Umoja wa watanzania Ujerumani ukiwa katika picha ya pamoja na Mhe Balozi wa Tanzania Nchini Ujerumani,Mh. Ahmada Ngemera. Kushoto ni Mhe Mwenyekiti wa Umoja huo. Na kulia Ni Mhe Katibu wa Umoja huo.Viongozi wa muda wa umoja wa watanzania Ujerumani. kushoto Mhe Katibu wa Umoja Bi Tulalumba Mloge wa pili kushoto Mhe Mwenyekiti wa Umoja Bw Mfundo Peter Mfundo, katikati Mhe Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mh. Ahmada Ngemera, Anayefuata ni Mhe Makamo M/Kiti Mhe Xavier Komba Na mwisho kulia Ni Muweka Hazina Bi Nashe Mvungi Picha ilipigwa mara baada ya kuchaguliwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Hii ndo inatakiwa - siyo kuanzisha sijui tawi la Chadema, CCM, CUF. Lengo liwe ni kuunganisha watanzania nje ya nchi na si kubaguana kwa itikadi.

    ReplyDelete
  2. Nashe itabidi nikutafute nikusaidie kuweka hizo pesa

    ReplyDelete
  3. Nimefurahi sana kuona hili tangazo mm ni mtanzania ninaishi germany nitawapataje nami nijiunge plz nahitaji hiki kitu

    ReplyDelete
  4. Hongera sana.Jamani ninamtafuta rafiki yangu ambaye sijamuona miaka sasa.Watu wa ujerumani naomba msaada wenu.Winnie Mbugu ninakutafuta.Olease wasiliana nami kwa mail:muhanga333@hotmail.com.Tuliishi wote Lumumba street Dar.Niko Norway rafiki yako nilikuwa nikifanya kazi posta house na wewe Tanesco.

    ReplyDelete
  5. Hao ni familia ya wanaofanya kazi ubalozini na rafiki zao. Hawawakilishi Watanzania wote wanaoishi Ujerumni. Hao wanaishi Berlin tu.

    ReplyDelete
  6. KAZI NZURI SANA. HII NDIO TUNATAKA KWA WATANZANIA TULIO NJE "UMOJA WA WATANZANIA" NA SIO WANA CCM, CUF SIJUI CHAMA CHA MAENDELEO. N.K
    JOB WELL DONE

    ReplyDelete
  7. Huu ni umoja wa watanzania wa ukweli kabisa na una nia njema kabisa, Na sio wa Ubalozi wala nini, Ubalozi upo Berlin na wanachama wamekutana Frankfurt angalia Ramani hapo uone umbali ulivyo. Watu wote wapo Positive Hapa. Watanzania Ujerumani subirieni Matunda ya umoja

    ReplyDelete
  8. wewe anony wa Nov.29.03:59:00PM
    Usikulupuke tu na kutoa maoni pumba,na kuleta mawazo vinyu katika jambo la heri.Kwa taarifa yako huu ni umoja wa watanzania Ujerumani,unaowakilisha watanzania katika kila pembe hapa ujerumani,sio Berlin tu.Viongozi wa Umoja huu sio marafiki sio ndugu wa familia fulani au kabila fulani.
    Mhe.Balozi Ngemera ametushauri watanzania lazima tuungane na kushikama na umoja ni chombo pekee cha kuleta nguvu kwa watanzania hapa ujerumani.
    Sasa mwenzetu huoni umuhimu wa umoja huu.kwa kuwa mmshezoea vyama vyenu vya kuomba omba na kuchangisha misaada!
    Jaribu kuwa makini na kuelemika unapotoa maoni.
    Kamanda wa FFU
    Ughaibuni

    ReplyDelete
  9. jamani na mimi ni mtanzania ninaishi ujerumani, Berlin. toka nifike sijakutana na Mtanzania hata mmoja, Je nitajiungaje na umoja huu. email yangu ni ninaa857@gmail.com. ahsanteni

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...