Meneja Miradi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Clayton Kimber (kulia) akimuonesha moja ya miradi inayoendelea kujengwa katika kiwanda cha TBL, Dar es Salaam, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya SABMILLER Plc, Graham Mackay (katikati) anayemiliki zaidi ya viwanda 60vya bia Duniani. Mackay anayeishi Uingereza alitembelea Kampuni hiyo leo kuona utendaji kazi. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa TBL, Robin Goetzsche.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya SABMILLER Plc, Graham Mackay (kushoto) anayemiliki zaidi ya viwanda 60 vya bia Duniani, akizungumza na Mpishi Mkuu wa bia za Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Gaudance Mkolwe baada ya kuitembelea kampuni hiyo leo jijini Dar. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Masoko wa TBL, David Minja (kulia) pamoja na Trevor Gray ambaye ni Mkurugenzi wa Ufundi wa TBL.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya SABMILLER Plc, Graham Mackay anayemiliki zaidi ya viwanda 60 vya bia Duniani, akiangalia bia aina ya Castle alipotembelea kiwanda cha TBL, Dar esSalaam leo.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...