records)
S.L .P 14663 D'Salaam
Tanzania
+255 713 888 779.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Big up sir-Unajitoa kwa jamii.
    In return mungu atakupa baraka.
    Pia u have a chance kupata wasanii wazuri utakaoweza kufanya anao biashara ya music na hivyo kufanikiwa ktk malaengo yako
    nice heart and da best strategy

    ReplyDelete
  2. I wish ningekuwa bongo na mimi nirecord wimbo wangu kuhusu Ukimwi, well done guys for such a great project, wasanii wasio record nitawashangaa opportunity kama hiyo sio mchezo.
    Mungu awabariki saaaana Backyard Studios, sio wengi wenye moyo kama huo, watu wengi wametanguliza pesa mbele

    ReplyDelete
  3. Mungu awabariki sana, tutawasiliana kuona tunaunga mkono Backyard Studio. Naamini hata serikali inabidi iwafikirie na kutoa surpot ili ujumbe ufike. Vip kuhusu malaria? Je Backyard mnalionaje hilo! Naomba email yenu ps- James UK

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...